• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mradi wa maji wa Shilingi milioni 588,756,487 wakabidhiwa Kijiji cha Mugungia kata ya Kasely wilaya ya Iramba mkoa wa Singida.

Posted on: August 4th, 2018

Muwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Ndg. Dijovison Ntangeki akiongozana na wataalamu wa maji amekabidhi Mradi wa maji wa Shilingi milioni 588,756,487/=, Katiba na Hati ya usajili wa jumuiya ya watumia maji (WASOWA) Kijiji cha Mgungia kata ya Kaselya Wilayani Iramba.

Muwakilishi Mkuu wa Wilaya ya Iramba akizungumza na wananchi amesema Mradi huo umekabidhiwa katika mikono salama hivyo wakazi wa Kijiji cha Mgungia watapata huduma ya Maji safi na salama. Ameongeza kwa kusema nimatumaini kwamba kasi ya magonjwa yatokanayo na Matumizi haba ya maji yatapungua, utoro wa wanafunzi shuleni utapungua unaosababishwa na muda mwingi kutumika kutafuta maji mbali na makazi wanakoishi.

Ndg. Ntangeki amesema jukumu lao ni kuhakikisha wananchi wa Mgungia wanapata maji hivyo wananchi watoe ushirikiano katika kutunza miundo mbinu iliyopo na kutoa taarifa pindi wanapoona bomba linavuja.

Ndg. Ismail Ally Ghone, Mwenyekiti wa Kijiji cha mugungia Akipokea mradi huo kwa niaba ya wananchi, ameshukuru Halmashauri ya wilaya ya Iramba kwa kuendelea kuchangia maendeleo ya jamii na kuhaidi kutuza miundo mbinu ya mradi huo.

Akisoma Taarifa ya Mradi wa maji, Mwandisi Athuman Mkalimoto alisema Mradi huu umetekelezwa na Halmashauri ya wilaya ya Iramba na umekabidhiwa kwa jumuiya ya watumiaji maji (WASOWA) Kijiji cha Mugungia kata ya Kaselya, Mradi ulianza kutekeleza Juni 2014 na kukamilika mwezi Novemba 2017.

Mpaka kukamilika kwa mradi huu, umetumika shilingi Milioni 588,756,487/= na shilingi Milioni 5 nguvu za wananchi.

Lengo la mradi ni kuwapatia wananchi wa Kijiji cha Mugungia huduma ya maji safi na salama pamoja na kuboresha Afya na kuinua shughuli za kiuchumi za Wananchi.

Mradi wa maji katika Kijiji cha Mugungia ulitokana na Wananchi wa Kijiji hiki kuchagua kuwa ni kipaumbele chao, hivyo waliamua kuomba mradi wa maji kutokana na shida ya maji iliyokuwa inawakabili hapo awali.

Aidha mradi huo wa maji unahudumia wananchi wapatao 5,375 chenye vitongoji vitano vya Ndyala kati, Ndyala juu, Mwandu, Ugani na Msisi kwa kuwapatia huduma ya maji safi na salama karibu na makazi wanayoishi ndani ya umbali wa mita 400 kutoka mita 1500, pia mradi wa maji unahudumia mifugo 5,689 kwa kupata huduma ya maji ya uhakika kwenye milambo miwili ya mradi iliyojengwa.



Announcements

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.