• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mwaka mmoja wa Rais Samia madarakani wananchi Iramba wafurahia miradi ya maendeleo

Posted on: March 29th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amesema kuwa hakuna kama Rais Samia kwa namna ambavyo ametakeleza miradi ya maendeleo ya zaidi ya takribani Tsh 90 bilioni katika Tarafa ya Ndago ndani ya mwaka mmoja wa utawala wake.

Mwenda ameeleza mafanikio hayo leo Jumatatu Machi 28, 2022 punde baada ya kukagua miradi ya maendeleo katika kata sita za Tarafa ya Ndago wilayani hapa akiwa na kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kamati ya Usalama wilaya.

Ni wajibu wetu kuwaeleza wananchi kuwa serikali yenu imefanya nini ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia kwa sababu nyie ndio mliiweka serikali hii madarakani.

Akizungumzia sekta ya elimu msingi na sekondari, Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa serikali ndani ya mwaka mmoja imejenga madarasa, mabweni, maabara na samani nyinginezo ambapo jumla ya takribani Tsh 782.6 milioni zimetumika.

Katika kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma sahihi za afya na kwa wakati serikali ya Rais Samia ndani ya mwaka mmoja imejenga vituo vya afya katika kata ya Kisiriri, Mtoa, Mwanduigembe, Urughu na Kidaru ambapo kila kimoja kimepata takribani 500 milioni.

Pia, katika kila kituo cha afya na zahanati kuna ujenzi wa matundu ya vyoo bora unaendelea ukiwa na thamani ya takribani Tsh 98.8 milioni huku Tsh 100 milioni nyingine zikijenga Zahanati katika kijiji cha Misuna na Kaselya.

Kutimiza azma ya serikali kumtua mama ndoo ya maji kichwani na kutatua migogoro inayosababishwa na akinamama kuchukua muda mrefu katika kutafuta maji serikali ya Rais Samia ndani ya mwaka mmoja akiwa madarakani imeleta takribani Tsh 1.1 bilioni ambapo miradi hiyo ipo katika hatua za mwisho, hivyo ni dhahiri kuwa sasa wananchi wataweza kuvuta maji katika nyumba zao.

“Hawa akinamama kubeba ndoo ya maji kichwani watasahau kabisa kwa sababu maji yatakuwa yanapatikana katika nyumba zao.” Alisistiza

Aidha, aliongeza kuwa sasa hivi mwanamke akiolewa ataendelea kungaa kwa sababu maji yatakuwa yanapatikana ndani.

Akiongelea kuhusu miundombinu ya mawasiliano, Mwenda alisema kuwa katika mwaka huu mmoja wa Rais Samia aliishaleta zaidi ya Tsh 80 bilioni kwa ajili ya kujenga barabara kwa kiwango cha lami inayoanzia Kizaga, Mukulu, Ndago, Mbelekese, Sepuka hadi Singida mjini.

“Tunataka maendeleo kwa ajili ya watu wote, hivyo niwahakikishie kuwa hakuna atakayedhulumiwa wala kuvunjiwa nyumba kabla ya kupata fidia yake, kila mmoja atapata haki yake.” Alisema

Aidha, aliongeza ipo barabara ya kutoka Kata ya Mbelekese, Misuna kuelekea Tumuli barabara kuu itokayo Singida mjini kuelekea Jijini mwanza imetengewa takribani Tsh 109 milioni na ujenzi unaendelea.

Halikadhalika, kuna ujenzi wa karavati kubwa sana katika barabara ya Malango ambapo takribani Tsh 200 milioni zinajenga ili kuhakikisha watu wakati wa masika wanapita katika karavati hilo na kuendelea na shughuli zao za kiuchumi.

Yapo matengenezo ya barabara kutoka Urughu kupitia Mangole mpaka Mpugizi kilometa 9.5 kwa takribani Tsh 765 milioni huku barabara ya kutoka Mtekente kupitia Msansao hadi kijiji cha Ujungu yenye urefu wa kilometa 11.7 kwa gharama ya Tsh 999 milioni Mkandarasi anaendelea kujenga barabara hiyo.

Pia, ujenzi wa barabara ya kutoka Kibaya kupitia kijiji cha Luzilukulu hadi Kipuma yenye urefu wa kilometa 15 yenye kugharimu fedha za kitanzania Tsh 624 milioni unaendelea, hivyo hakuna kama Rais Samia.

Fedha zote hizi ni kwa tarafa ya Ndago ambayo ni kati ya tarafa zinazopatikana ndani ya Wilaya ya Iramba.

Kwa upande wake mmoja wa washiriki wa mkutano huo, Jasmini Hamisi alimshukuru Rais Samia kwa kumtua mama ndoo ya maji kichwani, hivyo wameahidi kuendelea kumuombea afya njema ili aendelee kuliongoza Taifa hili kwa weledi na manufaa makubwa.

Jasmini alisema kuwa hatua yakupatikana maji katika maeneo yao imesababisha kutokuwepo ugovi kati yao na waume zao kwani maji sasa yanatoka katika nyumba zao ukilinganisha na zamani ambapo walilazimika kutembea umbali mrefu na kukaa muda mrefu.

Naye Pili Shabani alisema kuwa anampenda sana Rais Samia nakumuomba aendelee kuwaletea miradi mingi ili wanawake waendelee kunufaika na jamii kwa ujumla.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.