• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

SERIKALI YAWAHIMIZA WAFUGAJI MKOANI SINGIDA KULINDA MIFUGO KUPITIA CHANJO NA UTAMBUZI

Posted on: July 8th, 2025

SERIKALI YAWAHIMIZA WAFUGAJI MKOANI SINGIDA KULINDA MIFUGO KUPITIA CHANJO NA UTAMBUZI


Wafugaji mkoani Singida wametakiwa kushiriki kikamilifu katika zoezi la uchanjaji na utambuzi wa mifugo yao, ambapo utekekelezaji wa zoezi hilo mkoani humo limeanza rasmi leo, Julai 8, 2025, katika Kata ya Kyengege, Kijiji cha Makunda, Wilaya ya Iramba. Lengo la zoezi hilo ni kulinda mifugo dhidi ya magonjwa na kuboresha ubora wake kwa ajili ya ushindani katika soko la kimataifa.


Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mafunzo ya Mifugo (LITA), Dkt. Pius Mwambene, amesema kuwa zoezi hilo ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya uchanjaji na utambuzi wa mifugo, iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 16 Juni 2025. Amesema kampeni hiyo inalenga kuongeza tija kwa wafugaji nchini, hivyo ni muhimu kulizingatia.


Dkt. Mwambene alieleza kuwa katika kampeni hiyo, wafugaji watanufaika na chanjo kwa gharama ya ruzuku baada ya Serikali kutoa kiasi cha Shilingi Bilioni 216 kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo kwa kipindi cha miaka mitano.


"Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alishazindua kampeni hii ya chanjo na ameridhia kuchangia nusu gharama ya chanjo ili kuwasaidia wafugaji kote nchini kuikinga mifugo yao dhidi ya magonjwa na kuimarisha biashara ya Mifugo na mazao yake katika masoko ndani na Kimataifa, hivyo wafugaji wa mkoa huu wa Singida jitokezeni na mshiriki kikamilifu kwenye kampeni hii" alisema Dkt. Mwambene.


Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Wilaya ya Iramba, Bw. Morton Msowoya, alibainisha kuwa aina za chanjo zitakazotolewa ni pamoja na chanjo dhidi ya homa ya mapafu kwa Ng’ombe, Sotoka kwa Mbuzi na Kondoo, pamoja na chanjo dhidi ya Kideli, Mafua na Ndui.


Baadhi ya wafugaji wilayani Iramba wameishukuru Serikali kwa kuwawezesha kupata chanjo kwa ruzuku, wakieleza kuwa kabla ya kuanzishwa kwa kampeni hiyo, mifugo mingi ilikufa kutokana na magonjwa mbalimbali.


Utekelezaji wa zoezi hilo kwa ngazi ya mkoa wa Singida unaendelea sambamba na uhamasishaji kwa wafugaji kushiriki kikamilifu, ambapo zaidi ya mifugo laki tano inatarajiwa kuchanjwa wilayani Iramba na zaidi ya milioni nne kwa mkoa mzima.





Tangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI KUJADILI NA KUPOKEA TAARIFA YA CAG MWAKA WA FEDHA 2023/2024 TAREHE 18, JUNI 2025 June 16, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • SERIKALI YAWAHIMIZA WAFUGAJI MKOANI SINGIDA KULINDA MIFUGO KUPITIA CHANJO NA UTAMBUZI

    July 08, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA SABASABA 2025

    July 07, 2025
  • TRA IRAMBA YAVUKA MALENGO YA UKUSANYAJI KODI KWA ASILIMIA 130, YAWASHUKURU WALIPAKODI

    July 01, 2025
  • DC MWENDA AKABIDHI SPIKA KWA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII IRAMBA

    July 01, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.