• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa amesikiliza kero na changamoto mbalimbali za watumishi wa wilaya ya Iramba Mkoani Singida na kuzitolea majibu. Picha na Hemedi Munga

Posted on: January 8th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa amesikiliza kero na changamoto mbalimbali za watumishi wa wilaya ya Iramba Mkoani Singida na kuzitolea majibu.

Dkt. Mwanjelwa amezungumza na watumishi mbalimbali wa wilaya ya Iramba katika kikao kilichofanyika leo  Alhamisi Januari 8, 2020 katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba mjini hapa.

Katika kikao hicho Dkt. Mwanjelwa  amewataka waajiri kote nchini kutenga muda wa kutoa elimu kwa watumishi  waliopo katika mamlaka zao.

 “Ninawaagiza waajiri wote nchini    muwatendee haki watumishi waliopo katika mamlaka zenu,  inaelekea watumishi wengi hawajui haki zao kiasi ambacho hushindwa  kuelewa sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma hivyo kusababisha malalamiko mengi yasio kuwa ya msingi”

 “Nanyi watumishi wa umma  mnapaswa kushukuru  kuwa mmekuwa watumishi wa umma, kuwa mtumishi wa umma ni hadhi kubwa kwa serikali inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli hivyo  utumishi wa umma ni neema mnapaswa kuitendea haki”

“ Utumishi wa umma ni fursa kwa kuwa kila idara na sekta zinahitaji rasilimali watu kufikisha huduma kwa wananchi,” alisisitiza Dkt. Mwanjelwa

Pia amewataka kuwa wavumilivu wakati serikali inazifanyia kazi changamoto mbalimbali za utumishi huku akiwataka kuacha kuiga yasiofaa na kuwa na tabia ya kushauriana haswa pale unapoona mwenzio anafanya vibaya.

Akiongelea suala la uhamisho wa watumishi amewataka kutumia utaalamu wao kuboresha mapato ya serikali kama sehemu hiyo ilikuwa na changamoto ya kuwa na mapato hafifu.

 

Hata hivyo amewataka waajiri wote nchini kuwatendea haki watumishi wote wanaotaka kuhama kuwaidhinishia uhamisho wao nasio kuziweka barua zao katika droo kwani uhamisho hutolewa na katibu mkuu wa wizara inayohusika.

 Akitoa kero yake kwa niaba ya maafisa   Tarafa wa wilaya hiyo , Afisa Tarafa wa Tarafa ya  Shelui Nicolas Makoye amemuomba Naibu Waziri huyo kuwasaidia kupata ofisi kwani ofisi wanazofanyia kazi ni chakavu na haziko kiofisi.

 

Naye mtumishi kutoka idara ya mifugo na uvuvi, Deogratius Isagala ameiomba serikali kuongeza kasi ya kulipa stahiki mbalimbali ikiwemo ya kukaimu  ukuu wa idara au kitengo.

“Mheshimiwa Naibu Waziri  ninaiomba  serikali kuanzisha programu maalumu ya kimkakati ya kuwaandaa wastafu miaka sita  kabla ya  kustafu ili kuwajengea dira na mwelekeo mzuri katika maisha baada ya kustafu utumishi wa umma, sekta ya wastaafu iliyoboreshwa inaweza ikawa fursa muhimu katika eneo la mapato na maendeleo ya nchi,” alifafanuwa Isagala

Pia Afisa Mtendaji wa kata ya  Tulya , Mwajuma Lugambwa amesema kuwa hawajawahi kulipwa madeni yao licha ya kuambiwa yalikwisha hakikiwa na kupelekwa TAMISEMI.

“Mheshimiwa Naibu Waziri tunaiomba serikali kutupatia usafiri kwani tunafanya kazi katika mazingira magumu kwa kuwa baadhi ya kata ina vijiji vingi na viko mbalimbali kiasi ambacho kufanya utendaji wetu kutofikia malengo tuliyojiwekea,” alisema Lugambwa                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                

Wakuu wa idara mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakimfuatilia kwa makini Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa wakati akizitolea majibu kero na changamoto mbalimbali za watumishi wa wilaya ya Iramba Mkoani Singida. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                                                                                

Wakuu wa idara na watumishi  mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakimfuatilia kwa makini Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa wakati akizitolea majibu kero na changamoto mbalimbali za watumishi wa wilaya ya Iramba Mkoani Singida. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.