• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

UANZISHWAJI WA MADAWATI YA ULINZI NA USALAMA WA MTOTO NDANI NA NJE YA SHULE NI MUHIMU KATIKA KUMLINDA MTOTO- Dkt. BAGANDA.

Posted on: April 1st, 2023

UANZISHWAJI WA MADAWATI YA ULINZI NA USALAMA WA MTOTO NDANI NA NJE YA SHULE NI MUHIMU KATIKA KUMLINDA MTOTO- Dkt. BAGANDA.

Afisa Elimu Mkoa wa Singida Dkt. Elipidius Baganda  amesema Serikali inaendelea kuhakikisha Ulinzi na usalama wa Mtoto unazingatiwa ili kutokomeza ukatili wa aina zote kwa Watoto waliopo ndani na Nje ya Shule.


Dkt. Baganda  ameyasema hayo  wakati akizungumza na Walimu Wakuu na  Maafisa Elimu Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Wakati wa Ufunguzi wa Mafunzo ya Ulinzi na Usalama wa mtoto yanayotolewa na Programu ya Mradi wa Shule Bora kwa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mkoani Singida ,Tarehe 31/03/2023 .


“Uanzishwaji wa Dawati hili Shuleni  utasaidia kukabiliana na Ukatili unaojitokeza ndani na nje ya shule kwa wanafunzi  na hata kwa watoto waliopo nyumbani na mitaani kwenu na nataka mfahamu kwamba kuna ukatili wa aina tatu kwa watoto ambao wa kwanza ni ukatili wa Kudhuru mwili, Wa pili ni ukatili wa Kingono na Wa tatu ukiwa ni ukatili wa Kihisia”.alisema Dkt. Bagenda.


Dkt Baganda  aliendelea kwa kusema kwamba, Serikali inazidi kupambana na wimbi la ukatili linalo sababisha watoto wengi kukatisha ndoto zao, hivyo kuwasihi wanafunzi hao kuhakikisha wanapinga vikali ukatili wakianza na kutokufanyiana ukatili wao kwa wao.


“Kumekua na wimbi kubwa la Ushoga na usagaji ambalo chanzo chake kimebainika kuwa ni ukatili wa kingono wanaofanyiwa Watoto na kusababisha kuwapotezea dira kwenye Maisha yao”alifafanua Dkt. Baganda


Naye Mratibu wa Programu ya Mradi wa Shule Bora Mkoa wa Singida Ndugu Samwel Daniel ,Alimweleza Mgeni rasmi kuwa Programu hiyo inatekeleza  maeneo manne ambayo ni ufundishaji,Ujifunzaji,Ujumuishi (Shule salama,watoto wenye ulemavu  na Elimu kwa Msichana)na Uimarishaji wa mifumo. Mtoto kuwa salama shuleni inarahisisha Ujifunzaji wake.Pia Programu hii ya Shule Bora inatekelezwa kwenye Mikoa inayofanya vibaya Kitaaluma na moja ya sababu ni Usalama wa mtoto.


Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Singida bwana Edward Masero amewaambia washiriki wa mafunzo hayo Kuhakikisha wanatumia Miongozo iliyotolewa kwa ajili ya Kuhakikisha Ulinzi na Usalama wa mtoto unawashirikisha Walezi,Wazazi na walimu wa Malezi  waliopo shuleni.


 “Mtu mwenye Uadilifu ni mtu ambaye anaweza kutunza siri utakapomwambia shida yako, Mtu anaefanya vizuri katika masomo yake ambae anaweza kubeba jukumu la ziada,Hivyo mnatakiwa kuhakikisha mnawasaidia watoto kuzitatua changamoto zao pindi wanapokuletea shuleni ”Alisema Masero.


Madawati ya ulinzi na usalama wa watoto 1,363 na Mabaraza ya watoto 562 katika mikoa 8 yameanziahwa tangu kampeni hii kuzinduliwa mwezi Juni, 2023.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.