• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda ametoa ofa ya kwenda katika Hifadhi ya Taifa yoyote Nchini kwa walimu wa Shule ya Sekondari Lulumba

Posted on: July 30th, 2021

Hemedi Munga Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda ametoa ofa ya kwenda katika Hifadhi ya Taifa yoyote Nchini kwa walimu wa Shule ya Sekondari Lulumba waliofaulisha Wanafunzi wa kidato cha Sita kwa asilimia mia moja mwaka 2021.

Mwenda ametoa ofa hiyo leo Ijumaa Julai 30, 2021 wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza Walimu pamoja na Wanajumuiya wa Shule ya Sekondari Lulumba iliyopo Mjini Kiomboi Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Akiongea katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya amewapongeza wanajumuiya ya Sekondari ya Lulumba kwa kumuheshimisha na kuuheshimisha Mkoa wa Singida kufuatia kuingiza katika kumi bora Kitaifa somo la fizikia kushika nafasi ya 5 kati ya 462 na somo la jiografia kushika nafasi ya 7 kati ya 750 huku masomo yote 7 yakiongoza kimkoa.

“Ndugu wanajumuiya mpenipa heshima kubwa ambayo ninahitajika kuilinda na kuiendeleza kwa kutimiza mtazamo wangu wa kwanza wa elimu katika uongozi wangu wilayani hapa.” Ameshukuru Mwenda na kuongeza kuwa

“Ni nyinyi Walimu ndio mtakaonivusha hapa, hivyo fahamuni kuwa tunayo kazi kubwa ya kuimarisha na kuyaendeleza mafanikio haya.”

Kufuatia ufaulo huo, Mwenda ametoa ofa ya kwenda katika Mbuga yoyote ya Wanyama Tanzania na kukaa huko kwa muda wa siku tatu, akiamini kuwa Walimu hao baada ya kurejea watakua na ari na kasi mpya itakayowezesha matokeo ya mwakani shule ya Lulumba kuingia katika kumi bora kitaifa.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya amewahakikishia Walimu kuwa atakuwa mstari wa mbele kutatua changamoto zao wakati na mahali popote utakapohitajika msaada wake.

Awali akitoa taarifa fupi mbele ya Mkuu huyo wa Wilaya, Mkuu wa Shule ya Sekondari Lulumba, Jeremia Kitiku amesema kuwa Shule imekuwa inapata mafanikio ya kupanda kwa ufaulu wa kidato cha sita mwaka hadi mwaka.

Akifafanua ufaulu huo, Kitiku amesema kuwa mwaka 2018/2019 walifaulu wanafunzi 71 sawa na asilimia 100, mwaka 2019/2020 walifaulu wanafunzi 151 sawa na asilimia 100 na mwaka 2020/2021 walifaulu wanafunzi 130 sawa na asilimia 100.

Aidha Kitiku amebainisha mikakati ambayo itawasaidia kufikia malengo ya kuingia kumi bora kitaifa mwakani kuwa ni kuhakikisha walimu wanajiandaa ipasavyo na kufundisha kila kipindi ili kumaliza mada mapema na kufanya marejeo, kuandaa mitihani mingi ya ndani na nje kwa vidato vya mitihani, kuwa na vikao vya tathimini vya mara kwa mara kwa kila ngazi na idara na kushirikiana na shule nyingine za ndani na nje ya wilaya yetu ili kukuza ufanisi wa walimu na wanafunzi.

Jumuiya ya Shule ya Lulumba imekuwa ikitoa motisha ya chai, chakula cha mchana na fedha kutokana na namna mwalimu atakavyopata daraja, jambo mbalo limekuwa chachu ya mafanikio hayo.

Akiongea na Mwandishi wetu, Mwalimu wa Taaluma wa Shule hiyo, Nyakusuma Sospeter amesema kuwa Shule imewatunuku motisha Tsh 5.6 milioni Walimu  mbalimbali waliofaulisha kwa kupata daraja la A na B.

Amefafanua kuwa Walimu waliofaulisha kidato cha pili wamepata laki tano na tisini (590,000), kidato cha nne 2.1 milioni, kidato cha sita 1.9 milioni na Idara mbalimbali kupata laki tisa elfu saba na mia tano (907,500).

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari wa Halmashuri hiyo, Godfrey Mwanjala amesema kuwa mafanikio hayo yanatokana na upendo na ushirikiano walionao kati yao na Utawala, hivyo amewaomba wadumishe mwenendo huo ndio utakaowawezesha kufuta daraja la 3, 2 na zero.

Naye mmoja wa walimu wa Shule hiyo, Madamu Sarafina amemuahidi Mkuu huyo wa Wilaya kuwa matoke ya kidato cha sita mwakani wataingia katika kumi bora Kitaifa.

Shule ya Sekondari Lulumba kwa sasa inawanafunzi 971 kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita ambapo 370 ni wasichana na 601 ni wavulana.

MWISHO

Mkuu wa Shule ya Lulumba Sekondari, Jeremia Kitiku  akifafanua ufaulu wa kidato cha sita  kuwa mwaka 2018/2019 walifaulu wanafunzi 71 sawa na asilimia 100, mwaka 2019/2020 walifaulu wanafunzi 151 sawa na asilimia 100 na mwaka 2020/2021 walifaulu wanafunzi 130 sawa na asilimia 100. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari, Godfrey Mwanjala akiwataka wanajumuiya ya Lulumba Sekondari  kudumisha  mafanikio ya ufaulu  yanatokana na upendo na ushirikiano walionao kati yao na Utawala, hivyo mwenendo huo ndio utakaowawezesha kufuta daraja la 3, 2 na zero. Picha na Hemedi Munga

Walimu mbalimbali wa Lulumba Sekondari wakifuatilia nasaha za viongozi mbalimbali wakati wa  hafla fupi ya kuwapongeza Walimu pamoja na Wanajumuiya wa Shule ya Sekondari Lulumba iliyopo Mjini Kiomboi Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.