• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewataka wananchi wote kuyatunza mazingira kwa sababu mazingira yanatabia ya kumtunza anayeyatunza mazingira.

Posted on: January 30th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewataka wananchi wote kuyatunza mazingira kwa sababu mazingira yanatabia ya kumtunza anayeyatunza mazingira.

Mwenda ametoa wito huo mwishoni mwa juma hili wakati alipokuwa katika Bonde la Wembere kupanda miti ya gundi wilayani Iramba.

“Ndugu zangu fahamuni kuwa mazingira huwa yanatabia, ukiyatunza yanalipa fadhila na ukiyaharibu pia yanakulipa fadhila.” Alisema Mkuu huyo wa wilaya

Aidha, aliongeza kuwa moja ya majibu yanayotokona na kuyaharibu mazingira ni kuadimika kwa mvua na kujikuta nchini katika maeneo mbalimbali watu wanaangaika pamoja na kuomba maombi ili Mungu alete mvua.

Halikadhalika, alibainisha kuwa yapo mambo ambayo yamewekwa kikanuni kwamba ili mwanadamu apate mvua ni lazima awe na miti ambayo inasaidia kuwepo kwa mvua.

“Nitoe wito ndugu zangu tupande miti, tuitunze na kuilinda ili ikistawi iweze kutuletea mvua.” Alisema

Ni hakika kila mtu anategemea mvua kwa sabubu uwepo wa mvua ndio unasaidia wakulima kuweza kulima na kupata chakula ambacho hufukuza njaa, hivyo ili kuikimbiza njaa ni lazima tuitunze misitu yote.

Kufuatia upandaji wa miti unaondelea wilayani hapo, Mkuu huyo wa wilaya amewataka wafugaji na wakulima wote kuwa wahakikishe wanatunza misitu hiyo kwa sababu ikiwa hawatatunza watachukuliwa hatua kali za kisheria.

“Ndugu zangu siwezi kuona zaidi ya milioni mia mbili (200,000,000) zimeingizwa katika mpango huu na serikali kupanda miti zinaharibika kwa sababu ya watu wachache wasiotakakufuata sheria na kanuni tulizojiwekea, nitakuwa mkali mimi pamoja na kamati yangu ya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na TFS  kuwachukulia hatua.” Alionya Mwenda na kuongeza kuwa

“Wapelekeeni ujumbe watu wote kuwa miti hii tumepanda ni kwa manufaa yetu sio kwa manufaa ya watu wengine, hivyo tuitunze ili itutunze.”

Awali akitoa taarifa fupi wakati wa zoezi lakupanda miti likiendelea Meneja wa Wakala wa Misitu Tanzania wilayani hapa, Shabani Nyamasagara alisema kuwa tayari wamekwisha panda miti laki mbili (200,000)  katika hekari 500 na kubakiwa na miche 50 ambayo itapandwa kukamilisha hekeri 625.

Nyamasagara alisema kuwa wanapanda miti katika hifadhi ya msitu wa Wembere kwa sababu hapo awali ulikuwa na miti ya migunga ambayo ilikuwa inazalisha gundi lakini misitu hiyo iliharibiwa.

Pia alisema wanapanda miti hiyo ikiwa ni jitihada za kurudisha uoto wa asili pamoja na kupambana na uharibifu wa mabadiliko ya tabia ya nchi.

“Mheshimiwa Mkuu wa wilaya pamoja na zoezi hili lakupanda miti pia TFS imezalisha ajira ya zaidi ya watu mia moja (100) kwa kila siku hasa katika kipindi cha kuotesha miti na wakati wa kupanda miti.”

Aidha, aliongeza kuwa wanaiomba jamii zinazoishi pembezoni mwa hifadhi hizo kuona kuwa uwepo wa misitu hiyo ni sehemu ya kutengeneza ajira kwa vijana na kuweza kujipatia kipato.

Kwa upande wake diwani wa Kata ya Urughu, Simon Tyosela aliomba kuwa msitu huo wanaoupanda kuwa endelevu kwa sababu unasaidia kutoa ajira.

Pia alimuomba meneja wa TFS kuhakikisha kuwa msitu huo uwe na wale wadudu wanaosaidia kuzalisha gundi ili gundi ipatikane kwa wingi.

Naye mmoja wa wananchi ambaye anaishi pembezoni mwa hifadhi hiyo, Shabani Juma aliwaomba wananchi wenzake kuwa watunze miti ya Migunga ambayo wanaipanda kwa sababu miti hiyo itawasidia hapo baadaye.

“Kwa kweli nipo hapa katika zoezi la kupanda miti nikijivunia kuwa miti hii itanisaidia baadaye pamoja na kuboresha mazingira, hivyo natoa wito kwa wananchi wenzangu kuwa tuyapende mazingira yetu yatatusaidia baadae.” Alisema

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.