• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleimani Mwenda ametatua mgogoro wa Wachimbaji wa Madini ya dhahabu Sekenke Namba Moja.

Posted on: August 18th, 2021

Hemedi Munga Irambadc

irambadc@singida.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amesikiliaza na kutatua mgogoro wa wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu katika Mgodi wa Sekenke Namba Moja Wilayani Iramba Mkoa wa  Singida.

Mwenda ametatua mgogoro huo leo Jumatano Agosti 18, 2021 wakati akiwa katika ziara zake za utatuzi wa kero mbalimbali kwa wananchi wa Wilaya hiyo.

Akiongea na Wamiliki wa Leseni wa eneo hilo pamoja na Wachimbaji Wadogo, Mwenda amewataka kufahamu kuwa wao wanategemeana katika kuwendesha Mgodi huo.

Uchimbaji wa madini ya dhahabu katika eneo hilo unawezesha shughuli za kiuchumi kwa mama ntilie, walimaji wa mpunga wauzao kwa mama ntilie, shughuli nyinginezo pamoja na madini yanayo uzwa kutoa mrabaha kwa serikali kujipatia mapato.

Ameifafananisha hali hiyo na mnyororo ulioungana ambapo ukikatika shughuli za uchumi na ajira kwa wachimbaji zitakuwa zimesimama.

Kufuatia hali hiyo, Mwenda amewaomba wamiliki wa Leseni ya Mgodi Namba Moja kutoza asilimia mbili (2)badala ya tatu (3)  waliokuwa wamewapandishia Wachimbaji wadogo kulipia klemu.

Akikifafanua kuhusu asilimia tatu ya kulipia klemu ya Wamiliki wa leseni ya Mgodi huo, kwa niaba ya Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, Jeshua Nduche amewataka wamiliki hao kudumisha mahusiano mazuri na wachimbaji Wadogo.

“Ndugu zangu Wachimbaji, hili ni swala la mahusiano kuona namna bora ya kuimaliza changamoto hii hata kama mtakuwa ndani ya sheria.” Amesema Nduche  

Awali akibainisha sababu iliyopelekea Wamiliki wa Leseni hiyo kutoza asilimia tatu (3)  kwa klemu, Katibu wa Wamiliki wa leseni hiyo, Joseph Mnemba amesema kuwa Bodi hiyo inamalengo yakufikia uchimbaji wa kati, hivyo taratibu za uendeshaji wa leseni ya mgodi huo zinabadilika.

Sasa hakuna uadui kati ya Bodi ya Sekenke Namba Moja na Wachimbaji wadogo, wenyenacho na wasiokuwa nacho na wala Bodi hiyo haitawazarau wachimbaji hao.

Aidha amemshukuru Mkuu huyo wa Wilaya kwa sababu amewapatanisha kati ya Bodi ya Mgodi huo na Wachimbaji hao.

Kwa upande wake mmoja wa Wachimbaji wadogo wa Mgodi huo, Maduhu Lameki amewataka Wamiliki wa Leseni ya Mgodi huo kudumisha kauli nzuri kwa Wachimbaji wadogo.

Mgogoro kati ya Wachimbaji Wadogo na Wamiliki wa Leseni ya Mgodi huo uliibuka baada ya Wamiliki hao kupandisha asilimia ya kulipia klemu kutoka kwenye asilimia Mbili (2)  hadi tatu (3).

Ikiwa ni siku chache tu, tangu Mkuu wa Wilaya hiyo aliporudisha rasmi shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu katika Mgodi wa Sekenke Namba Moja  uliokuwa umefungwa tangu mwaka 2019.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.