• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda aiagiza TAKUKURU Wilayani humo kumkamata na kumuhoji Mwenyekiti wa Kijiji cha Lutamla kufuatia madai ya kuchukua fedha za Wananchi 9.5 milioni.

Posted on: August 25th, 2021

Hemedi Munga Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amemuagiza Kamanda wa TAKUKURU, Ahmed Sungura kumkamata na kumuhoji Mwenyekiti wa Kijiji cha Msai Kata ya Mtoa Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Mwenda ametoa agizo hilo leo Jumanne Agosti 24, 2021 punde baada ya kusikiliza kero ya Wananchi alipotembelea kijijini hapo.

Akitoa kero kwa niaba ya wananchi wa kijiji hicho mbele ya Mkuu huyo wa Wilaya, Mwenyekiti wa kitongoji cha Lutamla, Ngasa Kasema, amewasilisha kuwa Wananchi wa kitongoji hicho wanalalamikia fedha zao walizochanga mwaka 2018 kwa ajili ya kuwekewa alama za utambulisho wa mipaka katika ardhi (beacon) ili kutambulisha eneo la malisho na ulimaji la wanakijiji hao.

Ameainisha kuwa Wananchi hao walichangishwa kila moja takribani laki tano (500,000) kwa watu kumi na tisa (19) na kufanya jumla ya Tsh  milioni tisa na laki tano (9, 500, 000 ).

Ngasa amesema kuwa hivi karibuni kumewekwa alama za utambuzi wa mipaka katika ardhi (beacon) ndani ya makazi ya watu bila ya Wananchi kuhusishwa, hivyo kuliona tukio hili kuwa ni la kifisadi na kumuomba Mkuu huyo wa Wilaya kuutatua mgogoro huo ili wananchi wapate haki yao.

Kufuatia kero hiyo, Mkuu huyo wa Wilaya, akatoa agizo kwa TAKUKURU kumkamata Mwenyekiti wa Kijiji hicho pamoja na kila aliye husika katika kuchukua fedha hizo kuwahoji ili kuhakikisha haki ya wananchi inarejeshwa kwa Wananchi.

“Niagize kuwa mpaka kufikia tarehe 15 Septemba mwaka huu fedha za hawa Wananchi ziwe zimerudi na mimi nitarudi tarehe hiyo hapa kwa ajili ya kikao” amesisitiza Mwenda

Katika hatua nyingine Mwenda amewataka wananchi hao kuwa na imani na Serikali inayoongozwa na Mhe, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa sababu hivi karibuni imewaletea fedha milioni mia nne (400,000,000) kwa ajili ya kujenga kituo cha Afya kata ya Mtoa, hivyo kuondoa kabisa changamoto ya upatikanaji wa huduma za Afya.

Akiongelea Zahanati iliyojengwa na Wananchi wa kijiji hicho na kuiomba Serikali kuwaunga mkono kuimalizia, Mwenda amewatoa hofu wananchi hao na kuwahakikishia kuwa Serikali tayari imeleta takribani milioni themanini (80,000,000) kwa ajili ya kukamilisha Zahanati hiyo.

Akiongea na Mwandishi wetu, Mwenyekiti wa Kijiji cha Msai, Samwel Shillah amekanusha kuwa hakuchangisha fedha yoyote kutoka kwa wananchi hao.

“Mimi sijachangisha fedha ya aina yoyote, ispokuwa kwa fedha yangu mwenyewe nimenunua simenti kwa makubaliano na serikali ya kijiji na Muhtasari ninao” amekanusha Sillah  

Kwa upande wake mmoja wa Wananchi waliohudhuria Mkutano huo, Yustina Klementi amemuomba Mkuu huyo wa Wilaya kuwasaidia kwa sababu wamekuwa wakionewa sana na Serikali ya kijiji chini ya Mwenyekiti huyo.

“Mhe, Mkuu wa Wilaya hata kero hii tunayoiwasilisha kwako nafahamu kwa tabia ya Mwenyekiti wetu atakuwa na uadui kwa aliye wasilisha kero hii, tusaidie!” ameomba Klementi

Changamoto hiyo imedaiwa kuibuka baada ya Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) kuweka alama nyingine za utambauzi wa mipaka katika  ardhi (beacon) kwa ajili ya eneo la kuhuisha msitu katika mbonde la Wembere na makazi ya Wananchi Wilayini humo.

MWISHO

Viongozi wa Kijiji cha Ujungu Wilayani Iramba wakimvika uchifu na kumuomba Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda  kuwa Mlezi wa Kijiji hicho punde alipofanya ziara Kijijini hapo. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akiagiza wananchi wa Kijiji cha Ujungu kutunza miti iliyopandwa na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) . Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.