• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Samwel Joel amewaagiza viongozi wote wa wilaya hiyo kuwa karibu na miradi ambayo inatekelezwa ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na ubora unaotakiwa.

Posted on: December 25th, 2021

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz


Singida - Iramba. Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Samwel Joel amewaagiza viongozi wote wa wilaya hiyo kuwa karibu na miradi ambayo inatekelezwa ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na ubora unaotakiwa.

Joel ametoa agizo hilo leo Ijumaa Desemba 24, 2021 wakati akiwa katika ziara ya Kamati ya Siasa ya wilaya hiyo punde baada ya kutembelea na kukagua mradi wa karavati linalojengwa katika barabara ya Songambele – Misuna kata ya Ndago wilayani hapa.

“Kwa kweli ninaendelea kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Ni fedha nyingi ametuletea Iramba, hivyo niwaombe viongozi wenzangu kuwa karibu na miradi hii ili itekelezwe kwa wakati na thamani yake iweze kuonekana. Tunahitaji kuona thamani ya fedha ya mradi huu.”  Aliagiza Joel

Alibainisha kuwa eneo hilo kuwa na karavati litasaidia mbuga hiyo iweze kupitisha mazao ya dengu kwa urahisi na hivyo kuweza kuwanufaisha wananchi kiuchumi.

“Niwaombe watekelezaji wa mradi huu, kuukamilisha kwa wakati ili kutimiza azma ya Serikali inayoakisi matakwa ya jamii.” Alisema

Akiongea katika ziara hiyo Mkuu wa wilaya hiyo ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya, Suleiman Mwenda amemuahidi Mwenyekiti wa Kamati hiyo kuwa maagizo yote aliyotoa Serikali itayatekeleza kwa wakati na kiwango bora ili kutimiza azma ya Serikali kuihudumia jamii kwa kurahisisha mawasiliano.

Awali akiwasilisha taarifa fupi mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa Meneja wa TARURA wilayani hapa, Evance Kibona alisema kuwa Serikali inatekeleza mradi wa karavati lenye urefu wa mita 16.6 na upana wa mita 8.8 huku likiwa na milango mitatu lenye jumla ya gharama ya Tsh 201.9 milioni.

Kibona alisema kuwa ujenzi wa mradi huu ulianza Oktoba 6, 2021 ambapo kwa  sasa ujenzi umefikia asilimia 67 na kutarajia kukamilika mapema ifikapo Aprili 5, 2022.

Aidha alifafanua kuwa ujenzi ukikamilika utachangia wanacnhi kupita katika barabara hiyo hata wakati wa mvua na hivyo kuendelea na shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa kijiji cha Usure, Songambele, Misuna na Mbelekese.

Kwa upande wake Diwani wa Kata hiyo, Ernest Kadeghe alisema kuwa wananchi wa kata hii wanamshukuru sana Mhe Rais kwa kuleta mradi huu ambao unafungua mawasiliano wakati wote.

“Kwa kweli wananchi wameitikia na kuunga jitihada zote kila zinapohitajika katika mradi huu na mingineyo.” Alisema Kadeghe

Naye mmoja wa vibarua wanaojenga karavati hilo, Ashrafu Rashidi aliwaasa vijana wenzake kuacha tabia ya kuchagua kazi badala yake kila ajira za muda na za kudumu zinapopatikana kuendelea kupambana ili maisha yaende.

Pia alimshukuru sana Mhe Rais kwa kuleta fedha za kutekeleza miradi mbalimbali ambayo imesababisha vijana wanajipatia ajira na kuepukana na tabia za udokozi na kujiingiza katika madawa ya kulevya.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.