• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amewapongeza viongozi na wananchi wote kufanikisha Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Wilayani Iramba.

Posted on: July 21st, 2021

Hemedi Munga Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amewapongeza viongozi na wananchi wote kwa kufanikisha kuupokea Mwenge wa Uhuru ukiwa unawaka, unameremeta, kufanikiwa kuutunza na kuukimbiza Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Mwenda ametoa pongezi hizo leo Jumatano Julai 21, 2021 punde baada ya kumkabidhi wakimbiza mbio maalum za Mwenge wa Uhuru kitaifa na Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Sophia Mfaume katika viwanja vya kijiji cha Kidii kata ya Msingi Wilayani hapo.

Mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa viongozi na wananchi wa Iramba mnastahili pongezi kwa namna ambavyo mmekua mstari wa mbele tangu maandalizi ya miradi ya maendeleo na shughuli zote zilizotembelewa  kuhakikisha zinakamilika kwa  wakati na ubora unaohitajika.

 Mwenda amebainisha kuwa miradi yote iliotembelewa na Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru zilikua na garama ya takriban Tsh 1.8 bilioni.

Aidha amefafanua kuwa fedha hizo zimechangiwa na nguvukazi (wananchi) kwa kutoa Tsh 7.5 milioni sawa na asilimia 0.4, Serikali kuu imetoa Tsh  517.8 milioni  sawa nasilimia 27.5 huku Halmashauri ya Wilaya ya Iramba ikiwa imetoa Tsh 12 milioni sawa na asilimia 0.6 na Wahisani kutoa Tsh  1.3 bilioni sawa na asilimia 71.4.

Hivyo Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru zimezindua mradi wa barabara ya mchepuo iendayo Hospitali kongwe ya Kiomboi, jengo la Uthibiti ubora wa Elimu liliopo mjini kiomboi na Mradi wa maji uliopo katika kijiji cha Kyalosangi Tarafa ya Kinampanda Wilayani hapa.

Aidha Mbio hizo za Mwenge wa Uhuru zimefanikwa kutembelea na kuona shughuli sita (6).

Awali akifikisha ujumbe wa Mwenge wa Uhuru kwa  wananchi katika kijiji cha Misigiri kiongozi wa wakimbiza Mbio  maalumu za Mwenge wa Uhuru  Kitaifa, Luteni Josephine Paul amewataka wananchi hao kuwa mabalozi wa kufikisha ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa wananchi ambao hawakupata nafasi ya kuhudhuria katika mbio hizo.

Akieleza ujumbe Mkuu wa Mwenge wa Uhuru unaoonesha dira ya Taifa letu uliobeba kauli mbiu isemayo “TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu; itumie kwa usahihi na Uwajibikaji” amewataka wananchi kuitumia TEHAMA kwa usahihi na kujipatia habari, ajira na kusoma kwa njia ya mtandao nakutolea mfano kuwa unaweza kuwa Iramba huku unasoma chuo kikuu cha Dodoma ( UDOM) au chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM).

Pia kwa kutumia TEHAMA imekua rahisi kununua bili za maji na umeme na kufanikiwa kuondoa adha ya kupanga foleni na kupoteza muda.

“Ndugu Wananchi nitoe wito kwenu kuhakikisha mnadai risiti za kielektroniki pale mtakapo kua mmenunua bidhaa yoyote au kupata huduma yoyote” amesisitiza Luteni Paul na kuongeza kuwa

“Niziagize Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinakusanya mapato kielektroniki.”

Aidha amebainisha ujumbe wa kudumu wa mapambano dhidi ya Rushwa yenye kauli mbiu isemayo “Kupambana na Rushwa ni Jukumu langu”, hivyo amewataka wananchi  kutoa taarifa dhidi ya vitendo vya rushwa kwa mamlaka zinazohusika ili nchi isonge mbele.

