• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Stella Manyanya akikagua ubunifu wa Benson Mkoma aliyebuni kifaa na kukiita pawatila chenye gia box ya mkanda kulingana na kazi kinazofanya katika viwanja vya Maonesho ya Kilimo Nzuguni Jijini Dodoma

Posted on: August 6th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

ded.irambadc@singida.go.tz

Dodoma. Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Eng. Stella Manyanya amesema kuwa Watanzania wako tayari  kuitimiza azma ya Tanzania ya viwanda kivitendo na kinachotakiwa sasa ni kuwaongezea ujuzi na mtaji.

 Mhandisi Manyanya ameyasema hayo leo Agosti 06, 2020 alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Uwanja wa Maonesho ya kilimo Nzuguni Jijini Dodoma na kukutana na mbunifu wa kifaa alichokiita pawatila kutokana na kazi kinazozifanya toka Wilayani Iramba.

“Ni wakati sasa kwa vijana wanaomaliza vyuo kutumia ubunifu huo kuwa ni funzo na  fusra ya kujitegemea baada ya kupata mafunzo katika vyuo vyao”  amesema Eng. Manyanya na kuongeza kuwa

“Kuna haja ya hawa wenye ubunifu walio na maono ya kubuni vifaa mbalimbali kuungana na wale waliotoka masomoni wenye maono na ujuzi wakuweza kubuni vifaa mbalimbali ili waanze kuvitengeneza.”

Amempongeza ndugu Benson Makoma kuwa mbunifu wa kifaa hicho chenye uwezo wa kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo kulimia na kupukuchukulia mahindi kwa muda mfupi.

Akitoa taarifa fupi mbele ya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Eng. Stella Manyanya mbunifu wa kifaa hicho, Benson Makoma amesema kuwa changamoto zilizokuwa zimemzunguka ndio chachu ya msingi iliyomfanya aweze kubuni kifaa hicho kiwe msaada wa kutatua changamoto hizo.

“Nilipo kaa na kutulia niliweza kubuni kifaa hichi ambacho kinanguvu ya kuvuta tela lenye magunia kumi na kinauwezo wa kupukuchua mahindi kiasi cha ngunia mia moja kwa masaa mawili,” amefafanua Makoma na kuongeza kuwa

“Kifaa hichi kinauwezo wa kukimbia kwa spidi nzuri na kwenye barabara ya aina yoyote.”

Amesema kuwa kumekuwa na changamoto hasa katika upatikanaji wa vifaa vya kuundia kifaa hicho katika maeneo ya karibu na hivyo kulazimika kuvifuata umbali mrefu.

“Hata hivyo vifaa vya kuchomelea sio vyakwangu mara kwa mara nimekuwa nikienda mji wa Shelui kwa ajili ya kuchomelea,” ameongeza Makoma

Akijibu swali la Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara aliotaka kujua kiasi cha gharama zilizotumika kukamilisha ubunifu huo, Mkoma amesema kuwa Kifaa hicho kimegharimu takribani Tsh 2.2 milioni  ambapo mpaka sasa gharama hizo  zimekwisha rudi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Jackson Masaka alihoji aina ya mafuta ambayo yanaotumika katika kifaa hicho pamoja na muda uliotumika kukibuni kifaa hicho.

Akijibu hoja hiyo, Mkoma amesema kifaa hicho kinatumia mafuta ya dizeli na kimechukua muda wa mwezi moja kukamilika.

MWISHO

Kufuatia ubunifu wa ndugu Benson Mkoma toka kata ya Mtekente Wilayani Iramba Mkoa wa Singida, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Eng. Stella Manyanya amemzawadia fedha ili kuunga mkono  juhudi zake za kutekeleza azma ya Tanzania ya Viwanda kuwa inawezekana na Watanzania wanaweza. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Idara ya Kilimo na Ushirika, Marietha Kasongo akimuonesha Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Eng. Stella Manyanya ubunifu wa pawatila iliyobuniwa na Benson Mkoma toka kata ya Mtekente Wilayani Iramba Mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Idara ya Kilimo na Ushirika, Marietha Kasongo akiongozana na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Eng. Stella Manyanya katikati na wambele kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Jackson Masaka kuelekea kwenye banda la Halmashauri ya Wilaya  hiyo liliopo kwenye Viwanja vya Maonesho ya kilimo Nzuguni Jijini Dodoma. Picha na Hemedi Munga

Mjasiriamali toka kijiji cha Doromoni kata ya Tulya Wilayani Iramba Mkoani Singida akimuonesha samaki aina ya Kamongo wanaopatikana Ziwa Kitangiri Wilayani humo, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Eng. Stella Manyanya wakati alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya hiyo liliyopo katika Viwanja vya Maonesho ya Kilimo Nzuguni Jijini Dodoma. Picha na Hemedi Munga


Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Eng. Stella Manyanya akionesha ubunifu wa chungu kilichobuniwa na Jawel Maganga toka Wilayani Iramba Mjini Kiomboi kikionesha kauli mbiu ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ya hapa kazi tu wakati alipotembelea banda la Halmashauri hiyo katika viwanja vya Maonesho ya Kilimo Nzuguni Jijini Dodoma. Picha na Hemedi Munga

Mkuu wa Idara ya Kilimo na Ushirika, Marietha Kasongo akimuonesha Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Eng. Stella Manyanya shamba darasa la alizeti liliopo viwanja vya maonesho ya Kilimo Nzuguni Jijini Dodoma. Picha na Hemedi Munga.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.