• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

TAKUKURU Wilayani Iramba yaokoa 13.6milioni za Wakulima wa Pamba kijiji cha Kikunku zilizokua zimepotezwa na Viongozi 7 wa Jikomboe AMCOS msimu wa 2018/2019.

Posted on: June 11th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula ameipongeza TAKUKURU kwa kuokoa takriban Tsh 13.6milioni za Wakulima wa pamba ambao ni Wanachama wa Chama cha Msingi cha Ushirika Jikomboe AMCOS ambazo zilikua zimepotezwa na viongozi 7 wa AMCOS hiyo msimu wa 2018/2019.

Luhahula ametoa pongezi hizo leo Juni 10, 2020 wakati alipokua akikabidhiwa pesa hizo na Mkuu wa Taasisi ya kupambana na kuziwia rushwa (TAKUKURU) Wilayani Iramba, Ahmad Sungura katika kijiji cha Kikunku Tarafa ya Shelui Wilayani humo.

Akiongea na Wanachama wa AMCOS hiyo waliokua wakidai pesa hizo, Mkuu huyo wa Wilaya amevipongeza Vyombo vya Usalama vya Wilaya hiyo.

“Ninavipongeza sana Vyombo vya Usalama katika Wilaya yetu kwa kuwa wameshirikiana nakufanikisha kuokoa pesa hizi,” amesema Luhahula na kuongeza

“Kampuni ya ununuzi ilitoa pesa zote za Wakulima kwa Viongozi wa AMCOS, lakini Viongozi wa Jikomboe AMCOS wakala hizo pesa, hivyo kusababisha Wakulima kukosa pesa zao.”

Baada ya kubaini kuwa Wakulima wa kijiji hicho hawakupata pesa zao kwa sababu ya Viongozi wao wasiokua waadilifu tulilikabidhi kwa TAKUKURU.

“Ninampongeza tena Mkuu wa TAKUKURU Iramba kwa kulifanikisha hili, na leo tumekuja kifua mbele kuwalipa pesa zenu zote baada ya kuwabana Viongozi wa AMCOS waliokula na kuzirudisha,” amesema

Halikadhalika, Luhahula amewaasa Wakulima hao kuhakikisha wanazitumia pesa hizo vizuri bila ya kuwasahau wakinamama ambao walioonesha uvumilivu na waume zao halafu mkaenda tafuta Wanawake wengine.

“Tafadhalini msiseme leo tumepata pesa zetu tunakwenda kuzipiga faini na kuoa mke mwingine, hao Wanawake mlioteseka nao kusubiria wakapate faida hiyo,” ametilia mkazo Mkuu wa Wilaya

Katika hatua nyingine, Luhahula amemuagiza Afisa Ushurika wa Wilaya hiyo, Heriman Kimario kuwachukulia hatua Viongozi wa AMCOS wilaya nzima wasiokua waadilifu na waaminifu huku akiwataka watendaji wa vijiji vyote kuwafichua Viongozi hao wasiokua waadilifu ili kuuwekea hashima Ushirika.

Akifafanua namna ya walivyoweza fanikisha malipo ya pesa hizo, Kamanda wa TAKUKURU wa Wilaya hiyo, Amhad Sungura amesama baada ya kupokea taarifa ya upotevu wa Tsh 13.6milioni za mauzo ya pamba ya Chama cha Ushirika Jikomboe AMCOS chenye namba ya usajili SIR/0737B toka kwa Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya hiyo Mei 4, mwaka huu, uchunguzi ulifanyika nakubaini kuwa viongizi 7 wa AMCOS wamezipoteza pesa hizo.

Sungura amesema msimu wa 2018/2019 Jikomboe AMCOS ilikusanya pamba kutoka kwa wanachama wake kilo 106,820 zenye thamani ya Tsh 128.18milioni ambapo zilinunuliwa na kampuni ya Biosustain (T) LTD na kulipa pesa zote kwa Jikomboe AMCOS.

TAKUKURU ilibaini kuwa kunawakulima ambao ni wanachama wa Jikomboe AMCOS 64 waliouza pamba yao kilo 11,318 zenye thamani ya Tsh 13.6milioni hawakulipwa pesa zao.

Kufuatia uchunguzi huo, TAKUKURU imeweza kuokoa Tsh 13.6milioni na kuzikabidhi kwa Mkuu wa Wilaya hiyo kwa lengo la kuwagawia wakulima hao.

Kwa upande wake mmoja wa waathirika wa upotevu wa fedha hiyo, Amani Bernad amesema kuwa Viongozi wa AMCOS waliohusika na upotevu huo wa pesa wanapaswa kutumbuliwa kwa sababu wamewasababishia Wakulima hao hali ngumu ya maisha na kujikuta wanashindwa kulima vizuri kilimo cha mpunga kutokana na hali ya mvua ya mwaka huu.

“Hawa Viongozi hawafai na wangetakiwa kutumbuliwa kwa kuwa wametuhujumu, kutukandamiza na kuturudisha nyuma ili kuchagua wengine watakaoleta maendeleo katika kijiji chetu,” amesema Bernad

Pia, ameishukuru Serikali kwa kuanzisha mfumo mpya katika msimu wa mwaka huu ambao unamtaka mkulima kufungua akaunti benki ambapo ataweza kapata pesa yake ndani ya masaa 48 punde baada ya kuuza mazao yake.

Naye Fatuma Elia muhanga wa upotevu wa pesa hiyo, ameipongeza Serikali kwa kurahisisha mfumo wakulipa pesa za wakulima baada ya kuuza mazao kupitia akaunti za benki au namba za simu, hivyo kumfanya mkulima kulipwa hata kwa njia ya simu.

MWISHO

Kamanda Mkuu wa TAKUKURU Wilayani Iramba, Ahmad Sungura akimkabidhi Mkuu wa Wilaya hiyo, Emmanuel Luhahula Tsh 13.6milioni zilizokua zimepotezwa  na Viongozi 7 wa Jikomboe AMCOS baada ya kuwa wameuza pamba kwa kampuni ya Biosustain(T) LTD na kulipwa fedha zote. Picha na Hemedi Munga

Fedha za Wakulima wa Pamba kijiji cha Kikunku Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba zilizokua zimepotezwa  na Viongozi 7 wa Jikomboe AMCOS baada ya kuwa wameuza pamba kwa kampuni ya Biosustain(T) LTD na kulipwa fedha zote. Picha na Hemedi Munga

Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Herman Kimario akigawa pesa za Wakulima wa Pamba kijiji cha Kikunku Tarafa ya Shelui Wilayani Iramba zilizokua zimepotezwa na Viongozi 7 wa Jikomboe AMCOS baada ya kuwa wameuza pamba kwa kampuni ya Biosustain(T) LTD na kulipwa fedha zote. Picha na Hemedi Munga


Baadhi ya Wakulima wa Pamba kijiji cha Kikunku wakisubiri kugawiwa pesa walizokua wameuza pamba msimu wa 2018/2019.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.