• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Utoaji wa kinga tiba ya minyoo tumbo kuwanufaisha walengwa 66,186 wenye umri wa miaka 5 hadi 15 Wilayani Iramba.

Posted on: March 6th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewaomba Watumishi wa Mungu na Watumishi wa umma kuifanyia kazi elimu walioipata katika kikao cha mpango mkakati wa magonjwa yaliokuwa hayapewi kipaumbele katika ukumbi wa Mkuu wa Wilaya ya Iramba.

Luhahula ametoa ombi hilo leo Ijumaa Machi 6, 2020 wakati akifungua kikao hicho kwa ajili ya mafunzo mafupi ya ugonjwa wa minyoo na madhara yake kwa jamii katika Ukumbi wa Mkuu wa Wilaya mjini kiomboi.

Mkuu huyo wa Wilaya amewaomba Watumishi wa Mungu kuendelea kuiombea Iramba na Taifa zidi ya Ugonjwa ambao unaendelea kutawala.

“ Niwaombe Watumishi wa Mungu kuendelea kutuombea sisi na Taifa kwa sababu ya ugonjwa ambao unaendelea kutawala,” ameomba Luhahula

Akisoma taarifa fupi  ya utekelezaji wa unyweshaji wa dawa ya minyoo tumbo na kichocho inayotekelezwa na Mpango  wa Taifa wa magonjwa yaliokuwa hayapewi kipaumbele, Grace Kiunsi amesema wamepanga kufikia asilimia 100% ya walengwa walioko shuleni.

Amesema kitengo cha magonjwa yaliokuwa hayapewi kipaumbele chini ya CHMT ya Halmashauri hiyo itaendelea kutekeleza zoezi la utoaji wa kinga tiba kwa watoto wenye umri wa kwenda shule kwa kuzingatia maelekezo ya Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia  Wazee na Watoto.

Zoezi la utoaji wa kinga tiba litafanyika mach 16 hadi 17, 2020 kwa kugawa dawa ya aina moja ya minyoo tumbo kwa walengwa 66,186 wenye umri wa miaka 5 hadi 15.

Idadi hiyo imeongezeka ukilinganisha na mwaka jana ambapo jumla ya walengwa 57,746 walipatiwa kinga tiba ya minyoo ya tumbo na kichocho huku wasichana wakiwa 32,037, wavulana 32,137 na watoto wenye umri wa kwenda shule ambao hawapo shuleni 386.

Naye Mratibu wa magonjwa yaliokuwa hayapewi kipaumbele wa Halmashauri hiyo, Dkt. Msengi Ntanagala amesema kuwa dawa hiyo inatibu minyoo ya mviringo, minyoo ya mjeledi na minyoo ya safura ambayo uambukizwa kwa kula mayai ya minyoo hiyo kutoka kwenye udongo au kupenya kwenye ngozi.

Pia amebainisha baadhi ya madhara yatokanayo na minyoo hiyo kwenye haja kubwa, kwenye ini, kwenye utumbo na kwenye ubongo.

Akijibu swali lililoulizwa na mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Dkt Ntanagala amesema kuwa wanaolengwa ni watoto kwa sababu athari ya maambukizo ni kubwa mno kutokana na tabia zao za kuchezea udongo, mchanga na ulaji wa matunda bila kuyasafisha.

Kwa upande wake mchungaji wa kanisa la Evangelist Assembles of God la mjini hapo, Robert Kijanga amewaomba Wataalamu kufika katika nyumba za ibada ili kutoa elimu hiyo.

“Sisi watu wa dini tunawakaribisha katika nyumba zetu za ibada kuongea na jamii ili kufikisha elimu hii,” ameomba Kijanga

Katika mafunzo hayo, viongozi wa dini mbalimbali walitumia fursa ya kuiombea Wilaya ya Iramba na Taifa kwa ujumla kuepukana na ugonjwa unaoendelea kuenea kwa sasa  duniani pamoja na janga la nzige.  

MWISHO                                                                                                                                                                                                                                                                                                                   

Grace Kiunsi akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa unyweshaji wa dawa ya minyoo tumbo na kichocho mbele ya wajumbe wa kikao cha mpango mkakati wa magonjwa yalikuwa hayapewi kipaumbele. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                                                                                                                                          

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akisikiliza taarifa ya utekelezaji wa unyweshaji wa dawa ya minyoo tumbo na kichocho mbele ya wajumbe wa kikao cha mpango mkakati wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele. Kushoto kwake ni katibu tawala wa wilaya hiyo, Pius Songoma na kulia mwa Mkuu huyo wa Wilaya ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri hiyo, Emmanuel Makwaya. Picha na Hemedi Munga                                                                                                                                                                                                                                                                         

Mchungaji wa kanisa la Evangelist Assembles of God, Robert Kijanga akichangia mada baada ya taarifa ya utekelezaji wa unyweshaji wa dawa ya minyoo tumbo na kichocho mbele ya wajumbe wa kikao cha mpango mkakati wa magonjwa yalikuwa hayapewi kipaumbele. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.