• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Wafanyakazi Singida wampongeza Mhe. Rais magufuli kwa kufuta kikokotoo kimpya

Posted on: January 4th, 2019

BAADA ya Rais Dkt. John Magufuli kurejesha Kikokotoo cha zamani kwa mafao ya WATUMISHI WA UMMA nchini, wafanyakazi kupitia mashirikisho huru ya vyama wameendelea kuunga mkono agizo hilo kwa kufanya maandamano ya amani.

Shirikisho huru la vyama vya wafanyakazi Mkoa wa Singida, leo limefanya maandamano ya amani ya kumpongeza Mhe. Rais Dkt. John Magufuli kwa kuondoa tatizo la KIKOKOTOO ambacho kilisababisha watumishi wengi kukosa amani na utulivu mioyoni mwao.

Maandamano hayo yaliyoanzia ofisi za TUCTA mkoa zilizopo mtaa wa Mughanga na kupitia mtaa wa Boma road kisha kupokelewa katika ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Singida na Dkt. Rehema Nchimbi ambaye ndiye mkuu wa mkoa wa Singida akisindikizwa na viongozi mbalimbali wa Vyama na Serikali.

Katika risala ya watumishi hao iliyosomwa na Katibu wa TUCTA mkoa, Bw. Max Chaba, wafanyakazi hao wamepongeza hatua ya Mheshimiwa Rais Magufuli kurejesha kikokotoo cha zamani, hali waliyoieleza kuwa amesikiliza maombi yao na sasa amefuta machozi yaliyokuwa yakiwatoka kwa muda mrefu sana.

Katibu huyo wa TUCTA amesema kuwa, uamuzi wa Rais Magufuli umepokelewa kwa furaha sana na watumishi wote wa mkoa wa Singida na Tanzania kwa ujumla.

“Uamuzi huu umerejesha hali na morali ya watumishi wa umma nchini katika kufanya kazi kwa nguvu zao zote. Hii inatokana na imani kwamba baada ya kustaafu kuna kitu ambacho watakipata chenye nafuu cha kumwezesha kujikimu yeye mwenyewe na familia yake” Bw. Max amesema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TUCTA mkoa wa Singida, Bw. Emmanuel Misholi, amesema kikokotoo kilichotangazwa awali kilikuwa ni JENEZA lililoandaliwa kwa ajili ya watumishi wanaotarajiwa kustaafu.

“Kwa kweli Rais Magufuli ni kiongozi msikivu mno amesikia kilio chetu na kuchukua hatua stahiki. Binafsi nina furaha na amani moyoni haijawahi kutokea. Sisi kama watumishi wa umma, hatuna zawadi ya kumpa Dkt. Magufuli isipokuwa ni kuchapa kazi na kukidhi mahitaji ya Watanzania wote bila ubaguzi” amesema Misholi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amempongeza Rais kwa uamuzi wa busara, huku akiwataka watumishi wa mkoa wa Singida kuendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais Magufuli kwa kufanya kazi kwa bidii zaidi ili kuleta ufanisi.

Mkuu huyo wa mkoa wa Singida, amewataka watumishi wa umma mkoani hapa kutumia furaha yao na amani waliyoipata baada ya kikokotoo kufutwa, kuongeza bidii ya kazi mara dufu katika kuitumikia Serikali na Watanzania ikiwa ni kumshukuru Rais Magufuli kwa kusikia kilio chao hicho cha muda mrefu.

Aidha, Dkt. Nchimbi amewaagiza wakuu wote wa idara, vitengo na viongozi wengine mkoani Singida, waendelea kuwa karibu na watumishi walio chini yao, na tabia ya kukemea, kuwatishia, isiwepo ili kumfanya mfanyakazi kuwa na amani wakati wote awapo kazini.

“Wafanyakazi, jambo hili ambalo mmelitambua na kuja kulisherekea leo kwa maandamano ya amani kwa ajili ya kumpongeza na kulitolea shukrani kwa Mheshimiwa Rais Magufuli ni jambo kubwa sana kwa uhai na uhai endelevu wa utumishi wetu na matunda ya kazi zetu”

“Hakika hakukukuwa na namna nyingine yoyote ya kusema isipokuwa ni kutoka na kusema hongera mheshimiwa Rais asante sana kwa haya yote uliyotufanyia na hasa la kutuondolea tatizo hili la kikokotoo… hongera mheshimiwa Rais Magufuli”.

“Waheshimiwa sana wafanyakazi, mnahaki tena mnahaki sana ya kumpongeza Rais na hata mngeamua kushinda kutwa nzima hapa kwa kumpongeza Rais mnahaki, na msiishie hapa endeleeni kumpongeza popote pale, hata mkiwa kwenye madawati yenu endeleeni kumpongeza. Hili la kikokotoo hili, sio letu ni la familia zetu na taifa kwa ujumla” amesema Dkt. Nchimbi kwa furaha tele.

Awali akizungumza baada ya kupokelewa maandamano, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Bw. Juma Kilimba, aliwaomba watumishi wa umma kufanya kazi karibu zaidi na Serikali yao ili kuunga mkono utekelezaji wa sera za Chama Cha Mapinduzi.

Kanuni ya kikokotoo kipya kilichokuwa kinalipa asilimia 25 ya mafao ya watumishi, kililalamikiwa sana na kupingwa na wadau wengi nchini, hali iliyomlazimu Rais Magufuli kuingilia kati na kurejesha utaratibu wa zamani.

Maandamano haya yameaandaliwa na chama cha wafanyakazi TUCTA mkoa wa Singida kwa ushirikiano na vyama vya CWT, TUICO, TALGWU, TUGHE, RAAWU pamoja na TAMICO kwa lengo la kumshukuru na kumpongeza Rais Magufuli kwa uamuzi wake wa kufuta kikokotoo.


Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.