• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Timu ya mpira wa wavu ya Watumishi wa Wilaya ya Iramba imeifunga timu ya wavu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama seti mbili bila.

Posted on: March 7th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Timu ya mpira wa wavu ya Watumishi wa Wilaya ya Iramba imeifunga Timu ya wavu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama seti mbili bila.

Mchezo huo umefanyika leo Jumamosi machi 7, 2020 katika uwanja wa Mabatini uliopo  mjini Kiomboi.

Dakika chache baada ya kuanza kwa mchezo huo timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba walioenekana kulisakama lango la wapinzani wao huku Fabiano Nyamuhaga akionekana kuwa mwiba mpachikaji wa mabao zidi ya timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Mkalama.

Baada ya mchezo wa wavu kuisha Watumishi hao waliuanza mchezo wa mpira wa mguu katika kiwanja cha Mabatini kilichopo mjini hapo.

Mchezo huo wa mpira wa mguu ulianza kwa timu zote mbili kushambuliana kwa kasi ambapo dakika ya 11 Ashadi Abdallah anaipatia goli la kuongoza timu ya Watumishi wa Mkalama.

Mchezo ulizidi kuwa na kasi ya kushambuliana kwa zamu jambo ambalo lilipelekea timu ya Watumishi ya Mkalama kupata penati dakika ya  35 ya mchezo huo.

Hata hivyo Afisa Utamaduni wa timu ya Halmashauri ya Mkalama, Luzegele Kilala anaukosa mkwaju wa penati nakufanya matokeo kuwa Mkalama goli moja na halmashauri ya Wilaya ya Iramba bila.

Hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinakamilika ni timu ya Watumishi wa Halamashauri ya Wilaya ya Mkalama wanaotoka wakiwa wanaongoza goli moja bila zidi ya timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakilisakama lango la timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Mkalama.

Ilikuwa dakika ya 58 ambayo Jemsi Tambue anaisawazishia timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba baadaya kupokea krosi safi iliyotoka kwa kapteni wa timu hiyo.

Mchezo huo uliongeza kasi kwa timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kulisakama lango la timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.

Dakika ya 78  Godfrey Sanga  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama anapiga shuti kali lililomshinda mlinda lango wa timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba na kugonga mwamba kutoka nje.

Timu hizo zilitoshana jasho kwa mchezo mzuri hadi dakika 90 zinakamilika zikiwa zimefungana goli moja na kufanya matokeo hayo kuwa sare ya moja moja.

Kampteni wa timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Mahmudu Said amesema matokeo hayo yametokana na timu kutokuwa pamoja na hivyo kupanga kikosi kwa kutumia uzowefu na kufanya kipindi cha kwanza kushambuliwa mara kwa mara na  kipindi cha pili baada ya kujua kila aliyekuwa vizuri ndio maana tuliukamata mchezo.

Wanajipanga kwa kuwakusanya wachezaji ili wafanye mazoezi ya pamoja ili watakaporudiana waifunge timu ya Watumishi wa Mkalama

“ Tumeanza  mazoezi ya pamoja yatakayodumu kwa   muda wa wiki mbili au tatu ili tutakaporudiana na timu ya Watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Mkalama tupate ushindi,” amesema Said

Naye kapteni wa timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Luzegele Kilala amesema wanakwenda kujidhatiti ili wawe  na timu imara zidi ya timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.

“Tufanye mazoezi ili tupate stamina ambayo ni sehemu ya afya zetu napengine tukiunganisha na Watumishi wa wilaya zingine tunaweza kupata timu bora ya Watumishi Mkoa wa Singida,” amesema Kilala

 

Baada ya mchezo huo kukamilika Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba amesema kuwa wamedhihirisha umoja wao kwa kucheza michezo hiyo na kufanya kuwa Iramba na Mkalama kuwa ni moja huku akiahidi kuwa watakwenda  Mkalama kwa ajili ya mchezo wa marudiano.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama  Godfrey Sanga  ameushukuru uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kwa ukarimu waliowapatia.

MWISHO

Jemsi Tambue akiwa hewani kuwania mpira wa wavu katika mchezo uliowakutanisha timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama. Picha na Hemedi Munga

Kikosi cha timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakipanga kikiosi kitakacho anza zidi ya timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Kikosi cha timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kikiwa tayari kwa mtanange zidi ya timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Vikosi vyote viwili vikiwa tayari kwa mtanange wa ujirani mwema kati ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, B’hango Lyangwa akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama,  Godfrey Sanga  akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni. Picha Hemedi Munga

Vikosi vyote viwili vikisikiliza nasaha baada ya dakika 90 kukamilika katika uwanja wa mabatini mjini kiomboi. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.