• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Innosent Msengi amemuagiza meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini Tanzania (TARURA) kuhakikisha Mji wa kiomboi unapata barabara za lami.

Posted on: January 8th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Innosent Msengi amemuagiza meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini Tanzania (TARURA) kuhakikisha Mji wa kiomboi unapata barabara za lami.

Msengi ametoa agizo hilo leo Januari 7, 2022 katika Baraza la Madiwani wakati wakupitisha rasimu ya bajeti ya matengenezo ya barabara kwa mwaka wa fedha 2022/2023 lililofanyika katika ukumbi mdogo wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

“Nikuombe Meneja wa TARURA utusaidie tupate barabara za lami katika mji wetu wa Kiomboi na hiyo itakuwa ni heshima kwa wilaya hii kwa sababu wilaya hii ni kongwe ukilinganisha na wilaya nyingine Tanzania.” Alisema Msengi na kuongeza kuwa

“ Kwa kweli tunamshukuru sana Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan  kwa kushauri  kuwa bajeti ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini Tanzania (TARURA)  kuwa inajadiliwa na Madiwani kwa sababu wao ndio wawakilishi wa wananchi ili wananchi wapate kufahamu yanayopangwa kuhusu barabara za maeneo yao.”

Akiongea katika Baraza hilo, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Mhandisi Michael Matomora alisema kuwa kupita kwa bajeti hiyo kwa Madiwani itasaidia wananchi kuifahamu bajeti ya barabara na kujuwa kuwa ni nini serikali inataka kufanya katika kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuhusu barabara.

Awali akiwasilisha taarifa ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini Tanzania (TARURA) katika Baraza la Madiwani, Meneja wa TARURA Evance Kibona alisema kuwa rasimu ya bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 imeandaliwa kwa kuzingatia miongozo ya matengenezo ya barabara na mpango wa kitaifa wa miaka minne wa ujenzi na matengenezo ya barabara wa TARURA.

Kibona alifafanua kuwa wilaya ya Iramba inaomba kutengewa takriban Tsh 14.9 bilioni kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ukilinganisha na Tsh  7.1 bilioni  ambazo zilitengwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na ujenzi wa vivuko.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mbelekese Wilayani hapa, Omari Shabani alisema kuwa wamefurahishwa sana na namna ambavyo Rais Samia amewaletea fedha nyingi kwa ajili ya miradi mbalimbali.

“Kwa kweli tunampongeza sana Rais Samia kwa kutuletea fedha nyingi kupitia TARURA ambazo zitaibadilisha wilaya ya Iramba.” Alisema Shabani na kuongeza kuwa

“Sisi kama madiwani tutashirikiana na TARURA kuhakikisha fedha zilizotolewa zinatengeneza barabara kwa kiwango kinachotakiwa.”

Naye Diwani wa kata ya Shelui Wilayani hapa, Agness Amos alisema kuwa wako tayari kusimamia utekelezaji wa bajeti hii, hivyo wanaiomba TARURA kuhakikisha wanasimamia ipasavyo kutengeneza barabara kwa kiwango kinachokidhi thamani ya fedha zilizotolewa.

Wilaya ya Iramba ina mtandao wa barabara wenye urefu wa kilomita 743.55 ambapo kilomita 286.69 ni barabara za wilaya, kilomita 454.38 ni barabara za malisho na kilomita 2.48 ni barabara za jamii.

Mtandao huo una kilomita 1.5 barabara za lami, kilomita 1.5 barabara za zege, na  kilomita 224.36 barabara za changarawe.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.