• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Ndani ya siku 365 za Rais Samia aleta 89 bilioni zatekeleza miradi ya maendelo Iramba

Posted on: March 22nd, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

        

Singida - Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda aliwaeleza wajasiriamali kazi kubwa na mafanikio lukuki yaliopatikana wilayani Iramba ambayo ameyafanya Rais Samia ndani ya mwaka mmoja wa uwongozi wake.

Mwenda alieleza mafaniko hayo mwishoni mwa juma hili wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya ujasiriamali yalioendeshwa na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) katika ukumbi mdogo wa mikutano wilayani hapa.

Akielezea kuhusu takwimu za watu nchini, alisema kuwa akina mama ni wengi ukilinganisha na wananume.

“Wanawake ni kundi muhimu sana kwa sababu ukimuelimisha na kumuwezesha mwanamke unakuwa umeiwezesha na kuielimisha jamii” Alisema Mwenda

Aidha, alilipongeza Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) kwa kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa akina mama 49 na wanaume 8 ambao hivi karibuni wataanza kuzalisha matokeo chanya yatakayoinufaisha jamii.

Halikadhalika, alimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Mhandisi Michael Matomora kwa kutenga takribani Tsh 140 milioni kwa ajili ya akinamama, vijana na watu wenye mahitaji maalumu.

“Ni dhahiri kuwa mitaji na teknolojia hii mlioyoipata kutoka SIDO inawawezesha kuendesha shughuli za kusindika karanga, vitunguu, nyanya, mvinyo na kutengeneza keki, hivyo mazao yetu yataongezeka thamani na kuwakwamuwa wajasiriamali wetu katika nyanja ya uchumi.” Aliongeza

Kufuatia mafunzo hayo, Mwenda alitumia jukwaa hilo kuwataka wajasiriamali kutumia fursa ambazo zinakuja katika wilaya ya Iramba kupitia mradi wa bomba la mafuta, uwepo wa mafuta katika Bonde la Wembere, madini ya dhahabu na madini ya almasi yaliogundulika hivi karibuni.

“Sisi kama wajasiriamali nilazima tujipange kuzitumia fursa ambazo Rais Samia anazileta kwetu, hivyo tujipange kuuza vyakula, kupeleka vifaa vya ujenzi na shughuli za ulinzi.” Alisema

Halikadhalika, tunayo matarajio ya kupata kiwanda kikubwa cha mbolea wilayani hapa, hivyo tunatarajia kubadilisha maisha ya wananchi kupitia shughuli mbalimbali na muingiliano wa watu watakaohudumu katika kiwanda hicho.

Katika hatua nyingine yamafaniko yaliopatikana wilayani hapa baada ya kutimia mwaka mmoja wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, Mkuu huyo wa wilaya alielezea mafanikio lukuki yaliyopatikana Iramba katika utawala wa Rais huyo.

Alifafanua kuwa wakati Rais Samia anaingia madarakani upatikanaji wa maji wilayani Iramba ulikuwa asilimia 26 lakini ndani ya mwaka mmoja wa utawala wake upatikanaji wa maji umefikia asilimia 59 ambapo kuna miradi mikubwa ya maji yenye thamani ya takribani 4.8 bilioni inatekelezwa katika maeneo tofauti tofauti.

Katika sekta ya afya tangu kupatikana kwa uhuru wilaya ya Iramba ilikuwa na vituo vya afya 3 lakini ndani ya mwaka mmoja wa Rais Samia ameweza kujenga vituo vya afya 5 ambapo kila kimoja kinagharibu takribani Tsh 500 milioni.

Pia, aliongeza kuwa katika Hospitali ya wilaya kunaujenzi unaendelea wenye thamani ya takribani Tsh bilioni moja.

Akiongelea kuhusu sekta ya elimu, Mwenda alisema kuwa Rais Samia alileta takribani Tsh 2 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa ambapo wilaya imefanikiwa kujenga vyumba vya madarasa 57 nakufanikiwa kutokomeza upungufu wa madarasa wilayani hapa.

Katika sekta ya nishati wilaya ya Iramba ilikuwa na vijiji 46 vyenye umeme na vijiji 14 ambavyo havina umeme ambapo tayari Rais Samia aliishaleta fedha kwa ajili ya kumalizia vijiji 14 vipate umeme na kufanya vijiji vyote vya wilaya hii kuwa na umeme.

Aidha, aliongeza kuwa kupatikana umeme wilayani hapa kutawezesha wajasiriamali wadogo kufanya shughuli za usindikaji wa bidhaa mbalimbali wakati wote na popote hatimaye kuweza kujikwamuwa kiuchumi.

Akiongelea kuhusu sekta ya barabara na miundombinu, alisema kuwa wilaya imepata zaidi ya Tsh 80 bilioni kwa ajili kutengeneza barabara kwa kiwango cha lami inayoanzia Kizaga, Mukulu, Ndago, Mbelekese hadi Singida mjini.

“Haya ni mafanikio makubwa sana ambayo tunajivunia na hivyo tutaendelea kuwasimamia watumishi wenzetu ili kutimiza azma ya viwango na mafanikio ambayo Taifa linategemea kuyapata.” Alisisitiza

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Mhandisi Michael Matomora aliwahimiza wajasiriamali hao kuyaingiza mafunzo walioyapata kivitendo ili kupata viwanda vingi nchini.

“Nendeni mkayatumie mafunzo haya kama mwanzo wa kutengeneza viwanda vikubwa vilivyo katika ndoto zenu.” Aliagiza

Naye mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo kwa niaba ya wanafunzi wote, Emmanuel Yohana alimshukuru Rais Samia kwa kufanikisha kufadhili mafunzo haya kupita Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) lililofandhiliwa na Shirika la elimu (TEA).

Yona alisema kuwa wamefanikwa kujifunza kwa nadharia na vitendo na hivyo wanauwezo wa kuzalisha bidhaa mbalimbali zinazohitajika katika jamii yao.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.