• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mtoto anusurika wakati Basi la MJ Safari likigongana uso kwa uso na Lori kijiji cha Kizonzo Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba.

Posted on: March 27th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Kondakta wa basi la MJ Safari,  Mohammed Hussein  amefariki dunia kutokana na majeraha makubwa aliyoyapata kwenye ajali iliyotokea kijiji cha kizonzo kata ya Shelui Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Kifo hicho kimetokea kutokana na ajali iliyotokea leo Ijumaa Machi 27, 2020  ikihusisha Lori na Basi la abiria katika barabara kuu iendayo Mwanza toka Singida Wilayani Iramba.

 

Akitoa taarifa fupi mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula, Daktari Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Abel Mafuru amesema kuwa wamepokea majeruhi 11 ambao wamepatiwa matibabu na kuwa wanaendelea vizuri.


“ Tumepokea majeruhi ambapo Mohammed Hussein amefariki kutokana na majera aliyoyapata yaliosababisha kutoka damu nyingi,” amesema Mafuru na kuongeza

 

“ Majeruhi wanne tunawapeleka Hospitali ya Mkoa wa Singida kwa ajili ya matibabu zaidi kutokana na namna walivyoumia.”

Majeruhi ambao wamepatiwa rufaa kwenda Hospitali ya Mkoa wa Singida ni Mohammed Salehe (45), Ramadhani Said (44), Hassan Iddi na  Hoja Nkindikwa(24).

Mafuru amewataja majeruhi ambao wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya hiyo kuwa ni Said Ally (45), Zakaria Mdundu (50), Amina Nkimiye(53) na dada yake, Sara na mtoto wake ambaye hakupata majeraha yoyote.

Mkuu wa Wilaya hiyo amewapongeza madaktari na manesi kwa namna walivyotoa huduma kwa majeruhi hao huku akiwapa pole na kuwatakia majeruhi hao kupona haraka.

Aidha Mkuu huyo ametembelea eneo ambalo ajali ilitokea na kuwataka wananchi kudumisha usalama na kuendelea kuliombea eneo hilo kwa kuwa kumekua na ajali za mara kwa mara.

Halikadhalika, amewakumbusha kuendelea kufuata maelekezo ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya korona.

Kwa upande wake Mkuu wa Kituo cha Polisi Tarafa ya Shelui, Afande Haule amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo nakwamba chanzo cha ajali ni dereva wa lori lenye usajili namba T939 CBW alipokuwa analipita gari dogo (overtaking) na kugongana uso kwa uso na basi la MJ Safari lenye usajili namba T779 AWJ.

Lori hilo lililokuwa limebeba ngano likitoka Dar es Salaam kwenda Nchini Rwanda likapinduka huku basi hilo lililokuwa likitokea Geita kwenda Dar es Salaa likiharibika vibaya.

Naye mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo,Nkende Ndimalala mkazi wa Kizonzo ameiomba Serikali kuweka bamzi (matuta) eneo hilo kwa kuwa gari zimekuwa zikipita kasi sana, hivyo kusababisha ajali za mara kwa mara.

MWISHO

Lori likiwa limeanguka baada ya kugongana uso kwa uso na basi la MJ Safairi kijiji cha Kizonzo Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akiwajulia hali majehuri waliolazwa Hospitali ya Kiomboi Wilaya ya Iramba. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mwl. Linno P. Mwageni  akiwajulia hali majehuri waliolazwa Hospitali ya Kiomboi Wilaya ya Iramba. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.