• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Serikali ya Tanzania imesema shule zote za awali, msingi na sekondari zitafungwa kwa siku 30 kuanzia leo Jumanne Machi 17, 2020 ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi ya virusi vya Corona ( COVID–19)

Posted on: March 17th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Serikali ya Tanzania imesema shule zote za awali, msingi na sekondari zitafungwa kwa siku 30 kuanzia leo Jumanne Machi 17, 2020 ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi ya virusi vya Corona ( COVID–19)

                                        

Maamuzi hayo yametolewa na Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa leo Jumanne Machi 17, 2020 wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Amesema wanafunzi wa kidato cha sita walipaswa kuanza mitihani Mei 4, 2020 lakini na wawo watapaswa kusubiri Wizara ya Elimu ifanye utaratibu mwingine kulingana na matokeo ya hali ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Amesema mikusanyiko yote mikubwa ya ndani na ya nje isio yalazima imesitishwa kuanzia sasa ikiwamo shughuli za michezo, matamasha ya muziki, mikutano mbalimbali ikiwamo ya shughuli za kisiasa, mahafali na shughuli nyingine za kijamii.

Waziri Mkuu huyo amezitaka Wizara na Taasisi zisitishe semina, warsha, makongamano na mikutano yote hapa nchini ambayo inahusisha washiriki toka nchi zenye maambukizi makubwa.

“ Watanzania wenye safari zisizo za lazima kwenye nchi zenye maambukizi makubwa wanashauriwa wasitishe safari hizo,” amesisitiza Majaliwa

Akibainisha hatua nyingine zinazochukuliwa na serikali ili kuudhibiti ungonjwa huo, Waziri Mkuu amesema, “Serikali imesitisha michezo yote inayokusanya makundi ya watu ikiwamo ligi kuu ya Tanzania (VPL), Ligi Daraja la Kwanza (FDL), Ligi Daraja la Pili (SDL) na aina nyingine. Wizara ya Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo iziandikie taasisi zake.”

Halikadhalika, amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha maeneo yote yalioainishwa na kutengwa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa endapo watajitokeza katika maeneo yao yanakuwa na mahitaji yote muhimu na kuhudumiwa ipasavyo.

Pia, Waziri Mkuu amesema serikali tayari imetoa   Sh500 milioni kati ya Sh1 bilioni zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya mbio za Mwenge wa Uhuru zilizokuwa zianze Aprili 2, 2020.

“ Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameahirisha mbio za Mwenge wa Uhuru zilizokuwa zianze Aprili 2 mwaka huu na kuagiza sh1 bilioni zilizokuwa zimeandaliwa kwa ajili ya shughuli hiyo, zipelekwe Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ajili ya maandalizi ya kujiweka tayari kudhibiti maambukizi ya Corona. Serikali tayari imetoa milioni 500.”

Akizungumzia hatua zilizochukuliwa baada ya mgonjwa wa kwanza kubainika kuwapo nchini Tanzania, Waziri Mkuu amesema Serikali imechukua hatua ya kumchukuwa mgonjwa huyo na kumuifadhi kwenye eneo maalumu kwa ajili ya kumpatia huduma.

“ Pia, Serikali imefanya ufuatiliaji wa watu waliokutana na mgonjwa huyo tangu aingie nchini na kuwaweka kwenye karantini ya siku 14, pia kuchukuwa sampuli kwa ajili ya kubaini kama wameambukizwa virusi hivi,” amesema

 

Ugonjwa huu umeingia nchini baada ya Mtanzania mwenye miaka 46 aliyesafiri kwenda nchi za Ubeligiji, Sweden na Denmark hivi karibuni, kupimwa na kuthibitika kuwa na virusi vya Corona (COVID–19).

Akifafanua hatua zaidi zinazochukuliwa, Waziri Mkuu amesema licha ya hatua ambazo  zimechukuliwa  na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamaii, Jinsia, Wazee na Watoto Serikali itaimarisha ukaguzi na ufatiliaji wa wasafiri wanaoingia nchini kupitia viwanja vya ndege, bandari na mipaka ya nchi kavu ili kuwabaini wasafiri wenye dalili za ugonjwa na viashiria vya hatari.

“Tutaimarisha uwezo wa kupima sampuli kwa watu wanaohisiwa kuwa na viashiria au dalili za ugonjwa huo ambapo maabara yetu ya Taifa kwa sasa inauwezo wa kutoa majibu kwa haraka,” amesema

 

Amesema serikali inaendelea kuwajengea uwezo (mafunzo) watumishi wa sekta ya Afya ili kukabiliana na magonjwa ya milipuko ikiwemo namna ya kutoa tiba, kuchukua sampuli, uelimishaji na kuzingatia kanuni za Afya.

“ Serikali imetenga hospitali maalum za Mloganzila (Dar es Salaam), kituo cha Buswelu (Mwanza) na hospitali ya Mawenzi (Kilimanjaro), Mnazi Mmoja (Zanzibari) na Chake Chake (Pemba) kwa ajili ya kutoa huduma kwa waathirika.”

Ameiagiza Wizara ya Afya kuhakikisha vifaa vya kinga ikiwamo vimiminika vya kudhibiti maambukizi (Hand sanitizer) vinapatikana katika maduka yote husika na kwa bei ya kawaida huku akitahadharisha kuwa serikali itachukua hatua kwa wafanyabiashara watakaobainika kufanya uranguzi wa vifaa hivyo.

Aidha, amewataka watanzania kuzingatia ushauri unaotolewa na serikali na kupuuza taarifa za uzushi zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

“ Watanzania tuache mzaha wa kutumia mitandao ya kijamii kufanya upotoshaji wa jambo hili,” ameongeza Waziri Mkuu

 

 Amewaomba viongozi wa dini waendelee  kushirikiana na serikali kuwaelimisha waumini wao wote kuzingatia tahadhari ya ugonjwa huu huku akivitaka vyombo vyote vya habari kushirikiana na serikali kutoa elimu kwa umma kuhusu kujikinga na Corona bila ya kufanya upotoshaji wala kuipa jamii hofu.

 Amewataka wananchi watoe taarifa kuhusu uwepo wa mgonjwa au kupata ufafanuzi kuhusu ugonjwa huu kupitia namba za bure za 0800110124, 0800110125 na 0800110037.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.