• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Lemomo Kiruswa amemuagiza Mwekezaji wa kampuni ya Sunshine inayojishughulisha na kuchimba madini ya dhahabu katika kijiji cha Nkonkilangi wilayani Iramba mkoa wa Singida kuhakikisha anatoa ajira kwa wanawake.

Posted on: January 19th, 2022

Na hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Lemomo Kiruswa amemuagiza Mwekezaji wa kampuni ya Sunshine inayojishughulisha na kuchimba madini ya dhahabu katika kijiji cha Nkonkilangi wilayani Iramba mkoa wa Singida kuhakikisha anatoa ajira kwa wanawake.

Dkt Kiruswa ametoa agizo hilo leo Jumanne Januari 18, 2022 wakati alipofanya ziara katika kampuni hiyo inayochimba madini ya dhahabu katika kijiji cha Nkonkilangi wilayani hapa.

“Sisi serikali tutaendelea kukusaidia kuweka mazingira rafiki, hivyo hakikisha jamii inayokuzunguka inafurahi.” Alisema Naibu Waziri huyo na kuongeza kuwa

“Waajiri vijana wa hapa na hasa wanawake wanapohitajia ajira wape ajira kwa sababu wanaouwezo wa kufanya kazi.”

Jambo la wawekezaji kutoa ajira kwa jamii inayowazunguka linaifurahisha serikali.

Aidha amewahakikishia wawekezaji katika sekta ya madini kote nchini kuwa serikali imeweka mazingira rafiki yenye amani, usalama kwa kuzingatia taratibu, sheria na kanuni za nchi ili wazalishe wapate fainda, jamii zinufaike na serikali pia ifaidike.

“Ndugu zagu niwaambie kuwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan ametutuma kuwafikishia wawekezaji katika sekta zote ujembe kuwa Rais amefungua dirisha la kuwekeza katika sekta mbalimbali zitakazokuza uchumi, njooni muwekeze mpate faida na serikali ipate faida.” Alisema na kuongeza kuwa

“Tutafanya kila linalowezekana kuweka mazingira rafiki kwa sababu tunawapenda wawekezaji.”

Pia amewataka wawekezaji hao kuendelea kulipa kodi na kudumisha mahusiano mazuri kati yao na jamii inayowazunguka.

Lengo la serikali ni kuona wawekezaji wasiwe chanzo cha migogoro na badala yake walete neema na wao wapate neema.

Akiongea katika ziara hiyo Mkuu wa wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amemuhakikishia Naibu Waziri huyo kuwa serikali ya kijiji imekuwa mstari wa mbele kumsaidia kutatua migogoro inayodaiwa kuibuka katika mgodi huo.

Awali akiwasilisha taarifa yake mwekezaji wa kampuni ya Sunshine inayochimba madini ya dhahabu katika kijiji hicho, Ndugu Narcis alisesma kuwa anatoa shukrani kwa Mkuu wa Wilaya hiyo kwa kuwa mara wanapopata tatizo huwa analitatua na wanapohitajia msaada huwa wanaupata haraka.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho, Mohammed Abasi akamueleza Naibu Waziri huyo kuwa wanamuomba mwekezaji huyo kuanza kutekeleza mradi wa ujenzi wa Zahanati na kujenga madarasa katika shule mpya ya msingi katika kata hiyo kwa sababu tayari amaeanza uzalishaji.

“Kwa kweli mwakezaji huyu hana shida kabisa, hivyo kwa sababu ameanza uzalishaji tunamuomba ahakikishe anatekeleza makubaliano yetu ya kujenga Zahanati na madarasa katika shule mpya ya msingi.” Alisema Abasi.

Naye mmoja kati ya watumishi wa kampuni hiyo anayelinda eneo la kuwekea maji yanayodaiwa kuwa na chembechembe za kemikali, MG 4281 alisema kuwa katika kampuni hiyo kunachangamoto nyingi huku akitolea mfano wa kutokuwa na vifaa vya kuvaa mikononi pindi wanapo safisha eneo hilo.

“Tunaiomba serikali kuliangalia hili suala kwa sababu tunafanya kazi ambayo sio sahihi na ambayo ni hatarishi sana.” Alisema

MWISHO

Tangazo

  • WAHI NAFASI YA AJIRA August 19, 2021
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • TANGAZO LA KULIPA KODI YA ARDHI. February 26, 2018
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC Mwenda aahidi ufadhili masomo nchini China matokeo mazuri kidato cha 6 Iramba

    May 09, 2022
  • Waumini Iramba wamuombea Dua ya Kheri na Mafanikio Rais Samia kumi la mwisho Ramadhani

    May 01, 2022
  • DC Mwenda awapongeza viongozi ukamilishaji kuweka vibao anwani za makazi Iramba

    May 01, 2022
  • DC Mwenda awajaza matumaini watumishi Rais Samia kutamka neema Mei Mosi

    April 29, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.