• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Samwel Joel amewataka wauzaji wa mafuta ya alizeti kando mwa barabara kuu toka Singida kuelekea jijini Mwanza kuwa waaminifu katika biashara hiyo.

Posted on: December 26th, 2021

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, Samwel Joel amewataka wauzaji wa mafuta ya alizeti kando mwa barabara kuu toka Singida kuelekea jijini Mwanza kuwa waaminifu katika biashara hiyo.

Joel ametoa wito huo mwishoni mwa juma hili wakati akiongea na kikundi cha vijana kilichopata mkopo takriabani milioni 8 toka Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kupitia mapato ya ndani na kujishughulisha na kuuza mafuta ya alizeti kando kando mwa barabara kuu eneo la Shelui wilayani hapa.

“Niwaombe ndugu zangu nyinyi kama kikundi msifanye udanganyifu katika biashara kwa sababu kufanya hivyo kunauwa biashara.” Alisema Joel na kuongeza kuwa

“Nivizuri nyinyi mjaze kipimo kilicho sawa na kuuza kwa bei yenye maslahi kwa kuzingatia ujazo wa lita 5 bei yake na lita 4 kuwa na bei yake.”

Aidha amekipongeza kikundi hicho cha vijana kwa ubunifu wa kutumia fursa za mikopo inayotolewa na Halmashauri hiyo,

Alieleza kuwa uthubutu huo utawasaidia vijana hawa na wanaowazunguka waweze kujikwamuwa kimaisha.

“Endeleeni kujituma na kuzingatia uaminifu kwa sababu biashara yoyote inajengwa na uaminifu. Hivyo muwe waaminifu sana, msifanye udanganyifu hata kidogo na hata kama mafuta yataadimika jitahidini muwe wakweli” Alisisitiza

Akiunga juhudi za kikundi hicho cha vijana Mkuu wa Wilaya hiyo, Suleiman Mwenda amekiahidi kikundi hicho kukipatia tofali 200 ili kujenga ofisi kwa lengo la kuendeleza biashara zao kisasa.

“Kwa namna ya kipekee niwapongeze maana ni vikundi vichache ambavyo Serikali inapokuwa imetoa fedha ukaona matokeo kwa kutoa marejesho yake kwa wakati namna ilivyopangwa. Alisema Mwenda

Pia amevisifu vikundi vya akina mama kwa kuwa waaminifu na pale wanapokuwa wamepatiwa fedha wanaitumia kwa namna ambavyo walivyoomba na kuwa na tabia ya kurejesha makato kwa wakati ukilinganisha na vikundi vya vijana wakiume.

Akiongea na kikundi cha vijana hao Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Innocent Msengi aliwaahidi kuwa ikiwa watakuwa wanarejesha makato yao  kwa wakati endapo wataomba tena watapanuliwa wigo wa kuongeza kiwango cha fedha ili wafanye biashara yao kwa kuzingatia malengo yao.

Awali akiwasilisha taarifa fupi ya kikundi cha Jitume Grupu mbele ya Kamati ya Siasa ya Wilaya hiyo, Neema Shalua alisema kuwa kikundi kimekuwa na mafanikio yakupata mkopo usio na riba takribani Tsh 8.6 milioni.

 Kufuatia hali hiyo kikundi hicho kimemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kuhimiza Halmashauri kutoa mikopo hiyo kwa sababu kupitia mikopo hiyo imewezesha kuinua kipato cha mwanachama mmoja mmoja ndani ya kikundi chao.

Kwa upande wake katibu wa Chama cha Mapinduzi, Mwal. Ephraim Kolimba aliwaasa vijana hao kuwa na ofisi inayotambulika.

“Naomba mtambue vijana kuwa fedha hizi mnazokopeshwa ni za Serikali, hivyo mnapokuwa na ofisi inayotambulika mnaweza pata hata viongozi wakanunua kwenu ambapo itakuwa ni sehemu ya fedha ya Serikali.” Alisema Komredi Kolimba

Naye Mwenyekiti wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi, Joseph Mnemba alimuomba Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kutoa kipaombele kila fursa ya fedha inapokuwa imepatikana kwa vikundi ambavyo vinajituma katika shughuli za ujasiriamali.

Kikundi cha Jitume Grupu kina jumla ya Wanachama 10 na kinajishughulisha na uuzaji wa mafuta kando mwa barabara kuu itokayo Singida kuelekea jiji la Mwanza.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.