• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akimkabidhi Mhasibu wa Chama cha Ushirika cha Wakulima wa Pamba waliodaiwa kudhulumiwa na Viongozi wa Chama hicho kijiji cha Lutamla Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba Mkoa wa Singida

Posted on: October 13th, 2021

Hemedi Munga Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Singida - Iramba. MKUU wa Wilaya ya Iramba,

Suleiman Mwenda amefanikiwa kubadhi fedha za Wakulima wa Pamaba zilizodaiwa kuliwa na viongozi wa Chama cha Msingi cha Ushirika wa Wakulima wa Pamba chenye namba za usajili SIR 3454 Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Mwenda amekabidhi fedha hizo leo Jumanne

Oktoba 12, 2021 wakati akiongea na Wananchi wa Kijiji cha Lutamla alipofanya zira kijijini hapo.

Takribani Tsh Milioni kumi (10,000,000) imekwisha kamilika ambayo itakabidhiwa kwa wananchi 178 ambao walikuwa hawajalipwa baada ya kudaiwa kuwa viongozi wa chama hicho kupata hasara.

“Ndugu zangu Wananchi baada ya uchunguzi toka kwa Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Singida, tumefanikwa kurejesha fedha hizo na leo kila mwenye risiti atapatiwa fedha zake na hakuna mwananchi ambaye atakayedhulumiwa.” Amesema Mwenda

Halikadhalika, alibainisha kuwa kwa wale ambao hawana risiti utaratibu wao unaandaliwa na watalipwa fedha zao hivi karibuni.

Akizungumza na Mwandishi wetu, Mwenyekiti wa

Kijiji cha Lutamla Kata ya Mtoa Wilayani hapo, Ngasa Ngasa alisema kuwa chanzo cha kuchelewa kulipa fedha za wakulima wa pamba kijijini hapo kinatokana na viongozi wa chama cha Ushirika huo kununua pamba na kudai kuwa wamepata hasara ya takribani  milioni Ishirini na mbili ( 22,000,000).

Ngasa amewataja viongozi hao kuwa ni Shabani Juma Mwenyekiti wa Ushirika, Stephano Msengi katibu wa ushirika na Hamisi Msengi mhasibu wa Ushirika huo.

Kwa sababu Wakulima wa pamba ndio tegemeo la zao la pamba Mkoani Singida walidai kuwa wameibiwa na viongozi hao, jambo ambalo lilimfanya Mkuu wa Wilaya hiyo kuagiza uchunguzi ufanyike na hatimaye leo wakulima hawa wanalipwa fedha zao. Aliongeza Ngasa

Kwa upande wake mmoja wa wakulima wa pamba wa kijiji hicho, Rasa Kasinili alimshukuru Mkuu wa Wilaya hiyo kwa kufanikisha zoezi la kuwagawia fedha zao na kuwaasa wakulima wenzake kuwa wazitumie fedha hizo katika kulima kilimo cha pamba katika msimu huu mpya na siyo kizitumia kunywa pombe na anasa nyinginezo zinazorudisha maendeleo yao nyuma.

“Mpaka sasa Mkuu wa Wilaya amefika hapa akiwa na fedha zetu, tunajisikia faraja kupata fedha hizo na tunampongeza Mkuu wa Wilaya.” Alishukuru Kasinili 

Naye Lameck Nyorobi wa kijiji hicho alisema kuwa wanaishukuru  Serikali kwa kutau mgogoro huo ambao ulikuwa unawanyima haki wakulima wapamba.

MWISHO.

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akitoa mrejesho wa namna alivyofanikisha kupata fedha za wakulima wa pamba ambao wanaodaiwa kudhulumiwa na Viongozi wa Chama cha Ushirika  kijiji cha Lutamla Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akitoa mrejesho wa namna alivyofanikisha kupata fedha za wakulima wa pamba ambao wanaodaiwa kudhulumiwa na Viongozi wa Chama cha Ushirika  kijiji cha Lutamla Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Ugawaji fedha za wakulima wa pamba ambao wanaodaiwa kudhulumiwa na Viongozi wa Chama cha Ushirika  kijiji cha Lutamla Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba Mkoa wa Singida ukiendelea. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.