• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Ushirika wa wachimbaji madini wa kisonga shelui (UWAWAKISHE) kata ya Mgongo wilayani Iramba wachangia madawati 60 katika shule ya sekondari Mgongo kuunga mkono jitihada za serikali.

Posted on: February 18th, 2019

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida Mhe: Emmanuel Luhahula amekabidhiwa madawati 60 kutoka kwa Ushirika wa wachimbaji madini wa kisonga shelui (UWAWAKISHE) kata ya Mgongo Wilaya ya Iramba kwa ajili ya shule ya sekondari Mgongo ili kuunga mkono jitihada za serikali.

 Makundi mengine yaliochangia madawati ni Kijiji cha Mgongo Madawati 16, Kijiji cha Mseko Madawati 16, Mhe: Diwani wa kata ya Mgongo Madawati 10, Ndg. Athuman Swalehe Madawati 10, Ndg. Waziri Hussein Madawati 10.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa ukamilishaji wa miundo mbinu katika shule ya sekondari ya mgongo. Ndg David Stephan alisema shule ya sekondari mgongo ilikuwa na upungufu wa madawati 63 na viti 92 hadi sasa hivi, kata imefanikiwa kutengeneza madawati 122 na viti 138 vyenye thamani ya Shilingi 7,800,000 ambao nimichango ya wananchi na Wadau mbalimbali.

Ndg. David Stephan aliongeza kusema, Wadau wengine wamechangia saruji mifuko 53 yenye thamani ya Shilingi 912,000 kwa ajili ya ujenzi wa Hosteli ya wasichana katika shule ya sekondari ya Mgongo.

WACHANGIAJI WA SARUJI
IDADI YA MIFUKO
THAMANI
KANISA LA E.A.G.T MGONGO
5
85,000
KANISA LA K.K.K.T MGONGO
5
85,000
KANISA LA ANGLIKANA
1
17,000
MGODI WA MBUYUNI
17
300,000
UWAWAKISHE
20
340,000
KANISA LA F.P.C.T MGONGO
5
85,000
TOTAL
53
912,000

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi madawati hayo, Mkuu wa wilaya ya Iramba Mhe: Emmanuel Luhahula ameshukuru sana Ushirika wa wachimbaji madini wa kisonga shelui (UWAWAKISHE) na Wadau wa maendeleo wa kata ya Mgongo kwa ushirikiano mkubwa wa kutoa michango mbalimbali. “Tunawashukuru kwa kuwa mpo karibu nasi, tunawapenda sana kwa kuwa tunapowahitaji mnakaribia na mkishirikishwa katika maendeleo mbalimbali, ninawahakikishia madawati haya muliyoyatoa yatatumika vizuri na ufaulu wa watoto wetu utaongezeka zaidi.” Alisema Mhe: Luhahula

Mhe. Luhahula ametoa shukrani za dhati kwa wafadhili kwa uzalendo wao wa kutoa msaada kwa kuchangia mifuko ya saruji 53 yenye thamani za Kitanzania Shilingi 912,000 kwa ajili ya ujenzi wa Hosteli ya wasichana katika shule ya sekondari ya Mgongo.  Vile vile ameshukuru sana Ushirika wa wachimbaji madini wa kisonga shelui (UWAWAKISHE) kuhaidi mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa hostel ya wasichana katika shule ya sekondari mgongo ambayo itakabidhiwa Tarehe 28.02.2019.

Mhe: Luhahula ametoa wito kwa wananchi na wazawa wa Iramba waliopo ndani na nje ya Iramba kuiga mfano wa Ushirika wa wachimbaji madini wa kisonga shelui (UWAWAKISHE) na Wadau wa maendeleo wa kata ya Mgongo”. Malengo ya wilaya yetu ni kuhakikisha wanafunzi wote wanasoma kwenye mazingira mazuri, ushirikiano wenu unahitajika sana kati ya serikali na Wadau wa maendeleo ili kuunga mkono jitihada za serikali” alisema Mhe: Luhahula.


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA November 03, 2023
  • KUITWA KAZINI November 29, 2023
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wamefanya ziara ya Ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa Wilayani Iramba

    October 24, 2023
  • RAIS DKT. SAMIA AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI SINGIDA KWA KISHINDO, WANANCHI WAMSHUKURU KWA MIRADI YA MAENDELEO

    October 17, 2023
  • MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amepokea rasmi Mbio za Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoani Tabora na aliyekabidhi ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Batlida Briani.

    September 22, 2023
  • MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Abdalla Shaibu Kaim amewataka Watanzania kuhakikisha wanakemea vitendo vya rushwa kwa maelezo kuwa rushwa inakwamisha maendeleo ya Mkoa pamoja na Taifa kwa ujumla

    September 22, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.