• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

TAKUKURU IRAMBA YATOA SEMINA KWA MAAFISA USAFIRISHAJI KUZUIA RUSHWA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

Posted on: October 9th, 2025


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Wilaya ya Iramba Mkoani Singida imetoa semina kwa Maafisa Usafirishaji (Madereva Bajaji na Bodaboda) Juu ya kuzuia Vitendo vya Rushwa kuelekea Uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani mwaka huu 2025.


Semina hiyo ilifanyika katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba tarehe 09 Oktoba, 2025.


Akizugumza wakati wa ufunguzi, Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleiman Mwenda amewataka Maafisa hao kuhakikisha wanazuia vitendo vya rushwa akisisitiza kuwa kuwepo kwa vitendo hivyo katika Jamii Kunasababisha Kuchelewa kwa Maendeleo.


"Tuungane kwa pamoja kuhakikisha kwamba tunaipiga vita rushwa ili tuweze kupata maendeleo kwa haraka. Tukiendekeza rushwa hatutapata maendeleo kwa haraka... Lazima wakati wote tujitahidi kuikataa na kuhakikisha hatujiingizi katika vitendo ambavyo vitatufanya tuweze kutoa ama kupokea rushwa katika maeneo yetu ya utendaji kazi." Alisema DC MWENDA


Kwa upande wake Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Iramba Ahmad Sungura alisema baada ya elimu kutolewa kwa maafisa hao, ni matarajio ya TAKUKURU kuwa, wataweza kufichua vitendo vya rushwa vinayotendeka katika mazingira ya kazi zao na hata kipindi hiki cha uchaguzi, kufichua waalifu wengine ikiwa ni pamoja na wahamiaji haramu na wataweza kushiriki uchaguzi mkuu 2025 kwa uhuru na amani bila kushawishiwa au kurubuniwa kwa rushwa.


Semina hiyo ya siku moja ilitolewa kwa maafisa usafirishaji 125 kati ya 181 walioalikwa ikiwawezesha maafisa usafirishaji kupata elimu kutoka TAKUKURU, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Polisi, Uhamiaji, Zimamoto na Idara ya Maendeleo ya Jamii, lengo likiwa kuwafikishia elimu ya mapambano dhidi ya rushwa chini ya kauli mbiu isemayo "Kuzuia rushwa ni jukumu lako na langu; tutimize wajibu wetu".

Tangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA NA KUITWA KWENYE MAFUNZO (WASIMAMIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA) October 23, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • WAKAZI WA KIOMBOI WAENZI UTAMADUNI KUPITIA MICHEZO YA JADI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 19, 2025
  • DAS MWAKIBETE ASHIRIKI BONANZA LA MICHEZO YA JADI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 25, 2025
  • IRAMBA YANUFAIKA NA HUDUMA YA MADAKTARI BINGWA WA RAIS DKT. SAMIA

    October 14, 2025
  • KUMBUKUMBU YA MIAKA 26 YA KIFO CHA MWALIMU J. K. NYERERE

    October 14, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.