• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Naibu Waziri, Stela Ikupa akihutubia ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri Simion Tiyosela na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba, Linno Mwageni. Picha na Hemedi Munga

Posted on: August 22nd, 2019

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@singidadc.go.tz

Iramba. Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu na Katibu Mkuu Sera, Uratibu na Uwezeshaji, Stela Ikupa emewaasa wanafunzi wa msingi na sekondari kiomboi wilaya ya Iramba Mkoani Singida Tanzania kuwa mabalozi wazuri  kwa wenzao kwa kutokujiingiza katika mapenzi katika umri mdogo na kumshika mungu ili wawe na hofu yamungu itakayowafanya kuepukana na kutojingiza kwenye mambo ambayo ni kinyume na maadili.

Naibu Waziri ameyasema hayo leo Agosti 22, 2019 wakati akitembelea mradi wa timiza malengo kwa wasichana baleghe na wanawake vijana katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.

Akiongea na wasichana na wanafunzi hao  amewataka kutokujiingiza katika mapenzi katika umri mdogo yakayowasababishia kupata mimba, kukatisha  ndoto zao na kupata maambukizi ya ukimwi. Aliongeza Ikupa

Hayo yamekuja wakati akisikiliza taarifa fupi ya utekelezaji wa mradi wa timiza malengo kwa wasichana baleghe na wanawake vijana unaotekelezwa wilayani Iramba uliopata ufadhili kutoka Mfuko wa Dunia kwa ajili ya kutekeleza mradi wa mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU) na athari za UKIMWI kwa wasichana baleghe na wanawake vijana nchini kutoka Januari, 2018 mpaka Desemba, 2020.

Akisoma taarifa fupi ya Mradi Mratibu wa TASAFU Wilayani Iramba, Adam Msangi amesema lego la mradi ni kuwasaidia wasichana walioko shuleni kuendelea na kuhitimu masomo yao na kufikia ndoto zao wakiwa salama dhidi ya VVU na UKIMWI.

 Msangi aliongeza kuwa mradi huo unawahusu pia wale walio nje ya mfumo wa elimu kupata stadi za maisha ikiwemo ujasiriamali na kupewa mtaji utakaowawezesha kuanzisha miradi ya kiuchumi ili kujikimu kimaisha wakiwa salama dhidi ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI.

Mpaka sasa wasichana 2,730 katika vijiji 50 vilivyopo kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini  (TASAFU) Wilayani Iramba walinufaika na  mradi. Alisema Msangi

Ambapo wasichana walionufaika na mradi huo walio ndani ya mfumo ni 1,372 huku wale walio nje ya mfumo wa shule ni 1,358.

Akibainisha  walengwa hao wamekwisha patiwa Tsh140 .7milioni katika awamu mbili za Novemba, 2018 na Februari, 2019 ili ziwasaidie kupata madaftari, kalamu, sare  za shule pamoja na vifaa vingine muhimu vya kujisomea na kujifunzia.

Akitoa ushuhuda Rosemary Shani kwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe, Rais John Pombe Magufuli pamoja na wadau mbalimbali kama vile TACAIDS kwa kuwakumbuka wasichana ambao ni kundi muhimu.

Ameongeza kuwa amenufaika kwa kupata mafunzo ndani ya Mkoa wa Singida yanayohusu afya ya uzazi, jinsi ya kujikinga na magonjwa ya ngono pamoja na UKIMWI, Stadi za maisha na jinsi ya kuepuka unyanyasaji wa kijinsia vilivyo muwezesha kujikinga na mimba za utotoni na magonjwa ya ngono.

Kupitia mafunzo hayo aliweza kuwaelimisha mabinti zaidi ya 500 waliopo ndani na nje ya kata katika maeneo ambayo hayafikiki kwa urahisi

kupitia njia ya kupata ujumbe mfupi unaoweza kuwapa elimu kuhusu afya ya uzazi na kujiepusha na tabia hatarishi. Alisema Shani

 Kwa upande wake mwanafunzi wa sekondari ya New – Kiomboi kidato cha tatu Wilayani Iramba   , Loyce Juma ameshukuru kuanzishwa kwa mradi huu ambao umemuwezesha kutimiza mahitaji yanayotakiwa kwa muda kama vile  daftari na sare za shule .

“Mradi huu umeniwezesha kutimiza mahitaji yangu muhimu kwa mda unaotakiwa na kufanya nipate elimu ya afya, kujitambua mimi ni nani na kujithamini katika jamii na kiuchumi, kuepukana na vishawishi vya kujiingiza katika mahusiano katika umri mdogo, kupata taulo za kike na kua jasiri ninapokuwa shuleni kwa kuniongezea umakini wakati wa hedhi’ Alisema Loyce

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni  amemshukuru mhe, Rais John Pombe Magufuli  kwa jitihada anazoendelea kuzifanya kwa ajili ya kuliendeleza Taifa Letu.

Amewataka walimu wa shule za msingi, Sekondari  na wanufaika wote wa mradi huu  kuendelea kujifunza na kuyachukua yote yalifundishwa hapa  kwenda nayo ili kutambua Taifa letu kwa sasa liko wapi na sasa tunatakiwa tujenge misingi ya namna gani liende wapi. Aliongeza Linno

Mradi wa timiza malengo kwa wasichana baleghe na wanawake vijana Tanzania unatekelezwa katika Wilaya 10 ambazo ni Kilombero, Ulanga na Malinyi Mkoa wa Morogoro, Mpwapwa, Kongwa, Bahi na Kondoa Mkoa wa Dodoma, Iramba, Singida MC na Singida DC Mkoani Singida.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.