• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Naibu Waziri Wanchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa amewapongeza wananchi wa kijiji cha kisiriri kwa kubadilisha maisha kupitia mradi wa kunusuru kaya maskini (TASAF). Picha na Hemedi Munga

Posted on: January 8th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Naibu Waziri Wanchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa amewapongeza wananchi wa kijiji cha kisiriri kwa kubadilisha maisha kupitia mradi wa kunusuru kaya maskini (TASAF).

Mwanjelwa ameyazungumza hayo wakati wa ziara yake leo Ijuma tano Januari 8, 2020 kijiji cha Kisiriri Tarafa ya Kisiriri Wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

Akiongea na wananchi katika ziara hiyo, amewataka kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania, Dkt. John  Pombe Magufuli kwa kuleta zaidi ya 120 milioni  kijijini hapo huku zaidi  6.9 bilioni zimeletwa kwa wilaya nzima.

Amewaeleza kuwa Rais Magufuli amekubali mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF) awamu ya pili kuendelea huku akiwahakikishia kuwa vijiji 70 vitafikiwa na mradi huo ukuilinganisha na awamu yakwanza ulionufaisha vijiji 50.

Utaratibu wa kuchaguwa kaya maskini umeboreshwa ili kuepusha uchakachuaji na itapita timu nyingine kujiridhisha kama zoezi hilo limefanyika sawasawa.

“Tutakuwa tunakuja  kwenye kaya kuona kwa macho na itapita timu nyingine kujiridhisha, ” alisisitiza Mwanjelwa

Aidha amewataka kuyaishi yale wanayoyatolea ushuhuda kuwa ni tija waliyonufaika kipitia mpango wa kunusuru kaya maskini(TASAF).

Mwanzoni akisoma taarifa fupi ya Mpango wa kunusuru  Kaya maskini (TASAF) mbele ya Naibu Waziri Wanchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, kaimu Afisa Mtendaji wa kijiji, James Shani amesema mradi huo umewawazesha kutekeleza shughuli nyingi.

Shani amezitaja shughuli zilizotekelezwa kuwa  ni uhaulishaji fedha za ruzuku na utimizaji wa masharti ya afya na elimu, pili ni ajira ya muda mfupi, tatu ni fedha za vifaa vya utekelezaji wa ajira ya  muda mfupi huku akihitimisha na ujenzi wa miundombinu katika maeneo maalum katika sekta za afya na elimu.

Mradi huo umeweza kuwanufaisha wasichana balehe 1,372 kwa kuwapa fedha za kujikimu maisha.

Kugawa taulo za kike 8,910 kwa wasichana balehe 1,372 huku akibainisha kuwa wasichana balehe 827 walio nje ya mfumo wa shule wameweza kupata mafunzo ya ujasiriamali, uwandaaji wa mpango wa biashara katika kata 17 na vijiji 50 vilivyoko kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini(TASAF), alisema Shani.

Aidha amemuhakikishia Naibu Waziri kuwa Halmashauri imechukuwa hatuwa mbalimbali za ufumbuzi wa changamoto anuwai ikiwa ni pamoja na kuendelea kuielimisha jamii  kuhusu malengo na dhamira ya serikali na wadau wa maendeleo kuhusu kutoa fursa mbalimbali za kupunguza umaskini.

Akitoa ushuhuda wa kunufaika na mpango wa kunusuru kaya maskini(TASAF), Esta Makala (80) amesema ameweza kununua bati 23 na kusogeza mawe kwa ajili ya ujenzi wa nyumba.

Naye Upendo Mashantala amesimulia kuwa alikuwa na hali mbaya ya kukosa chakula na mahali pazuri pakulala, lakini baada ya kupewa ruzuku kupitia mpakongo wa kunusuru kaya maskini  (TASAF)  aliweza kununua mbegu bora zilizomuwezesha kupata mahindi na baada ya kuyauza aliweza kujenga nyumba ya bati.

Kwa upande wake Sara Kiongo amesema kuwa ameweza kunufaika kupitia mradi huo kwa kununuwa mbuzi na kulipia kadi ya CHF iliyoboreshwa kwa ajili ya kulinda afya zao.

Kupitia mpango wa mafunzo ya timiza malengo yalioendeshwa kupitia mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF), Lucyana Shaluwa amesema wamejifunza kujiamini, namna ya kupanga bei kulingana na mshindani wako, kuzifahamu faida na hasara na kujiepusha na makundi yasio stahili kama vile  uvutaji bangi, uvutaji wa madawa ya kulevya, kuingia kwenye ndoa za utotoni na  mimba za utotoni.

Akiongea katika ziara hiyo katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Iramba, Ibrahimu Mjanaheri amemsifu Rais wa Tanzania, John Magufuli kwa kutekeleza kwa vitendo miradi mbalimbali.

Mjanaheri amesema Hospitali za wilaya 99 zimejengwa kwa kipindi cha miaka 4 ukilinganisha na wakati  anaingia madarakani 2015 ambapo kulikuwa na hospitali 77.                                                                                                                                                                       

Naibu Waziri Wanchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa katikati akienda kwenye nyumba ya mnufaika wa mpango wa kunusuru kaya maskini ili kuangalia utekelezaji wake, kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula wakati kushoto kwa Naibu Waziri ni Adamu Msangi Mratibu wa Mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF) Iramba. Picha na Hemedi Munga                                                                           

Naibu Waziri Wanchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa akiwa na wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF) huku kushoto kwake ni Adamu Msangi Mratibu wa Mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF) Iramba. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.