• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mwenda aita wawekezaji madini dhahabu, almasi na zilkoni Iramba.

Posted on: November 18th, 2021

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. MKUU wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda aitisha kongamano la wadau wa madini ya dhahabu, almasi na zilkoni ili kupata wawekezaji wa uchimbaji mkubwa wenye tija kwa wananchi wa Iramba.

Mwenda ametoa wito huo leo Alhamisi Novemba 18, 2021 wakati akiongea na wamiliki mbalimbali wa leseni za kuchimba madini katika kijiji cha Nselembwe Tarafa ya Shelui wilayani hapa.

“Ndugu zangu! nitajihisi kuwa nimefanikiwa ikiwa nitaifanya wilaya hii kuwa katika kumi bora zinazozalisha madini kwa wingi nchini.” Alisema Mkuu huyo wa wilaya na kuongeza kuwa

“Wilaya yetu ya Iramba imebarikiwa rasilimali ya madini mengi takribani kata 14 kati ya 20 zote zinamadini, huku baadhi ya maeneo yakiwa namafuta.”

Alisema kuwa ipo haja ya kutafuta wawekezaji wenye teknolojia kubwa ambazo zinauhakika wa kupata madini kwa sababu madini katika ardhi hii yapo.

Halikadhalika aliongeza kuwa katika hatua za awali zimejitokeza kampuni tatu ambapo moja inatoka Uturuki na mbili zinatoka China kwa ajili ya kuja kuchimba madini kwa kushirikiana na wenye leseni.

Kupatikana wawekezaji hawa na wakafanikiwa kuanza uzalishaji, ni hakika Halmashauri hii itaongeza uwezo wa kukusanya mapato yake ya ndani.

“Ni imani yangu kuwa ukipata mwekezaji mkubwa mwenye kutumia vifaa vya kisasa vya kuvuta maji na kuchimba lazima atapata dhahabu, almasi na zilkoni kwa sababu madini haya yapo.”

Kwa upande wake kaimu Afisa Madini Mkazi Mkoani Singida, Chone Malembo amesema kuwa kongamano hilo litashirikisha makampuni makubwa ikiwemo makampuni ya GGM, SHANTA, BARIKI na TWIGA.

“Ndugu zangu sio kweli kwamba wakati wajerumani wakichimba madini hapa Sekenke walimaliza madini yote, hivyo tuyakaribishe makampuni makubwa yashiriki ili tuyaoneshe fursa tulizonazo ili waone namna gani wanaweza kushirikiana na sisi.”

Hali hii itaitangaza Wilaya ya Iramba katika sekta ya uchimbaji wa madini ambapo kimkoa Iramba inaongaza kwa uzalishaji ukilinganisha na wilaya zote saba za Mkoa wa Singida.

“Tunataka tuzitangaze hizo fursa kwa kuwakutanisha wachimbaji wadogo na makampuni makubwa ili tuvutie uwekezaji na kuinuwa uchimbaji.” Aliongeza

Pia amepiga marufuku tabia ya wachimbaji wa almasi eneo la Luzilukulu Wilayani hapa ambapo baada ya kupata madini hayo wanakwenda kuyauza Mkoani Shinyanga.

Akiongea katika mkutano huo mjiolojisti, Yuda Tadei amesema kuwa makongamano yamekuwa yakitumika katika mikoa na wilaya za jirani na kuzifanya kujulikana kwa wawekezaji.

Tadae ilifafanuwa kuwa maeneo ya Geita, Kahama, Chunya na sehemu nyinginezo walitumia makongamano hayo kutoa data za upatikanaji wa madini na hivyo kuwafanya wawekezaji kujuwa kuwa wakiwekeza kwako watapata faida.

“Niwaombe ndugu zangu tushirikiane na Mkuu huyu wa Wilaya kuitangaza Wilaya yetu kwa madini haya yaliopo yanotasha kuifanya Iramba kuwa ya mfano nchini.”

Kwa upande wake mdau wa kuchimba madini eneo la Kenkangombe wilayani hapa, Salumu Kigalula amesema kuwa wazo alilolileta Mkuu huyo wa wilaya linafaida kubwa kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla.

“Kwa kweli tunashukuru kwa kupata Mkuu wa wilaya ambaye amekuwa na mawazo ya uchumi, hivyo siye tunakuunga mkono katika kulitekeleza hili” alisema Kigalula

Naye Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi Chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye ni mchimbaji wa madini eneo la Mbuyuni , Alex Odepo amesema kuwa ni kweli wamechoka kutumia nyundo katika uchimbaji nakutamani vyombo hivyo vya kisasa katika uchimbaji ili waweze kuyapata madini hayo na kuepukana na uchimbaji wa kubahatisha.

MWISHO

Baadhi ya wadau wa kuchimba madini wakiwa katika kijiji cha Nselembwe tarafa ya Shelui wilaya ya Iramba mkoani Singida wakifuatilia kwa kina maono ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda kuifanya Iramba kuingia kumi bora kuzalisha kwa wingi madini ya dhahabu, almasi na zilkoni. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.