• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amewatahadharisha Wenyeviti wa kamati ya Sensa ya Watu na Makazi ngazi ya Wilaya, Kata, Kijiji na Kitongoji dhidi ya mawazo finyu yanayodaiwa kuenezwa na baadhi ya watu wasiolitakia mema Taifa la Tanzania.

Posted on: October 24th, 2021

Na hemedi Munga

www.dediramba.go.tz

SINGIDA-Iramba, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amewatahadharisha Wenyeviti wa kamati ya Sensa ya Watu na Makazi ngazi ya Wilaya, Kata, Kijiji na Kitongoji dhidi ya mawazo finyu yanayodaiwa kuenezwa na baadhi ya watu wasiolitakia mema Taifa la Tanzania.

Mwenda ametoa tahadhari hiyo leo Alhamisi Oktoba 21, 2021 wakati akiongea na Wenyeviti wa kamati ya Sensa ya Watu na Makazi ngazi zote katika kijiji cha Nselembwe Tarafa ya Shelui Wilayani hapa.

“Ndugu zangu ili inchi iendelee inahitaji mipango na mikakati madhubuti ya maendeleo ambayo hufanikishwa na takwimu zinazoongoza kujua idadi kamili ya uhitaji ambapo Taifa linatakiwa liwahudumie, halikadhalika idadi ya wazalishaji ili Taifa liwaunge mkono katika kuzalisha.” Alisema Mkuu huyo wa Wilaya na kuongeza kuwa

“Ndugu viongozi, ni lazima sasa tuanze kujipanga kuelekea Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 kwa kutoa taarifa kwa wananchi wetu kuwa kutakuwa na zoezi la Sensa, zoezi la kitaifa ambapo Serikali inalitegemea, hivyo tujipange kutekeleza kwa ufanisi.”

Katika kulitekeleza hili amewataka wenyeviti hao kuhakikisha wanaunda kamati na kuanza kutoa taarifa ya utekelezaji wa Sensa ya Watu na Makazi punde baada ya kupokea taarifa hiyo.

Amewataka kufahamu kuwa Sensa ni muhimu kwa Taifa lao kwa kuwa Taifa huweza kufahamu kuwa ni huduma kiasi gani ziende kwenye maji, umeme, barabara na huduma nyinginezo ambazo Serikali huzitoa kwa raia wake.

“Taarifa hizi ambazo hueleza kuwa ni wananchi wangapi, wanapatikana wapi, wanahitaji huduma kiasi gani na wanaishi katika hali gani Serikali inahitaji taarifa hizi kwa ajili ya kuweka mipango yake vizuri.” Alisisitiza Mwenda

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya amewataka Wenyeviti hao kuwa na tabia ya kujitolea kuitumikia Serikali kwa uzalendo wa hali ya juu kwa sababu maendeleo wanayoyaona leo ni kutokana na moyo wa kizalendo ambao Mwl J.K. Nyerere Rais wakwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliujenga katika Taifa hili.

Alifafanua kuwa maendeleo na mafanikio makubwa yaliofikiwa na Tanzania na Duniani kwa ujumla yamepatikana kwa sabubu wananchi wa nchi husika walikuwa na tabia ya kujitolea.

“Napenda kuwakumbusha ndugu zangu kuwa maendeleo na usalama wa nchi ya Tanzania mnaouona ni kutokana na mioyo ya kujitolea aliyoijenga Mwl. J.K Nyerere.” Alikumbusha Mwenda

Tanzania imekuwa nchi ya amani, upendo na usalama ukilingani na nchi jirani mfano wa Kenya, Uganda, Msumbiji na Rwanda ambazo zimedaiwa kuwa na mapigano ya mara kwa mara kwa sababu za makabila na nyinginezo, huku makabila mfano wa Wayao, Wamakuwa na mengineyo ambayo hupigana kwa ajili ya maslahi binafsi.

Wakati makabila ya Wayao, Wamakuwa na mengineyo yapo nchini Tanzania lakini hawapigani kwa sababu Mwal. J.K. Nyerere alijenga misingi ya kuvumiliana na kila mmoja apate maendeleo katika Taifa hili.

Akiongea kwa niamba ya wenyeviti hao, Mwenyekiti wa Kijiji cha Nselembwe Tarafa ya Shelui, Paulo Daninga amemuhakikishia Mkuu huyo wa Wilaya kuwa wataunda kamati kwa namna ambayo muongozo unavyoelekeza na kuanza uhamasishaji wa Sensa ya watu na Makazi mwaka 2022 siku chache baada ya mkutano huo.

“Asante Mkuu wa Wilaya! nikuhakikishie kuwa maelekezo yote ulioyatoa tutayafanyia kazi kwa umakini.” Aliahidi Daninga na kongeza kuwa

“Ndugu zangu viongozi niwaombe katika maeneo yenu kuhakikisha kuwa hakuna migogoro kwa sababu migogoro haileti maendeleo wakati nchi hii inahitaji maendeleo.”

Kwa upande wake Afisa Tarafa wa Tarafa hiyo, Nicholaus Makoye amewataka wenyeviti hao kuifikisha elimu ya Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 iliyotolewa na Mkuu huyo wa Wilaya kwa wananchi ili wawe tayari kwa zoezi hilo la kitaifa.

MWISHO

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akiwaelekeza majukumu ya utekelezaji wa Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 Wenyeviti wa Sensa ya Watu na Makazi ngazi ya Wilaya, Kata, Kijiji na Kitongoji kijiji cha Nselembwe Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Baadhi ya Wanyeviti wa kamati ya Sensa ya watu na Makazi mwaka 2022 wakifuatilia kwa makini majukumu yao yaliokuwa yakiwasilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda. Picha na Hemedi Munga.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.