• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amerudisha rasmi uchimbaji wa madini ya dhahabu Mgodi wa Sekenke one Wilani Iramba Mkoa wa Singida.

Posted on: August 2nd, 2021

Hemedi Munga Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amerudisha rasmi shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu katika Mgodi wa Sekenke one uliokuwa umefungwa tangu mwaka 2019 Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Mwenda amerudisha uchimbaji wa Madini katika Mgodi huo leo Jumatatu Agasti 02, 2021 wakati akiwa katika ziara zake za utatuzi wa kero mbalimbali kwa wananchi wa Wilaya hiyo.

“Mimi ni Msimamizi wa usalama wa raia ikiwa nimehakikishiwa kuwa wachimbaji hawa watakwenda ardhini na kurudi wakiwa salama basi sina pingamizi sasa narudisha rasmi shughuli za uchimbaji hapa” ameruhusu Mwenda

Kwa kuzingatia thamani na umuhimu wa wachimbaji wadogo wenye mchango mkubwa nchini, tunaruhusu vijana waje hapa waendelee na shughuli za uchimbaji ambazo zitakuwa zimewapatia ajira na kutimiza mpango wa serikali.

Aidha amewataka wajumbe wa Bodi ya Sekenke one kuhakikisha wanazingatia kanuni na taratibu katika uchimbaji wa duara 00 na 27 na mengine yaliokuwa salama kwa namna ya utafiti uliofanywa na wataalamu.

Pia ameionya Bodi ya Sekenke One kuto yaendea maduara 12 yaliokatazwa kutokana na changamoto anuai katika eneo hilo.

Hatua hii imefikiwa ikiwa ni utekelezaji wa agizo alilolitoa Waziri wa Madini, Dotto Biteko alipofanya ziara ya ukaguzi wa soko la madini liliopo Shelui Wilayani hapo Julai 31, 2021.

Akiongea na wataalamu pamoja na wachimbaji wadogo wadogo waliofika katika soko hilo, Biteko aliwaambia kuwa usalama wa nchi upo kwa hawa wachimbaji wadogo wadogo kwa sababu wachimbaji wakumbwa muda wowote wanaweza kuhama au kuondoka.

“Turudishe nguvu kwa wachimbaji wadogo kwa sababu wakifanya kazi kwa weledi huwezi kuona uwazi uliopo kati yao na wachimbaji wakubwa,” alisema Waziri nakuongeza kuwa

“Nikuagize Kaimu Afisa Madini Mkazi kukutana na hawa wachimbaji wadogo wadogo endapo watakuandikia barua ya kujidhamini katika uchimbaji wao dhidi ya eneo hili basi wafunguliwe shughuli za uchimbaji ziendelee.”

Kwa upande wake Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Chone Malembo amemuhakikishia Mkuu huyo wa Wilaya kuwa wachimbaji hao walikwisha andika barua ya kujidhamini kuchimba katika maeneo yaliokua salama katika eneo hili.

Malembo alifafanua kuwa maeneo hayo ni duaara namba 00 na 27, huku akiwataka kutofika katika maduara 12 yalikuwa na changamoto anuai.

Naye katibu wa Bodi ya Sekenke one ambaye ni mmoja wa miliki wa Mgodi huo, Joseph Mnemba ameishukuru serikali kwa kufungua mgodi huo kwa sababu maisha ya wananchi yalikua magumu, hivyo wanamuomba Mungu awasadie neema zipatikane ili kila mmoja apate kipato.

Mgodi wa Sekenke one una leseni mbili za mgodi wa Sekenke namba moja na Sekenke namba mbili ambazo zilifungwa mnamo Novemba 9, 2019 kutokana na changamoto anuai. Sasa shughuli za uchimbaji zitaendelea na kurudisha uchumi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Mkoa wa Singida na Taifa kwa ujumla.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.