Katika hatua nyingine Luteni Paul amewataka wananchi kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria chini ya kauli mbiu isemayo “Ziro Malaria inaanza na Mimi-Nachukua hatua kuitokomeza.” Hivyo awataka wananchi kuutokomeza ugonjwa wa malaria kwa kufukia madibwi na kuhakikisha wanalala ndani ya chandarua.

Pia amewakumbusha wananchi kuendeleza mapmbano dhidi ya madawa ya kulevya chini ya kauli mbiu isemayo “Elimu sahihi juu ya Dawa za kulevya huboresha huduma kwa Waraibu; chukua hatua.” 

Amewataka wanacnhi kuwa mstari wa mbele kutoa taarifa za watu wanozalisha, safirisha au kuuza dawa za kulevya ili wawezekuchukuliwa hatua, hatimaye kutokomeza kabisa suala la madawa ya kulevya nchini.

Aidha amewahimiza wanachi kuendeleza mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI chini ya kauli mbiu isemayo “Mshikamano wa Kitaifa; Tuwajibike kwa pamoja.” Hivyo ni wajibu wa wazazi kuwapa elimu vijana namna ya kujikinga na maambukizi ya VVU/UKIMWI na kuwa na tabia ya kupima mara kwa mara ili kutambua afya zao.

Halikadhalika amewaasa wazazi kuhakikisha wanatoa lishe bora kwa watoto chini ya kauli mbiu isemayo “Tujenge Jamii yenye Afya Imara kwa kuzingatia lishe bora.”

Kwa upande wake mmoja wa wanafunzi wa shule ya sekondari Shelui, Ernestina Shuka ameonesha kuwa ujio wa Mwenge wa Uhuru umekua na faida kubwa kwa sababu wamejipatia elimu ya namna ya kujikinga kujingiza katika madawa ya kulevya na hatua za kushauri kwa mtu alieathirika na madawa ya kulevya ili aweze kuacha kabisa matumizi ya madawa ya kulevya.

Mwenge wa Uhuru umekimbizwa kilometa 163.4 kutoka eneo la kupokelea Malendi na kupita katika tarafa 3, kata 7 na vijiji 12 mpaka  sehemu ulipokabidhiwa kijiji cha Kidii kata ya Msingi Wilayani Mkalama Mokani Singida.

MWISHO

Katibu Tawala Wilaya ya Iramba, Pius Songoma akisoma Risala ya Utii kwa Mhe, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Kulia ni Afisa Utumishi wa Wilaya hiyo, B’hango Lyangwa. Picha na Hemedi Munga

Kiongozi wa Wakimbiza mbio maalum za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Luteni Josephine Paul akitoa ujumbe wa Mbio za Mwenge kwa wananchi walihuohudhuria mbio hizo. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda kushoto akiwa na Kiongozi wa wakimbiza Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru katikati, Luteni Josephine Paul pamoja na wakimbiza Mwenge wa Uhuru wengine wakikagua barabara ya mchepuo iendayo hospitali kongwe ya Kiomboi tayari kwa kuizindua. Picha na Hemedi Munga


Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda watatu kutoka kushoto akiwa na Kiongozi wa wakimbiza Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru katikati, Luteni Josephine Paul pamoja na wajumbe wengine wakitroti baada ya kukagua barabara ya mchepuo iendayo hospitali kongwe ya Kiomboi tayari kwa kuizindua. Picha na Hemedi Munga

Mwanafunzi wa shule ya sekondari Shelui aliyo katika klabu ya kupiga vita madawa ya kulevya, Ernestina Shuka ameonesha kuwa ujio wa Mwenge wa Uhuru umekua na faida kubwa kwa sababu wamejipatia elimu ya namna ya kujikinga kujingiza katika madawa ya kulevya na hatua za kushauri kwa mtu alieathirika na madawa ya kulevya ili aweze kuacha kabisa matumizi ya madawa ya kulevya. Picha na Hemedi Munga

Viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakisikiliza ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mara ulipowasili katika viwanja vya shule ya msingi shelui . Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.