• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Shule ya msingi Kiomboi-Hospitali yawa ya kwanza kiwilaya kati ya shule 66, kimkoa 7 kati ya 375 na kitaifa 582 kati ya 9929. Picha na Hemedi Munga

Posted on: October 15th, 2019

By Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya kumaliza elimu ya msingi mwaka 2019 ambapo asilimia 81.50 ya watahiniwa 933,369 wamefaulu mtihani huo huku watahiniwa 909 wakifutiwa matokeo kwa sababu ya udanganyifu.

Akitangaza matokeo hayo leo Jumanne Oktoba 15, 2019 katibu mtendaji wa NECTA, Dk Charles Msonde amesema kwa ujumla yanaonesha ufaulu umeongezeka kwa aslimia 3.78 lakini ufaulu katika somo la kingereza bado ni mdogo ukilinganisha na masomo mengine.

“ Ufaulu katika somo la kingereza unaendelea kuimarika  mwaka hadi mwaka hivyo juhudi za maksudi zinahitajika kuendelea kufanyika ili kuinua kiwango cha ufaulu katika somo hilo” amesema Dk Msonde

Kufuatia matokeo hayo shule ya msingi Kiomboi- Hospitali iliyopo Wilayani Iramba Imekuwa ya kwanza katika wilaya hiyo.

Shule hiyo iliyopo katika kundi la wanafunzi 40 au zaidi imekua ya kwanza kihalmashauri kati ya shule 66, kimkoa ya 7 kati ya 375 na kitaifa 582 kati ya 9929.

Huku nafasi ya pili kiwilaya ikishikwa na shule ya msingi Misigiri, yatatu shule ya msingi Lulumba, yanne shule ya msingi Kiomboi-Bomani na ya tano ni shule ya msingi Kidaru.

Huku kundi la wanafunzi chini ya 40 katika wilaya hiyo shule ya msingi Salala imekuwa yakwanza kati ya 22, kimkoa ya 25 kati ya 156 na kitaifa 2608 kati ya 7102.

Wakati nafasi ya pili katika kundi hilo ikishikwa na shule ya msingi Ndurumo, yatatu shule ya msingi Munkonze, ya nne shule ya msingi Motomoto na ya  tano shule ya msingi Mukulu.

Huku shule ya msingi Msansao ikishika nafasi ya mwisho kiwilaya 66 kati ya 66, kimkoa 375 kati ya 375 na kitaifa 9920 kati ya 9929.

Hata hivyo shule ya msingi Ntwike na shule ya msingi sekenke hazijawekewa matokeo.

Shule 10 bora kitaifa ni Graiyaki ya Mara, Twibhoki ya Mara, Kemebos ya Kagera, Little Treasures ya Shinyanga, Musabe ya Mwanza, Tulele ya Mwanza, Kwema Morden ya Shinyanga, Peaceland ya Mwanza, Muguni ya Mwanza na Rocken Hill ya Shinyanga.

Kimkoa , Mkoa wa Dar es salaam umeshika namba moja, ukifuatiwa na Arusha, Iringa, Kagera, Katavi, Kilimanjaro, Mbeya, Simiyu, Njombe na Pwani.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.