• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda ameahidi kutokomeza mimba za Utotoni

Posted on: July 10th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda  ameahidi kutokomeza mimba za Utotoni

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akimkabidhi vitabu vya kiada na ziada Mwalimu wa Shule ya Utayari Kisingu iliopo kata ya Ulemo Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Diwani wa Viti maalumu Wilayani Iramba, Winjuka Songelael ameahidi kutoa gunia 2 za mahindi  na sukari kilo 25 kwa lengo la kuhakakikisha wanafunzi wa Utayari Kisingu wanakunywa uji wawapo katika kituo hicho. Picha na Hemedi Munga

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Chacha Kehogo akiipongeza Serikali ya kijiji cha Kitukutu Kisingu Wilayani Iramba  kwa kufanikisha kutoa eneo lenye ukubwa wa hekari 21 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya kielimu. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akikagua kituo cha Utayari Kisingu kilichojengwa Kata ya Ulemo Wilayani Iramba kwa ushirikiano wa Shirika la SEMA na Serikali. Picha na Hemedi Munga

Furaha ya  wanafunzi wa Utayari Kisingu wakiwa na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda alipotembelea na kukagua jengo la Utayari Kisingu kwa lengo la kukabidhiwa jengo hilo. Picha na Hemedi Munga

Kutuo cha Utayari Kisingu kilichojengwa Kata ya Ulemo Wilayani Iramba kwa ushirikiano wa Shirika la SEMA na Serikali kwa garama ya Tsh 29 milioni. Picha na Hemedi Munga

Hemedi Munga, Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda ameahidi kutokomeza mimba za utotoni kwa wanafunzi na kuendelea kusimamia kwa ukaribu suala la elimu ili kuinua ufaulu wa shule zilizopo Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Mwenda ametoa ahadi hiyo leo Ijumaa Julai 9, 2021 wakati akiongea na wananchi wa Kitukutu kata ya Ulemo Wilayani Iramba katika hafla ya makabidhiano ya Kituo cha Utayari Kisingu yaliofanyika kijijini hapo.

Amewaomba wazazi kufahamu kuwa wanalojukumu la kuhakikisha malezi ya watoto wao yanakua bora na kuhakikisha wanafunzi wanatimiza ndoto zao.

“Ndugu wananchi! tuwalinde vijana wetu  kutokana na tatizo la mimba, hivyo ninakemea Wilaya nzima kuhakikisha hakuna mimba za utotoni hasa kwa wanafunzi” amesisitiza Mwenda na kuahidi kuwa

“Nimekuja kutokemeza suala la mimba za utotoni, hivyo nimuombe kila aliyopo hapa kuwa mjumbe wakumfikishia taarifa asiyekuepo hapa kuwa mimba za utotoni sasa basi.”

Amewataka kufahamu kuwa yoyote atakayethibishwa kumtia mimba mwanafunzi atahukumiwa kwenda jela miaka thelathini.

Aidha mkuu huyo wa Wilaya ametoa wito kwa wananchi kuchangia mahindi ili kuhakikisha watoto wa shule ya Utayari wanapata uji na kwa wale wa shule za msingi na Sekondari wanapata chakula.

Akisoma risala fupi mbele ya Mkuu wa Wilaya, Afisa Mradi wa Shirika la SEMA, Mauth Cosmas amesema kuwa Serikali kwa kushirikiana na Shirika la SEMA wametekeleza mradi huu wa jengo la Elimu ya Awali Malezi na Makuzi kwa hadhi ya kisasa.

Cosmas amebainisha kuwa jamii ilijitolea mchanga na mawe vyenye jumla ya Tsh 2.9 milioni huku Shirika la SEMA wakitoa Tsh 26 milioni kukamilisha kituo cha Utayari chenye hadhi ya kisasa.

Kufuatia uwepo wa kituo hicho cha kisasa kumeongeza idadi ya wanafunzi kuwa 88 ambapo 43 ni wasichana na 45 ni wavulana ikiwa ni sawa na ongezeko la 75% ukilinganisha na idadi iliyokuepo mwaka 2018.

Kukamilika na kutumika kwa jengo hili kumevutia watoto toka vijiji vya pembezoni kuja kusoma hapa, hivyo kuongeza udahili katika shule mama ya Kitukutu ambapo jumla ya wanafunzi 65 wamejiunga na darasa la kwanza mwaka 2021.

Akiongea katika hafla hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Chacha Kehogo amelipongeza Shirika la SEMA kwa kushirikiana na Serikali kukamilisha ujenzi wa kituo hicho cha Utayari.

Pia amweshukuru wananchi ambao walitoa eneo na kuwaahidi kuwa hapo patajengwa shule kadri uwezo utakavyopatika.

“Nipongeze Serikali ya kijiji iliyotoa eneo hili lenye ukubwa wa hekari 21 na niwaahidi kuwa hapa patakua na shule” ameahidi Kehogo

Naye Meneja wa Sirika la SEMA, Ivo Manyaku amegawa vitambu vya kiada na ziada kwa lengo la kuwezesha ufundishaji na kuinua taaluma kwa wanafunzi hao.


Kwa upande wake mmoja wa wazazi wa wanafunzi hao, Benard Kisuka ameishukuru Serikali kwa kushirikiana na SEMA kufanikisha ujenzi wa kituo hicho cha Utayari kijijini hapo.

SEMA wamefanikiwa kukikabidhi kituo cha Utayari kilichojengwa kwa jumla ya Tsh 29 milioni  kwa Serikali ili iendelee kukilea na kuboresha mazingira yanayozunguka kituo hicho.

Mwisho.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.