• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Siku 365 za Rais Samia zawa lulu wilayani Iramba wanufaika na miradi ya zaidi ya Tsh 12 bilioni.

Posted on: March 17th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Singida, Yohana Msita amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Mhandisi Michael Matomora kwa namna anavyoshirikiana na Wakuu wa Idara na Vitengo kutekeleza miradi ya zaidi ya Tsh 12 bilioni wilayani Iramba mkoa wa Singida.

Msita ametoa pongezi hizo leo Alhamisi Machi 17, 2022 wakati akiwa na Kamati ya Siasa ya mkoa wa Singida kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) robo ya tatu Januari hadi Machi 2022 wilayani hapa.

Akiongea na wananchi waliohuduria katika miradi mbalimbali, Msita alisema kuwa wanakila sababu ya kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kuleta zaidi ya Tsh 12 bilioni zinazotekeleza miradi ya afya, elimu, barabara na maji wilayani Iramba.

Katika hatua nyingine amewaasa wakuu wa Idara na Vitengo kushirikiana na kutoa huduma bora kwa wananchi kwa sababu kila mmoja katika eneo lake analijenga Taifa.

Aidha, alitahadharisha tabia ya kucheza na mifumo ili kuchea fedha za umma.

“Ndugu zangu niwaambie kuwa tabia ya uaminifu, uadilifu na uchapa kazi wako ndio utakaokutoa hapa ulipo na kukupeleka sehemu nyingine maana haitaji sana muunganiko wako ispokua kazi yako ndio itakayokutambulisha” Alisisitiza Msita

Akiongelea ubora wa miradi iliyotekelezwa kwa kiwango stahiki kulingana na fedha iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, mjumbe wa kamati ya Siasa mkoa wa Singida Diana Chilolo alisema kuwa miradi hii imeleta ukombozi mkubwa kwa wananchi hasa akina mama wajawazito.

“Hakika sisi tunaondoka tukiamini kuwa miradi hii ni msaada kwa wananchi kujipatia huduma bora na kuwafanya wananchi kuendelea na shughuli za kiuchumi ili Taifa letu lizidi kuenndelea.” Alisema Diana

 Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Mhandisi Michael Matomora aliishukuru Kamti ya Siasa mkoa kwa kutembelea miradi na kuwakumbusha wao kama viongozi na kioo kwa jamii kuwa waadilifu.

“Ni kuhakikishie ndugu kiongozi kuwa sisi ni wamoja na lengo letu ni kuhakikisha kuwa tunaendelea kuwa waadilifu kwa kiwango tutakakacho kiweza.” Alisema Matomora

Aidha, alitumia nafasi hiyo kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza mwaka mmoja akiwa ni Rais maana wengi walidhania kuwa hatoweza lakini Rais amefanya makubwa ambayo hayajawahi fanyika tangu kupatikana kwa uhuru, hivyo mambo hayo yanaandika historia mya katika Taifa letu.

“Kwa kweli tunashukuru Mungu amemshika na kumpingania Rasi wetu hatimaye Taifa letu linazidi kuendelea katika nyanja zote za kiuchumi, kijamii na kisiasa.” Aliongeza

Naye Ali Rashidi mkazi wa Kijiji cha Msansao Tarafa ya Shelui Wilayani hapa alisema kuwa miradi hii imekuwa ni lulu na tunu kubwa kwa wananchi wa wilaya ya Iramba, hivyo aliupongeza utawala wa Rais Samia kwa namna unavyowajali wananchi.

Kamati ya Siasa mkoa wa Singida imetembelea mradi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari kata ya Maluga inayojengwa kwa Tsh 470 milioni, mradi wa maji kijiji cha Zinziligi uliotekelezwa kwa Tsh 311.8 milioni, ujenzi wa kituo cha Afya kata ya Mtoa kinachojengwa kwa Tsh 400 milioni na matengenezo ya barabara ya Shelui Nkyala kwa Tsh 450 milioni.

MWISHO

Kamati ya Siasa Mkoa wa Singida leo Machi 17, 2022 imefanya ziara kukagua ujenzi wa shule mpya ya Sekondari katika kata ya Maluga wilayani iramba mkoa wa Singida. Shule inajengwa kwa gharama ya Tsh 470 milioni. Picha na Hemedi Munga

Kamati ya Siasa Mkoa wa Singida leo Machi 17, 2022 imefanya ziara kukagua mradi wa maji kijiji cha Zinziligi wilayani iramba mkoa wa Singida. Mradi unatekelezwa kwa gharama ya Tsh 311.8 milioni. Picha na Hemedi Munga

Kamati ya Siasa Mkoa wa Singida leo Machi 17, 2022 imefanya ziara kukagua mradi ujenzi wa kituo cha Afya kata ya Mtoa wilayani iramba mkoa wa Singida. Mradi unatekelezwa kwa gharama ya Tsh 400 milioni. Picha na Hemedi Munga

Kamati ya Siasa Mkoa wa Singida leo Machi 17, 2022 imefanya ziara kukagua mradi matengenezo ya barabara ya Shelui Nkyala wilayani iramba mkoa wa Singida. Mradi unatekelezwa kwa gharama ya Tsh 450 milioni. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.