• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda akitatua kero mbalimbali zilizowasilishwa kwake na wananchi wa Kaselya na Ndulungu

Posted on: July 27th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda akitatua kero mbalimbali zilizowasilishwa kwake na wananchi wa Kaselya na Ndulungu .

                                                     

Wananchi wa kata ya Kaselya wakisikila utatuzi wa kero toka kwa Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda. Picha na Hemedi Munga

Diwani wa kata ya Kaselya, Juma Nakwaula akiwasilisha kero kwa niaba ya wanachi wa kata hiyo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda. Picha na Hemedi Munga

Wananchi wakifuatilia kwa makini utatuzi wa kero toka kwa Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda. Picha na Sarapion Kakiziba

Diwani wa kata ya Ndulungu, Salumu Bunyongoli akiwasilisha kero kwa niaba ya wananchi kwa Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda. Picha na Sarapion Kakiziba


 Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amesikiliza na kutatua kero za wananchi zilizowasilishwa na madiwani wa kata ya Kaselya na Ndulungu.

Mwenda ametatua kero hizo leo jumanne Julai 27, 2021 wakati alipofanya ziara katika kata hizo zilizopo Wilayani Iramba Mkoani Singida.

Akiwasilisha kero za wananchi mbele ya Mkuu huyo wa Wilaya Diwani wa Kata ya Kaselya, Juma Nakwaula amesema kuwa kuna changamoto ya barabara tokea Milade, Sepuka hadi Ussure na kuomba uongozi kukamilisha ujenzi wa Zahanati ili ianze kutoa huduma.

Nakwaula amebainisha changamoto ya kupata hati za kimila ziweze kutambulika ili zisaidie katika utatuzi wa migogoro ya ardhi.

Aidha ameomba uongozi kuhakikisha kuwa dawa zinapatika kwa wananchi waliokata kadi za iCHF.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Ndulungu, Salumu Bunyongoli amewasilia kero za wananchi mbele ya Mkuu huyo wa Wilaya kuwa kata hiyo haina shule ya sekondari na uwepo wa changamoto ya barabara iendayo shule ya msingi Kipuma.

Aidha Bunyongoli amefafanua kuwa wananchi wa kata hiyo wanapata tabu ya upatikanaji wa huduma za afya kwa sababu hulazimika kuzifuata kata ya Ndago.

Akitatua kero mbalimbali zilizowasilishwa na Madiwani kwa nyakati tofauti tofauti Mkuu huyo wa Wilaya amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba imetenga fedha katika bajeti zake kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa shule ya sekondari Ndulungu.

Mwenda amewahakikishia wananchi kuwa barabara ya kutoka Kizaga hadi Sepuka ipo katika ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa sababu CCM ni chama sikivu na chenye kukamilisha ilani yake ni wahakikishie kuwa barabara hiyo itaanza ujenzi hivi karibuni na kukamilika kwa viwango bora kwa wakati.

Pia amewataka Watendaji wa Kata Wilayani Iramba kuwatambua Wazee waliopo katika maeneo yao ili waweze kupata matibabu kwa wakati katika Zahanati, vituo vya Afya na Hospitali ya Wilaya.

Aidha ameitaka taasisi ya TANESCO kuhakikisha inafikisha umeme katika shule ya Msingi Mgungia.

Katika hatua nyingine, Mwenda amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Linno Mwageni kuhakikisha anafanya tathimini ya soko la madini Ndulungu – Kipuma.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.