• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula jukwaani akijibu maswali ya wananchi ya papo kwa hapo mbele ya Mkimbiza Mwenge kitaifa Ndugu Mzee Mkongea Ali. Picha na Hemedi Munga.

Posted on: August 25th, 2019

Hemedi Munga, IrambaDC

tehama@singidadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amesikiliza na kutatua kero za wananchi mbele ya Kiongozi wa wakimbiza mwenge kitaifa ndugu, Mzee Mkongea Ali.

Akisikiliza na kutatua kero za wananchi  leo Agosti 25, 2019 wakati wa kukimbiza mwenge kijiji cha Misigiri wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

 Akiwasilisha kero na kuomba ufafanuzi  mbele ya Mkuu wa Wilaya   Luhahula, Mkazi wa Misigiri  anayejulikana kwa jina maarufu la Mama Tururamba amesema kuna mwingiliano unaokuja kutoka TARURA kuwaondoa vijana waliobuni mradi wa kulinda  magari, wakihofia vijana kupoteza ajira zao na  kurudi kwenye hali yao ya  zamani inayohatarisha eneo hilo kwa udokozi.

Akijibu kero hiyo Mkuu wa Wilaya, Luhahula amesema ni kweli  serikali kupitia TARURA walitangaza kukusanya mapato yote yanayotokana na paki ya magari kwa hiyo tarura watakaa na wataalam  kujadiliana namna bora ya ukusanyaji wa maduhuli ya serikali.

“Ni kweli kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa serikali kupitia TARURA walitangaza kukusanya mapato yatokanayo na paki za magari, ukusanyaji wa maduhuil haya TARURA watakuja wakae na kamati ya usalama ya wilaya pamoja na wataalam tuone mfumo mzuri wa ukusanyaji wa mapato hayo, aidha atakaye jihusisha na wizi tutamkamata. “ aliongeza Luhahula

Naye Yoweri Shango akiwasilisha kero yake amesema wakati wa uchaguzi Mh, Rais John Pombe Magufuli alituahidi  kutoa mikopo Sh50 milioni kwa kila kijiji  imeishia wapi? huku akitaka kufahamu kwanini ajira hazitolewi licha ya kuwa wanaendelea kuwasomesha watoto wao.

Akijibu kero hiyo Mkuu wa Wilaya, Luhahula amesema kumekuwa na shule nyingi zinazotokana na usimamizi mzuri wa serikali hii na kuwataka wazazi kuwasomesha watoto wapate elimu iwasaidie katika kutatua changamoto zao, kwa kuwa shule na vyuo vikuu vimekuwa vingi, hata leo Mh Rais akitamka kwamba walioko kwenye ajira anawafuta ili aajiri  tena bado hawataisha.

‘’Tunasomesha vijana wetu  akiwemo  na wakwangu ili waweze kujitgemea nakujua namna ya kukabiliana na maisha yao.” Alisema Luhahula

Huku akijibu suala la mikopo kuwa inawezekana mikopo hiyo inakuja kwa mfumo wa kuwezesha maendeleo na kwakuwa ilani ya CCM inaisha baada ya miaka mitano kwa hiyo muda bado haujaisha.

‘’ Leo Iramba tumejenga kituo kikubwa cha afya Ndago na Kinampanda na zimeletwa pesa nyingi katika shule zetu na Mh, Rais John Pombe Magufuli.“ Aliongeza Luhahula

Naye Helana Mtigi mkazi wa kijiji cha misigiri mtaa wa msimbazi  ameomba kupitia Mwenge wa Uhuru apate ufumbuzi kuhusu  kero yao watu 15 ya kutolewa upande wa kasikazi mwa kijiji hicho tangu mwaka 2010  kupisha mradi wa umeme ambapo mpaka sasa hawajalipwa,  kuwa ni lini sasa watalipwa?

Luhahula amejibu kero hiyo kuwa wamelifanyia kazi kwa kutoa notisi ya kufuta hati miliki ili hawa wananchi wapate haki yao na tumeisha peleka kwa kamishna wa ardhi ili waweze kufuta.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba amemuomba mkimbiza Mwenge Kitaifa Ndugu Ali, kufikisha salama zao kwa Mh, Rais John Pombe Magufuli kwa kuwapendelea kuwapa miradi mikubwa karibuni katika kila tarafa kuna mradi unaendela.

Akihutubia Kiongozi wa mbio za mwenge kitafa Ndugu Ali, amemsifu Mkuu wa Wilaya Luhahula kwa kuwapa wananchi nafasi ya kumuuliza maswali ya papo kwa hapo yanayohusu maendeleo, jambo ambalo hakuna  yoyote amefanya tangu waanze kuukimbiza Mwenge wa Uhuru 2019.

Akieleza  namna ya kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere,  Mwenge wa Uhuru  2019   ni kuchapa  kazi  bila kuchoka, kuendelea kupambana  na adui ujinga  maradhi na umasikini na kuendelea kuwashajihisha wananchi kuchangia  kodi kwa ajili ya mapato ya Taifa letu. Aliongeza Ali

Ali amefikisha  ujumbe wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 kwa wananchi kuwa ni dira na muelekeo wa Taifa letu ambao  umejikita katika sekta ya maji na uchaguzi wa serikali za mitaa chini ya kauli mbiu isemayo maji ni haki ya kila mtu tutunze vyanzo vyake na tukumbuke kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa.

Kuendeleza mapambano zidi ya rushwa chini yakauli mbiu isemayo  kataa rushwa jenga Tanzania, maambukizi ya VVU, UKIMWI chini ya kauli mbiu isemayo  pima, jitambue, ishi. Malaria  chini yakauli mbiu isemayo mimi niko tayari kutokomeza malaria we je .

Huku akiomba ushirikiano  chini yakauli mbiu isemayo tujenge maisha yetu, jamii yetu na  utu wetu bila madawa ya kulevya .

Mwenge wa Uhuru wilayani iramba umekimbizwa  kilometa 142.5 hadi eneo la makabidhiano wilayani Igunga , umepitia  Tarafa 3 , kata 7 na vijiji 14 huku ukipitia miradii 4 na shughuli sita ambapo miradi yote na shughulizi zote inajumla ya garama ya Sh1.1 bilion .

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.