• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Ushirika wa wachimbaji madini wa kisonga shelui (UWAWAKISHE) kata ya Mgongo wilayani Iramba wachangia madawati 60 katika shule ya sekondari Mgongo kuunga mkono jitihada za serikali.

Posted on: February 18th, 2019

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida Mhe: Emmanuel Luhahula amekabidhiwa madawati 60 kutoka kwa Ushirika wa wachimbaji madini wa kisonga shelui (UWAWAKISHE) kata ya Mgongo Wilaya ya Iramba kwa ajili ya shule ya sekondari Mgongo ili kuunga mkono jitihada za serikali.

 Makundi mengine yaliochangia madawati ni Kijiji cha Mgongo Madawati 16, Kijiji cha Mseko Madawati 16, Mhe: Diwani wa kata ya Mgongo Madawati 10, Ndg. Athuman Swalehe Madawati 10, Ndg. Waziri Hussein Madawati 10.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa ukamilishaji wa miundo mbinu katika shule ya sekondari ya mgongo. Ndg David Stephan alisema shule ya sekondari mgongo ilikuwa na upungufu wa madawati 63 na viti 92 hadi sasa hivi, kata imefanikiwa kutengeneza madawati 122 na viti 138 vyenye thamani ya Shilingi 7,800,000 ambao nimichango ya wananchi na Wadau mbalimbali.

Ndg. David Stephan aliongeza kusema, Wadau wengine wamechangia saruji mifuko 53 yenye thamani ya Shilingi 912,000 kwa ajili ya ujenzi wa Hosteli ya wasichana katika shule ya sekondari ya Mgongo.

WACHANGIAJI WA SARUJI
IDADI YA MIFUKO
THAMANI
KANISA LA E.A.G.T MGONGO
5
85,000
KANISA LA K.K.K.T MGONGO
5
85,000
KANISA LA ANGLIKANA
1
17,000
MGODI WA MBUYUNI
17
300,000
UWAWAKISHE
20
340,000
KANISA LA F.P.C.T MGONGO
5
85,000
TOTAL
53
912,000

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi madawati hayo, Mkuu wa wilaya ya Iramba Mhe: Emmanuel Luhahula ameshukuru sana Ushirika wa wachimbaji madini wa kisonga shelui (UWAWAKISHE) na Wadau wa maendeleo wa kata ya Mgongo kwa ushirikiano mkubwa wa kutoa michango mbalimbali. “Tunawashukuru kwa kuwa mpo karibu nasi, tunawapenda sana kwa kuwa tunapowahitaji mnakaribia na mkishirikishwa katika maendeleo mbalimbali, ninawahakikishia madawati haya muliyoyatoa yatatumika vizuri na ufaulu wa watoto wetu utaongezeka zaidi.” Alisema Mhe: Luhahula

Mhe. Luhahula ametoa shukrani za dhati kwa wafadhili kwa uzalendo wao wa kutoa msaada kwa kuchangia mifuko ya saruji 53 yenye thamani za Kitanzania Shilingi 912,000 kwa ajili ya ujenzi wa Hosteli ya wasichana katika shule ya sekondari ya Mgongo.  Vile vile ameshukuru sana Ushirika wa wachimbaji madini wa kisonga shelui (UWAWAKISHE) kuhaidi mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa hostel ya wasichana katika shule ya sekondari mgongo ambayo itakabidhiwa Tarehe 28.02.2019.

Mhe: Luhahula ametoa wito kwa wananchi na wazawa wa Iramba waliopo ndani na nje ya Iramba kuiga mfano wa Ushirika wa wachimbaji madini wa kisonga shelui (UWAWAKISHE) na Wadau wa maendeleo wa kata ya Mgongo”. Malengo ya wilaya yetu ni kuhakikisha wanafunzi wote wanasoma kwenye mazingira mazuri, ushirikiano wenu unahitajika sana kati ya serikali na Wadau wa maendeleo ili kuunga mkono jitihada za serikali” alisema Mhe: Luhahula.


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA IRAMBA MAGHARIBI AWATAKA WAENDESHA VIFAA VYA BVR NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI (PHC) IRAMBA YAJADILI MIKAKATI YA CHANJO YA POLIO SINDANO YA PILI

    May 09, 2025
  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.