• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mradi wa maji wa Shilingi milioni 588,756,487 wakabidhiwa Kijiji cha Mugungia kata ya Kasely wilaya ya Iramba mkoa wa Singida.

Posted on: August 4th, 2018

Muwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Ndg. Dijovison Ntangeki akiongozana na wataalamu wa maji amekabidhi Mradi wa maji wa Shilingi milioni 588,756,487/=, Katiba na Hati ya usajili wa jumuiya ya watumia maji (WASOWA) Kijiji cha Mgungia kata ya Kaselya Wilayani Iramba.

Muwakilishi Mkuu wa Wilaya ya Iramba akizungumza na wananchi amesema Mradi huo umekabidhiwa katika mikono salama hivyo wakazi wa Kijiji cha Mgungia watapata huduma ya Maji safi na salama. Ameongeza kwa kusema nimatumaini kwamba kasi ya magonjwa yatokanayo na Matumizi haba ya maji yatapungua, utoro wa wanafunzi shuleni utapungua unaosababishwa na muda mwingi kutumika kutafuta maji mbali na makazi wanakoishi.

Ndg. Ntangeki amesema jukumu lao ni kuhakikisha wananchi wa Mgungia wanapata maji hivyo wananchi watoe ushirikiano katika kutunza miundo mbinu iliyopo na kutoa taarifa pindi wanapoona bomba linavuja.

Ndg. Ismail Ally Ghone, Mwenyekiti wa Kijiji cha mugungia Akipokea mradi huo kwa niaba ya wananchi, ameshukuru Halmashauri ya wilaya ya Iramba kwa kuendelea kuchangia maendeleo ya jamii na kuhaidi kutuza miundo mbinu ya mradi huo.

Akisoma Taarifa ya Mradi wa maji, Mwandisi Athuman Mkalimoto alisema Mradi huu umetekelezwa na Halmashauri ya wilaya ya Iramba na umekabidhiwa kwa jumuiya ya watumiaji maji (WASOWA) Kijiji cha Mugungia kata ya Kaselya, Mradi ulianza kutekeleza Juni 2014 na kukamilika mwezi Novemba 2017.

Mpaka kukamilika kwa mradi huu, umetumika shilingi Milioni 588,756,487/= na shilingi Milioni 5 nguvu za wananchi.

Lengo la mradi ni kuwapatia wananchi wa Kijiji cha Mugungia huduma ya maji safi na salama pamoja na kuboresha Afya na kuinua shughuli za kiuchumi za Wananchi.

Mradi wa maji katika Kijiji cha Mugungia ulitokana na Wananchi wa Kijiji hiki kuchagua kuwa ni kipaumbele chao, hivyo waliamua kuomba mradi wa maji kutokana na shida ya maji iliyokuwa inawakabili hapo awali.

Aidha mradi huo wa maji unahudumia wananchi wapatao 5,375 chenye vitongoji vitano vya Ndyala kati, Ndyala juu, Mwandu, Ugani na Msisi kwa kuwapatia huduma ya maji safi na salama karibu na makazi wanayoishi ndani ya umbali wa mita 400 kutoka mita 1500, pia mradi wa maji unahudumia mifugo 5,689 kwa kupata huduma ya maji ya uhakika kwenye milambo miwili ya mradi iliyojengwa.



Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA November 03, 2023
  • KUITWA KAZINI November 29, 2023
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wamefanya ziara ya Ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa Wilayani Iramba

    October 24, 2023
  • RAIS DKT. SAMIA AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI SINGIDA KWA KISHINDO, WANANCHI WAMSHUKURU KWA MIRADI YA MAENDELEO

    October 17, 2023
  • MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amepokea rasmi Mbio za Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoani Tabora na aliyekabidhi ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Batlida Briani.

    September 22, 2023
  • MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Abdalla Shaibu Kaim amewataka Watanzania kuhakikisha wanakemea vitendo vya rushwa kwa maelezo kuwa rushwa inakwamisha maendeleo ya Mkoa pamoja na Taifa kwa ujumla

    September 22, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.