• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mradi wa maji wa shilingi T.sh 578,498,580 wakabidhiwa kijiji cha Mlandala kata ya Urughu wilaya ya Iramba.

Posted on: December 20th, 2018

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida Mhe: Emmanuel Luhahula amekabidhi mradi wa maji kijiji cha Mlandala kata ya Urughu Tarafa ya Ndago wilayani Iramba mkoa wa singida.

Mhe: Emmanuel Luhahula ameongozana na Kaimu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba Mhe: Wilfred J. Kizanga (Diwani wa CCM kata ya Tulya), Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba Mwl Linno Mwageni, waandisi wa maji ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida, waandisi wa maji wa wilaya ya Iramba na wataalamu mbalimbali katika kukabidhi Mradi wa maji wa Shilingi T.sh 578,498,580/=,  Katiba na Hati ya usajili wa jumuiya ya watumia maji MWANGAZA Kijiji cha Mlandala kata ya Urughu wilayani Iramba.

Mhe: Emmanuel Luhahula amesema kuwa Mradi huo umekabidhiwa katika mikono salama hivyo wakazi wa Mlandala  wanaopata shida ya Maji kwa muda mrefu wategemee huduma safi za maji saa 24.

Ameongeza kusema jukumu lao ni kuhakikisha wakazi wa Mlandala wanapata maji hivyo wananchi watoe ushirikiano katika kutunza miundo mbinu iliyopo na kutoa taarifa pindi wanapoona bomba linavuja.” Nimekabidhi mradi huu wa maji katika mikono salama hivyo wakazi wa Kijiji cha Mlandala watapata huduma ya Maji safi na salama. nimatumaini yangu kwamba kasi ya magonjwa yatokanayo na Matumizi haba ya maji yatapungua, utoro wa wanafunzi shuleni utapungua unaosababishwa na muda mwingi kutumika kutafuta maji mbali na makazi wanakoishi alisema Luhahula.

Akisoma Taarifa ya Mradi wa maji Mwandisi Athuman Mkalimoto alisema Mradi huu umetekelezwa na Halmashauri ya wilaya ya Iramba na umekabidhiwa kwenye jumuiya ya watumiaji maji MWANGAZA Kijiji cha Mlandala ya kata ya Urughu.

Lengo la mradi ni kuwapatia wananchi wa Kijiji cha Mlandala huduma ya maji safi na salama pamoja na kuboresha Afya na kuinua shughuli za kiuchumi za Wananchi.

Huduma ya mradi wa maji katika kijiji cha Mlandala ilitokana na wananchi wa kijiji cha hiki kuchagua kuwa ni kipaumbele chao, hivyo waliamua kuomba mradi wa maji kutokana na shida ya maji iliyokuwa inawakabili hapo awali.

Mradi ulianza kutekelezwa Juni 2014 na kutakiwa kukamilika Januari 2015, kutokana na ukosefu wa fedha Mkandarasi aliendelea kutekeleza mradi kwa kuongezewa muda  kulingana na upatikanaji wa fedha hatimaye Mradi ulikamilika mwezi Disemba 2018.

Kazi zilizofanyika ni kuchimba kisima cha maji (1) kujenga tanki (1) la kusambaza maji lenye ukubwa lita 90,000,kujenga vituo  (8) vya kuchotea maji  vyenye jumla la koki (16),kujenga Milambo (2) ya kunyweshea mifugo,kujenga mitungi (2) ya kuhifadhia maji yenye ujazo wa lita 5,000 na lita 1,000,ufungaji wa tanki moja la plastiki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita 3,000 shule ya msingi, kuchimba mtaro wa kulaza bomba wenye urefu wa mita 15,574,kujenga nyumba (1) ya mashine,kufunga pampu (1) katika kisima cha maji,kufunga Jenereta (1) inayofua umeme wa kuendesha pampu ya maji,kuwapatia mafunzo waendesha mitambo (2) na wauza maji (8),kuunda Jumuiya (1) ya watumiaji maji na kutoa mafunzo kwa jamii  juu ya matumizi ya maji safi na Usafi wa Mazingira ili mradi uwe endelevu. Alisema Eng.Mkalimoto.

Mradi utawanufaisha zaidi ya wananchi 4,000 kwa kuwapatia huduma ya maji safi na salama karibu na makazi wanayoishi ndani ya umbali wa mita 400 kutoka mita 1500, pia mradi utanufaisha mifugo 15,607 kwa kupata huduma ya maji ya uhakika kwenye milambo miwili ya mradi iliyojengwa.

Mkuu wa wilaya Iramba Mhe: Emmanuel Luhahula akikabidhi mkataba na Hati ya usajili wa jumuiya ya watumia maji Kijiji cha Mlandala Kata ya Urughu Tarafa ya Ndago wilaya ya Iramba.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA November 03, 2023
  • KUITWA KAZINI November 29, 2023
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wamefanya ziara ya Ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa Wilayani Iramba

    October 24, 2023
  • RAIS DKT. SAMIA AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI SINGIDA KWA KISHINDO, WANANCHI WAMSHUKURU KWA MIRADI YA MAENDELEO

    October 17, 2023
  • MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amepokea rasmi Mbio za Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoani Tabora na aliyekabidhi ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Batlida Briani.

    September 22, 2023
  • MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Abdalla Shaibu Kaim amewataka Watanzania kuhakikisha wanakemea vitendo vya rushwa kwa maelezo kuwa rushwa inakwamisha maendeleo ya Mkoa pamoja na Taifa kwa ujumla

    September 22, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.