• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amewataka Watumishi kuishi katika vituo vyao vya kazi.

Posted on: July 29th, 2021

Hemedi Munga Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amemuagiza Afisa Elimu Kata ya Kisiriri kuwaandikia barua Walimu wote wanaokaa nje ya kata hiyo wawe wamekwisha hamia katika vituo vyao vya kazi ifikapo Agasti 10, mwaka huu.

Mwenda ametoa agizo hilo leo Alhamisi Julai 29, 2021 wakati akiwa katika ziara yake ya kusikiliza kero na kuzitatua katika kata ya Kisiriri Wilayani hapa.

“Kuanzia leo hii nimeagiza Walimu wote waishi katika kata hii, ambaye hawezi kuishi hapa kijijini atuandikie barua kuwa kazi imemshinda, sisi tutatafuta walimu wengine maana kuna vijana wengi sana wanamaliza vyuo vikuu wanahitaji kazi mahali popote.” Ameagiza Mkuu huyo wa Wilaya

Katika hatua nyingine, Mwenda amewataka wananchi kukata kadi ya CHF ili wasitozwe tena fedha yoyote wanapokuwa wamekwenda hospitali, kituo cha Afya au Zahanati.

“Ndugu zangu wananchi hakuna utaratibu wa mtu anayekua na kadi ya CHF kutakiwa kutoa tena shilingi elfu kumi anapokwenda Zahanati au hospitali ya Wilaya.” Amesema Mwenda na kuongeza kuwa

“Tukubaliane kuwa wananchi hawa wakate kadi za CHF halafu waone faida ya kuwa na kadi ya CHF pale watakapoumwa wanapata dawa itawafanya wahamasishane wao kwa wao kukata kadi ya CHF na kila mmoja atakua na kadi kwa kuwa anahitaji huduma ya matibabu na anayapata.”

Aidha amepiga marufuku kuwapiga faini wakinamama ambao wanajifungulia nyumbani. Hata hivyo amewahamasisha akina mama hao kujifungulia Hospitali.

“Kutoza faini kwa mzazi aliyejifungulia nyumbani ni jambo ambalo limesitishwa, hivyo ninawatangazia rasmi kupitia mkutano huu kwamba tozo hizi zimesitishwa, hivyo mtu yoyote atakayeendelea kutoza mimi nitashughulika naye.” Amepiga marufuku Mkuu huyo wa Wilaya

Halikadhalika amewaomba wananchi hao kumpa ushirikiano.

“Ndugu zangu Wananchi! tukifanya kazi kwa ushirikiano tutapata maendeleo” Ameomba Mwenda

Hayo yote yamekuja baada ya wananchi hao kuibua kero mbalimbali mbele ya Mkuu huyo wa Wilaya ambapo alizitatua papo hapo.

Akijibu kero za Wananchi Afisa Ustawi wa Jamii kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Happines Alex amesema kuwa tayari Serikali ilikwisha leta fedha za dawa, hivyo dawa zipo katika vituo vyote na Hospitali.

Kwa upande wake mmoja wa Wananchi aliewasilisha kero yake mbele ya Mkuu huyo wa Wilaya, Pelepetuwa Makala amemshukuru Mkuu huyo wa Wilaya kwa kuja katika kata yao na kutatua kero zilizokuwa zikiwakabili hasa kwa upande wa afya na elimu.

“Napenda kumshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kutuhakikishia kuwa kero ya upatikanaji wa dawa sasa imekwisha na katika upande wa Walimu kuhakikisha wanakaa katika vituo vyao vya kazi.”

Naye muinjilisti wa kanisa la KKKT Kisiriri, Daudi Napegwa amesema kuwa ujio wa Mkuu huyo wa Wilaya umeleta hamasa, faraja na matumani mapya  kwa wananchi kwa sababu kero ambazo walizokuwa nazo zimepata majibu stahiki toka kwa mkuu huyo wa Wilaya.

“Ninamshukuru sana mkuu wetu wa Wilaya kwa sababu ujio wake umefanya tuone suala la umeme, upatikanaji wa maji, walimu kukaa katika vituo vya kazi, upatikanaji wa dawa katika vituo vya afya na hospitali vimepata majibu stahiki.” Amesema Napegwa.

Mkuu wa Wilaya amefanya ziara kata ya kisiriri, Old Kiomboi, Kaselya, Ndulungu na akitarajiwa kufika katika kila kata zilizopo katika Wilaya hiyo.

MWISHO

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akiwahutubia wananchi waliohudhuria mkutano uliofanyika kata ya Kisiriri leo Julai 29,2021. Alipofanya ziara katani hapo. Picha na Hemedi Munga

Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Happines Alex akiwatoa hofu wananchi juu ya masuala mbalimbali yanayohusu afya wilayani hapo. Picha na Hemedi Munga

Wananchi mbalimbali waliohudhuria mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda alipofanya ziara kata ya Kisiriri Wilayani hapo. Picha na Hemedi Munga

Announcements

  • TANGAZO KUHUSU UJIO WA MADAKTARI BINGWA HOSPITALI YA WILAYA YA IRAMBA-KIOMBOI February 20, 2026
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.