• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Tuhuma za manunuzi hewa zadaiwa kufanyika wilayani Iramba kutokana na fedha za Mfuko wa Jimbo za mwaka 2019/2020

Posted on: February 27th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya  Iramba, Linno Mwageni kumsimamisha kazi mara moja Afisa Ugavi na Manunuzi, Ibrahimu Nkumbi kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za Mfuko wa Jimbo la Iramba Magharibi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake leo  Alhamisi Februari 27, 2020 Mkuu wa Wilaya hiyo Emmanuel Luhahula amesema kuwa Ibrahimu Nkumbi ambaye ni Afisa Ugavi na Manunuzi wa Halmashauri hiyo ametumia utaalamu wake vibaya kumdanganya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Linno Mwageni kwa kutoa nyaraka ambazo zinaonesha kuwa vifaa vya ujenzi vimekwisha pokelewa na Halmashauri hiyo wakati mpaka leo hakuna vifaa vyovyote vilivyonunuliwa na kupokelewa.

“ Kuanzia sasa ninakuagiza Mkurugenzi Mtendaji kumsimamisha kazi Afisa huyo, huku akiiagiza Ofisi ya kuzuwia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) kuchunguza tuhuma za ubadhilifu wa fedha hizo,” ameagiza Luhahula 

Mkuu huyo wa Wilaya amesema katika tuhuma hiyo  jumla ya shilingi milioni 34,984,500 ilisemekana kuwa zilitumika kununua saruji mifuko 600 na  bati 877.

Luhahula alipata  tetesi za ubadhirifu wa fedha hizo ambapo ilimlazimu  kuunda Timu ya Watu Watano  ili kuchunguza ubadhirifu huo na kubainika kuwa fedha hizo zimelipwa kwa mzabuni Kiteka General Supply ambayo inamilikiwa na Wifredi Kizanga  Diwani wa Kata ya Tulya.

“ Kikao cha kamati ya  Mfuko wa Jimbo  kilicho keti Desemba 19 mwaka jana  kiliazimia kuwa vifaa vilivyoagizwa visigawiwe popote  hadi pale kamati itakapotembelea maeneo yenye uhitaji. Hata hivyo Januari 20 mwaka huu Halmashauri ilifanya malipo ya shilingi 34, 196,610 kupitia hati ya malipo ya Januari 07, 2020 kwa mzabuni Kiteka General Supply kinyume na sheria ya manunuzi namba 7 ya mwaka 2016, na sheria hii inakataza taasisi kufanya biashara na mtumishi  au kiongozi wake kwa kukwepa mgongano wa kimaslahi,”

“ Uchunguzi unathibitisha kuwa Afisa Manunuzi na Ugavi Ibrahimu Nkumbi ametumia utaalamu wake vibaya kwa kumpotosha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya kwa kutofuata sheria za manunuzi wakati wa mchakato wa manunuzi ya vifaa vya mfuko wa Jimbo. Aidha kwa kutumia utaalamu wake alimdanganya Mkurugenzi Mtendaji kuwa vifaa vilivyonunuliwa vimeishafika Halmashauri, kwa taarifa hiyo ilimlazimu Mkurugenzi Mtendaji kuunda kamati ya Watu Watatu ili wakakague vifaa hivyo vilivyonunuliwa, hata hivyo kamati hiyo haikukagua stoo ya Halmashauri na badala yake ilikagua stoo ya mzabuni Wilfred Kizanga na kuandika taarifa kuwa vifaa vimenunuliwa kama ilivyoagizwa,” amebainisha  Luhahula

 

Aidha timu  hiyo  ya Watu Watano ilioteuliwa na Mkuu huyo wa Wilaya ilabaini kuwa sheria ya manunuzi ya umma, kanuni za kudumu za utumishi wa umma, na muwongozo  wa mfuko wa jimbo zimekiukwa kwa maksudi kwa lengo la kufanyia biashara fedha za serikali zilizo tolewa kwa ajili ya maendeleo ya Jimbo.

Katika uchunguzi huo timu hiyo imetoa mapendekezo kuwa watuhumiwa waliohusika na ubadhilifu huo wachukuliwe hatua za kinidhamu na Muajiri wao.

 

Hata hivyo Mkuu huyo wa Wilaya ameagiza vyombo vinavyohusika kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini kama kuna jinai iliyoisababishia serikali hasara ya fedha baada ya serikali kulipwa kwa mfanya biashara ambaye hajakabidhi vifaa hadi sasa licha ya wataalamu wa Idara ya Manunuzi na Mipango kuonesha kuwa vifaa hivyo vimekwisha pokelewa na Halmashauri hiyo.

Pia ameiagiza Idara ya Elimu kuhakikisha inalipa madai ya Walimu ifikapo februari 28, 2020.

“ Ninaiagiza Idara ya Elimu mpaka kufikia kesho iwe imelipa madai ya Walimu na  wasipowalipa nitawashughulikia,” amesisitiza Luhahula

Hata hivyo ametoa maelekezo kuwa vituo vya Afya Ndago na Kinampanda vianze kufanya kazi mara moja.

Akihitimisha maongezi yake na Waandishi wa Habari, Luhahula amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutimiza ahadi aliowaahidi wananchi wa shelui Desemba 2019 kuwapa 250 milioni kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Shelui.

 Mkuu wa wilaya amethibitisha kuwa Rais Dkt, John Pombe Magufuli amekwisha leta 400 milioni tangu Januari mwaka huu, huku akimshauri Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuharakisha ujenmzi wa kituo hicho kwa kutumia Suma JKT au Magereza.

Mwisho

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA IRAMBA MAGHARIBI AWATAKA WAENDESHA VIFAA VYA BVR NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI (PHC) IRAMBA YAJADILI MIKAKATI YA CHANJO YA POLIO SINDANO YA PILI

    May 09, 2025
  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.