• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amegawa magodoro na vitanda kwa watoto 58 wanaolelewa na kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana kilichopo chini ya kanisa la EAGT Kiomboi.

Posted on: July 9th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akiwa katika picha ya pamoja na watoto waliogawiwa magodoro na vitanda. Picha na Hemedi Munga

Hemedi Munga, Irambadc

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akiwaasa Wazazi kuendelea kumuomba Mungu atuondolee ugonjwa wa covid 19 pamoja na kuchukua tahadhari, hivyo kunawa maji tiririka, kuvaa barakoa na   kukaa kwa kuachiana nafasi. Picha na Hemedi Munga

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Chacha Kehogo akiwatambulisha Viongozi mbalimbali walioambatana na Mkuu wa Wilaya ya Iramba,

irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amegawa magodoro na vitanda kwa watoto 58 wanaolelewa na kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana kilichopo chini ya kanisa la EAGT Kiomboi.

Mwenda amegawa vifaa hivyo leo Ijumaa Julai 9, 2021 katika viwanja vya Kanisa la EAGT liliopo Mjini hapa.

Amewataka walezi wa watoto hao kuhakikisha wanatunza vizuri vitanda na magodoro vilivyogarimu  Tsh 11.1 milioni  ili viweze kudumu kwa muda mrefu.

“Ndugu zangu ! Mungu amewachagua nyinyi katika wengi kupata msadaa huu wa magodoro na vitanda, hivyo mwende mkavitunze viweze kuwanufaisha kwa muda mrefu” amesema Mwenda na kuongeza kuwa

“Niwaombe ndugu zangu kuendelea kumuomba Mungu atuondolee ugonjwa wa covid 19 pamoja na kuchukua tahadhari, hivyo tunawe maji tiririka, kuvaa barakoa na   kukaa kwa kuachiana nafasi.”

Pia amewataka Wazazi kuendelea kuwalea watoto vizuri ili waendelee kupata elimu itakayowasaidia kupambana na mazingira mbalimbali katika maisha yao.

Akiongea katika hafla hiyo fupi, Mchungaji wa Kanisa la EAGT, Robert Kijanga amesema kuwa suala la kuwasaidia watoto yatima ambao wamepoteza wazazi wao kwa namna tofautitofauti ni suala la muhimu katika jamii yetu.

“Lazima tufanye haya kwa sababu maadili ya kimungu yametufundisha kutoa zaka na sadaka ili kupata baraka za Mungu.” Amesema Mchungaji Kijanga

Mapema akisoma historia fupi ya kuanzishwa kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana, Mratibu wa Kituo, Emmanuel Kadama amesema kuwa Shirika limejikita kuwasaidia watu wanaoishi katika mazingira magumu ili kuwakomboa katika umasikini ulio katika nyanja ya kiroho, kiakili, kimwili, kiuchumi na kijamii.

Kituo kinaidadi ya watoto  na vijana 297 wanojipatia huduma mbalimbali kwa lengo la kuwanusuru toka katika umasikini.

Aidha Kanisa limefanikiwa kuanzisha chuo cha ufundi kwa lengo la kuendelea kuwainua watoto kupata ujuzi wa kushona, ualimu wa elimu ya awali, elimu ya afya, ufundi magari, uchomeleaji na elimu ya kompyuta.

Kwa upande wake mmoja wa walezi wa watoto hao, ameushukuru uongozi wa Kanisa hilo kwa kufanikisha zoezi la kuwagawia vitanda na Magodoro.

Aidha ameahidi kuwa watavitunza vifaa hivyo ili viweze kuwanufaisha watoto kwa muda mrefu.

Kituo cha Maendeleo ya Mtoto na Kijana chenye namnba za usajili T20686 kilianzishwa mwaka 2014 kwa ushirikiano wa Kanisa na Shirika la Compassion International Tanzania lenye makao yake Makuu Jijijni Arusha.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.