• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba mkoani Singida, Innocent Msengi amewaagiza watendaji wa kijiji cha Doromoni, Afisa Uvuvi na Mweka Hazina wa Halmashauri hiyo kusimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato katika Ziwa Kitangiri.

Posted on: April 22nd, 2022

Na Hemedi Munga

Singida - Iramba. Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba mkoani Singida, Innocent Msengi amewaagiza watendaji wa kijiji cha Doromoni, Afisa Uvuvi na Mweka Hazina wa Halmashauri hiyo kusimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato katika Ziwa Kitangiri.

Msengi ametoa agizo hilo leo Alhamisi Aprili 21, 2022 wakati alipofanya ziara katika Ziwa Kitangiri akiwa na Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala wa Halmashauri hiyo katika kijiji cha Doromoni wilayani hapa.

“Niombe sana tusimamie mapato haya maana sintahitaji kuona tunafeli katika Ziwa hili kuhusu ukusanyaji wa mapato.” Aliagiza

Aidha, aliongeza kuwa hichi ni chanzo cha mapato ndani ya Halmashauri, hivyo kuanzia ngazi ya kijiji shirikianeni katika kukusanya mapato yanayopatikana kupitia samaki wanaotoka katika Ziwa Kitangiri.

“Ninahitaji katika vikao vyangu vya Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala nione taarifa inayoonesha kunamabadiliko chanya ya kukusanya mapato toka katika Ziwa hili.” Aliagiza

Halikadhalika, Msengi amemuagiza Mweka Hazina wa Halmashauri hiyo, Aminiel Kamnde kuhakikisha kila eneo la kukusanyia mapato kuna kuwa na vifaa vya kukusanyia mapato (Point of Sell) vya kielektroniki.

“Siitaji kuona hili Mweka Hazina, nahitaji kuona maeneo yote yana POS ambazo zinafanya kazi kwa sababu wewe ni Mweka Hazina ulieaminiwa, hivyo timiza wajibu wako.” Aligiza

Akijibu hoja ya Diwani wa kata ya Mbelekese wilayani hapa Omari Shabani aliyetaka kufahamu kuwa ni kwa nini samaki ni wachache wakati ziwa lilikuwa limefungwa na kufunguliwa Aprili mosi. Afisa Uvuvi wa Halmashauri hiyo, Deogratius Isagala alisema kuwa kumekuwepo na baadhi ya wavuvi wasiokuwa waaminifu wakitumia nyavu za timba zenye sumu ambazo zinadaiwa kuathiri uzajilishaji wa makulia ya samaki.

Aidha, aliongeza kuwa sababu nyingine zinazopelekea samaki kutopatikana kwa wingi ukilinganisha na msimu uliyopita ni kwa sababu Ziwa limefunguliwa hivi karibuni na kiwango cha maji ni kidogo.

Pia, uwepo wa madai ya shunguli za kibinaadamu za uunganishaji wa mifereji toka katika Mto Manonga eneo la Masakaliwa Igunga ambao unaaminika kuwa ni chanzo kikubwa kinachochangia maji kuingia kwa kasi katika Ziwa Kitangiri.

Halikadhalika kupungua kwa kina cha maji kumesababishwa na upungufu wa mvua uliotokana na mabadiliko ya tabia ya nchi na mmomonyoko wa udongo uliosababishwa na ukataji ovyo wa miti katika maeneo yanayozunguka rasilimali ya Ziwa.

Akongea katika Ziara hiyo mjumbe wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala Diwani wa Kata ya Kaselya wilayani hapa, Juma Makwaula alishauri kuwa Idara ya Uvuvi ihakikishe kuwa kunakuwepo mikakati inayosaidia na kukataza uharibifu kando na ndani ya Ziwa ili kulinda Ziwa Kitangiri.

“Ni vyema sasa kuwepo na mikakati madhubuti ya kudhibiti wanaochimba mitaro toka Mto Manonga na wanaolima kuziwiliwa ili kudhibiti uharibifu utakaosababisha Ziwa Kitangiri kukosa maji na Samaki kutopatikana.” Alishauri

Wakiongea kwa nyakati tofauti na mwandishi wetu wakazi wa kando mwa Ziwa Kitangiri walishauri kuwa hatua madhubuti zinapaswa kuchukiliwa ili kukabiliana na wimbi la kukosa samaki toka katika Ziwa Kitangiri.
Kwa upande wake Chazi John alisema kuwa ikiwa kutakuwa na udhibiti katika Mto Manonga na kudhibiti uwepo wa nyavu haramu utachangia kupatikana samaki wengi.

Naye Umoja Jeshuwa wakala wa kukusanya ushuru wa samaki katika Mwalo wa Doromoni katika Ziwa hilo, alishukuru upatikanaji wa samaki ambao umekuwa ukiboresha afya zao na kukuza uchumi wao.

Ziwa Kitangiri ni moja ya rasilimali muhimu iliyopo wilayani Iramba. Zipo shughuli za uvuvi zinazotoa mchango mkubwa wa kuboresha lishe ya jamii, usalama wa chakula, chanzo cha mapato ya Halmashauri hiyo, kukuza uchumi wa kipato cha kaya, kuboresha maisha na maendeleo ya mwananchi na Taifa kwa ujumla ili kufikia malengo ya kufika uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

MWISHO

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba mkoani Singida aliyevaa suti, Innocent Msengi akifafanua jambo wakati alipofika aikiwa na Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala kutembelea miradi ya maendeleo katika kata ya Kidaru kijiji cha Tyegelo Aprili 21, 2022. Picha na Hemedi Munga

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba mkoani Singida aliyevaa suti, Innocent Msengi akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Fedha, Mipango na Utawala na baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba walipotembelea Ziwa Kitangiri kujionea shughuli za Uvuvi Aprili 21, 2022. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.