• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

MKUU wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amewataka Madiwani kuwa wakali dhidi ya wale wanaotorosha mazao.

Posted on: October 31st, 2021

Na Hemedi Munga

tehama@mgail.go.tz

Singida - Iramba. MKUU wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amewataka Madiwani kuwa wakali dhidi ya wale wanaotorosha mazao.

Mwenda ametoa wito huo juzi wakati wa salamu za viongozi katika Mkutano wa Baraza la Madiwani lililofanyika katika ukumbi wa mikutano Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Kuziba njia zote zinazotumika kutorosha mazao kutaifanya Halmashauri hii iweze kukusanya mapato na kuweza kuingia kumi bora katika ukusanyaji wa mapato ukilinganisha na Wilaya ya Meatu na Igunga zilizo jirani.

“Waheshimiwa Madiwani! wito wangu kwenu tuhakikishe tunasimamia Halmashauri yetu iweze kukusanya vizuri, Hivyo mnayo nafasi ya kuwasimamia Watendaji wa Serikali huko mlimpo kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa uadilifu, usimamizi bora na umakini.” Amesema Mwenda

Utaratibu huu ndio uwe muelekeo wetu wakwanza kuhakikisha Halmashauri hii inapaa katika nyanja ya mapato kwa sababu vyanzo vyote vya mapato vipo na vinaweza kuleta mapato stahiki.

“Ndugu zangu! kipimo kikubwa cha kitaifa cha utendaji wa Halmashauri yetu ni kukusanya mapato,hivyo tukawe wakali kusimamia kukusanya mapato” amesisitiza

Akiongea katika Mkutano huo, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Innocent Msengi alisema kuwa kupitia watumishi wa Serikali waliopo watahakikisha wanasimamia shughuli za maendeleo na kukusanya mapato.

Aidha aliongeza kuwa Baraza la madiwani limedhibitisha kazini watumishi 13, huku watumishi wawili wakiachwa katika kipindi cha matazamio.

“Kwa sababu tumeyagundua mapungufu ya kukusanya mapato kwenye robo ya kwanza, sasa tutasimamia vyanzo visivyokuwa na msimu na kuhakikisha robo ya pili tunavuka asilimia 50 ya ukusanyaji wa mapato.” Ameahidi Msengi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilayani hapo, Samwel Joel amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa fedha nyingi ambazo ameiletea Halamashauri hii ili kutekeleza miradi mbalimbali.

“Niwaombe Waheshimiwa Madiwani na Watendaji wote kusimamia miradi hii sawasawa ili thamani ya fedha ilingane na miradi inayotekelezwa.” Amesema Joel na kuongeza kuwa

“Tuisimamie miradi hiyo ili tija ionekane kwa namna ambavyo Serikali ilivyokusudia.”

Baraza la Madiwani limemaliza kikao chake cha robo ya kwanza na kuahidi kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa Wilayani hapo.

MWISHO

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Innocent Msengi katikati akiongoza Barala la Madiwani robo ya kwanaza mwaka wa fedha 2021/2022. Kulia ni Makamu Mwenyekiti Ndugu Monica na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Ndugu Maziku. Picha na Hemedi Munga

Waheshimiwa Madiwani wakiwa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani lililofanyika katika ukumbi Mdogo wa Halmashauri hiyo. Picha na Hemedi Munga

Baadi ya Wakuu wa Idara na Vitengo wakifuatilia kwa makini Baraza la Madiwani liliofanyika katika ukumbi Mdogo wa Halmashauri hiyo.Picha na Hemedi Munga

Baadi ya Wakuu wa Idara na Vitengo wakifuatilia kwa makini Baraza la Madiwani liliofanyika katika ukumbi Mdogo wa Halmashauri hiyo.Picha na Hemedi Munga

Baadi ya Wakuu wa Idara na Vitengo wakifuatilia kwa makini Baraza la Madiwani liliofanyika katika ukumbi Mdogo wa Halmashauri hiyo.Picha na Hemedi Munga



Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • SIKU YA UKIMWI DUNIANI DISEMBA 1,2025

    December 01, 2025
  • MAZOEZI YA VIUNGO YA KILA IJUMAA KWA WATUMISHI NA WANANCHI WOTE WA KIOMBOI NA MAENEO YA JIRANI

    November 27, 2025
  • RATIBA YA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO KATA YA KASELYA

    November 25, 2025
  • DC MWENDA AWAPONGEZA WALIMU NA WANAFUNZI WILAYANI IRAMBA KWA MATOKEO MAZURI MTIHANI WA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI

    November 24, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.