• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

RC SERUKAMBA ATAKA KAMATI ZA FEDHA KUJADILI HOJA ZA CAG KWENYE VIKAO VYAO KILA MWEZI

Posted on: June 15th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, amewataka Madiwani ambao ni wajumbe wa Kamati ya Fedha na Uongozi kila mwezi kuweka agenda moja ya kujadili hoja za ukaguzi zinazoibuliwa kwenye Halmashauri zao na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Amesema hayo leo (Juni 15, 2023) kwenye Kikao Maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba ambacho kiliketi kwa ajili ya kujadili hoja za CAG za mwaka 2021/2022 na za miaka ya nyuma.

Serukamba ambaye aliambatana na Katibu Tawala Mkoa wa Singida (RAS), Dkt. Fatma Mganga, amesema kama Kamati za Fedha zitajiwekea utaratibu huo wa kujadili hoja za ukaguzi za CAG kutamfanya Mkurugenzi wa Halmashauri na watendaji wake kutambua kuwa Madiwani wanafuatilia kwa karibu mambo hayo.

"Tukiwa tunafanya hivyo tutajua mzembe anayetukwamisha ni nani na ikiwa Mkuu wa Idara ataonekana amekaa zaidi ya miezi sita bila kujibu hoja za CAG ambazo zinajitokeza katika idara yake tuandikieni barua kutujukisha," alisema Serukamba.

Amesema kimsingi kuwepo kwa hoja nyingi za CAG kwenye Halmashauri ni suala la uzembe wa baadhi ya watendaji kutokuwa makini kufuatilia majukumu yao na kuagiza kila mtumishi ahakikishe anawajibika ipasavyo ili kila Halmashauri kusiwe kunajitokeza hoja za CAG.

Mkuu wa Mkoa akizungumza suala la ukusanyaji mapato katika Halmashauri ya Wilaya Iramba alisema bado hali sio nzuri hasa kutokana na baadhi ya watumishi kuendelea na tabia ya kula fedha mbichi wanazozikusanya badala ya kuzipeleka benki.

Alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Michael Matomora, kukomesha vitendo vinavyofanywa na baadhi ya watumishi wenye tabia ya kufuja fedha walizozikusanya.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatma Mganga, alisema ushauri unaotolewa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) uwe unafanyiwa kazi na Madiwani na Watendaji badala ya suala hili linahusu viongozi tu Halmashauri.

Alisema Madiwani wahakikishe hoja za ukaguzi za CAG hazijirudii mara kwa mara kila mwaka kwani hali kama hiyo ikiwa inajitokeza itaweza kusababisha Halmashauri kupata hati mbaya.

Dkt. Mganga alisema kujitokeza kwa hoja nyingi za ukaguzi za CAG katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kunatokana na kutojibiwa barua kwa wakati tatizo ambalo limejitokeza kwa Halmashauri nyingine za Mkoa wa Singida.

Hata Hivyo, aliwapongeza Madiwani na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kwa jitihada kubwa walizozifanya na kupunguza hoja za CAG kutoka 113 na kubakia hoja 33.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Iramba, Michael Matomora alimhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Singida kuwa tabia ya ulaji wa fedha mbichi haitajirudia tena katika Halmashauri hiyo atakuwa anachukua hatua kali kwa Watumishi watakaobainika kufanya vitendo hivyo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Innocent Msengi, alitoa wito kwa wananchi ndani na nje ya Wilaya hiyo kujitokeza kununua viwanja vilivyotengwa na Halmashauri ili kuujenga mji wa Iramba.

Msengi alisema katika miradi ya maendeleo inayotekelezwa hivi sasa katika Halmashauri hiyo ifikapo Juni 30, mwaka huu bila shaka itakuwa umekamilika.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Innocent Msengi akizungumza kwenye Kikao Maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba ambacho kiliketi kwa ajili ya kujadili hoja za CAG za mwaka 2021/2022 na za miaka ya nyuma

 

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, akizungumza kwenye Kikao Maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba ambacho kiliketi kwa ajili ya kujadili hoja za CAG za mwaka 2021/2022 na za miaka ya nyuma.


 

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA April 29, 2023
  • Kampuni ya EACOP imeanza usajili na mafunzo ya online kwa wiki 8 yatakayofwatiwa na mtihani wiki ya 9 kwa ajili ya kupata vijana 140 wenye umri kati ya miaka 18-28 June 05, 2023
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amepokea rasmi Mbio za Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoani Tabora na aliyekabidhi ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Batlida Briani.

    September 22, 2023
  • MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Abdalla Shaibu Kaim amewataka Watanzania kuhakikisha wanakemea vitendo vya rushwa kwa maelezo kuwa rushwa inakwamisha maendeleo ya Mkoa pamoja na Taifa kwa ujumla

    September 22, 2023
  • MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA TSH BIL. 4.151 WILAYANI IRAMBA MKOANI SINGIDA; IMEFUNGULIWA NA MINGINE KUWEKEWA MAWE YA MSINGI NA MWENGE WA UHURU SEPTEMBA 22 MWAKA HUU.

    September 23, 2023
  • KITUO CHA AFYA TYEGELO CHAZINDULIWA RASMI TAYARI KWA AJILI YA KUANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA NA KUPUNGUZA CHANGAMOTO ZA AFYA KWA WANANCHI KAMA SIYO KUZIONDOA KABIS

    September 18, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.