• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Wajibu wa serikali kutekeleza maoni na changamoto za wananchi

Posted on: April 1st, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, Suleiman Mwenda amewaeleza wananchi kuwa ni wajibu wao viongozi kueleza yale ambayo serikali imeyafanya na kwa nini imeyafanya kwa ajili ya wananchi ambao inaowaongoza.

Mwenda alibainisha hayo leo Alhamisi Machi 31, 2022 punde baada ya kukagua miradi ya maendeleo katika kata nne za Tarafa ya Kisiriri wilayani hapa akiwa na kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kamati ya Usalama wilaya kuelezea mafanikio ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ndani ya mwaka mmoja.

“Ni wajibu wetu wa msingi kutekeleza maoni na matarajio ya wananchi ambayo ndio vipaombele vyao.” Alisema Mwenda

Aidha, aliongeza kuwa wananchi huelezea kuwa wanayoshida ya maji, barabara na umeme ambapo serikali huyafanyia kazi na hivyo kuwa wajibu wa serikali kurudi kwa wananchi kuwaeleza yale ambayo serikali imefanya na kwa nini imefanya.

“Ndugu zangu wananchi! serikali inayoongozwa na Rais Samia imetekeleza miradi mingi na yenye thamani ya mabilioni  ambayo leo nimeikagua na sasa imenilazimu  kuwaeleza yale ambayo Rais Samia ameyatekeleza kupitia Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM).”

Baada ya kuelezea miradi ya afya, maji, elimu, barabara na umeme iliyotekelezwa katika kila kata na yenye tahamani ya mabilioni, Mwenda alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha wananchi mambo ya msingi yaliyombele ya wananchi kwa sasa.

Aliwakumbusha wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa vijana waliopata ajira za muda kwa ajili ya kukusanya na kuweka namba ili kukamilisha mfumo wa anwani za makazi.

Halikadhalika, aliwataka wananchi na viongozi kuanzia ngazi ya kijiji na wilaya kuendelea kujiandaa na sensa ya watu na Makazi inayotarajiwa kufanyika ifikapo Augosti mwaka huu.

“Ndugu zangu tujiandae kwa ajili ya kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi, tutoe changamoto na kuhakikisha kuwa zile kamati zinakutana na kuweza kuibua changamoto za awali ili serikali izipatie ufumbuzi kwa lengo la kufanikisha zoezi la sensa ya watu na makazi.”

Mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan akiwa madarakani, wananchi mbalimbali katika maeneo tofauti tofauti wameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuwajali wananchi kuwaletea miradi katika kila sekta.

Akiongea na wananchi wa kijiji cha Tyegelo kata ya Kidaru wilayani Iramba Diwani wa kata hiyo, Philipo Manguli alisema kuwa wanakila sababu ya kumshukuru Rais samia kwa kuwaletea miradi ya kihistoria.

“Kwa kweli miradi hii ni yakihistoria katika nchi yetu, hivyo ndugu zangu wananchi ni wakati sasa tuunge mkono kwa dhati juhudi za Rais wetu Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo anatekeleza vipaombele vyetu.” Alishukuru Manguli

Kwa upande wake mmoja wa wananchi wa kijiji cha Tyegelo kata ya Kidaru, Salumu Mohamed alimshukuru Rais Samia kwa sababu maendeleo ya ujenzi wa kituo cha afya yamekuwa mkombozi wa kupunguza vifo vilivyokuwa vikitokea kutokana na umbali wa Hospitali.

“Sasa hivi hatuna shida maana hapo awali tulikuwa tunaangaika sana na wengine kupoteza maisha kwa kukosa tiba mapema.”

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.