• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo ameambatana Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Mhe: Immanuel Luhahula, kutembelea wachimbaji wadogo wadogo na kutatua migogoro yao katika eneo la mlima Sekeke Misigiri wilayani Iramba

Posted on: October 11th, 2019

Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo akizunguka katika eneo la wachimbaji wadogo wa Madini ya dhahabu katika eneo la mlima Sekenke Misigiri Wilayani Iramba Mkoa wa Singida

Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo ameambatana  Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Mhe: Immanuel Luhahula, Afisa Madini Mkoa wa Singida Chone Malembo kutembelea wachimbaji wadogo wadogo na kutatua migogoro yao katika eneo la mlima Sekeke Misigiri wilayani Iramba mkoa wa Singida.

Naibu waziri stanslaus nyongo amewasili katika eneo hilo kwa ajili ya kusikiliza mgogoro wa wachimbaji madini ya dhahabu uliodumu takribani miaka 3 kati ya John Rutebeka na Nabii Elia katika eneo la wachimbaji wadogo lililopo katika Mlima wa Sakenke Misigiri Wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

Baada ya kusikiliza kero hizo, Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo, amewagiza John Rutebeka, Nabii Elia na Afisa Madini wa Mkoa wa Singida, Chone Malembo wafike ofisini kwake Jijini Dodoma siku ya Jumatano Oktoba 16 2019 ili wakae pamoja kwa ajili ya kutatua mgogoro huo na kila mmoja aje na vielelezo vinavyomruhusu kuchimba madini katika eneo hilo. “Mje dodoma jumatano tarehe 16.10.2019, mje ofisini tukae kwa pamoja na tume ya madini ili tutatue mgogoro huu, kila mmoja anahaki yake” alisema Mhe: Nyongo

Mhe; Nyongo ametumia fursa hiyo kuwataka watalamu wa Madini kuhakikisha kuwa wanaendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo ili matatizo kama hayo yanayojitokeza sasa yasiendele kujitokeza kwani ni wajibu wao kuhakikisha kuwa migogoro baina ya wachimbaji inakwisha. “Hawajui sheria na taratibu za uchimbaji, wangekuwa wanajua sheria na taratibu, watu hawa wasingekuwa wanagombana, lazima muwaelimishe, arafu mtu anapomiliki ardhi ya juu (surface area) ajue ana haki gani, na yule anayemiliki lesseni (mineral rights) ya uchimbaji ajue ana haki gani. Na pale wanapokuwa wanagongana lazima tuwasaidie na lazima tuwasaidie wanaoomba lesseni za uchimbaji, mtu ameona eneo lake linamadini anataka kuomba lesseni, anapokelewa na afisa wa madini lakini hawamuelekezi na kumsadia. Hizo lesseni zisitoke kwanza hadi mgogoro huu umetatuliwa”, Alisistsiza Mhe: Nyongo.

Naibu Waziri Nyongo, amemtaka Nabii Elia aachane na uchimbaji wa madini karibu na nguzo za umeme anatakiwa awe mita 100 kutoka kwenye nguzo za umeme, vinginevyo atachukuliwa hatua. “Buffer area inatakiwa kuwa mita 100 hakuna kuchimba chini ya nguzo ya umeme, hatutaki disturbance ya nguzo za umeme”, alisisitiza Mhe: Nyongo

Amewataka wachimbaji wadogo wadogo kutafuta lesseni kwa kuwa kutokana na wagunduzi wengi kuchimba bila kushirikisha uongozi wa kijiji, wilaya na vyama vya wachimbaji madini wamejikuta wakitoa mwanya kwa wajanja kuomba leseni hivyo kuzalisha migogoro isiyokwisha.

Alisema kuwa Serikali kupitia Tume ya Madini imeweka utaratibu mzuri sana wa kumlinda mgunduzi wa madini tangu anapogundua madini hayo hadi kupata leseni.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.