Wakuu wa Wilaya Suleiman Yusuph Mwenda (Iramba), Remidius Mwema Emmanuel (Kiteto), Michael John Semindu (Mbulu) walipata heshima maalum ya kutoa Mhadhara katika Chuo Kikuu Cha Kilimo nchini China (China Agricultural University - CAU) kitivo cha “Humanities and Management Studies “
April 13,2025 Wakiwa chuoni hapo, viongozi hao walipata fursa ya kutoa Mhadhara kwa wanafunzi kutoka Tanzania na mataifa mengine (CAU - International Students) pamoja na menejimenti ya chuo hicho.
Viongozi hawa watatu (3) walikuwa wanafunzi katika chuo hicho wakisoma shahada ya Uzamili “Rural Development and Management Studies” takribani miaka nane (8) data,Kufika kwao chuoni hapo katika kipindi hiki ni kumbukumbu muhimu na kutambua wao kama “CAU Alumni” kutoka nchini Tanzania.
Profesa Tang Lixia ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa ofisi ya mahusiano ya ndani ya chuo ( Deputy Director of office for the domestic Cooperation at China Agricultural University - CAU) wakati akiwasilisha salamu zake kwa niaba ya chuo alisema; “wakati wote viongozi hao wametambulika kama wahitimu wa mfano na mahiri (Outostanding Graduates) ambao wamewahi kusoma chuo kikuu hapo, na mara zote wametumika kama wanafunzi kwa wanafunzi waliopo chuoni hususani wanafunzi wa kimataifa”,
Mapema. wakati wa siku rafiki, Katibu Msaidizi wa CPC ( Deputy Party Secretary) kutoka chuo hicho Comrade WANG Yang amesema China inajivunia mahusiano na Afrika yote na akifanya kazi kwa muda mrefu katika ushirikiano wa Tanzania na wote wa CPC ( Deputy Party Secretary) mahiri wa Mhe. Xi Jinping (Rais wa China) na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan (Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania).
Wakuu wa Wilaya hao kwa sasa wako Jijini Beijing nchini China kwa ziara maalum ya mafunzo, ambapo pamoja na mambo mengine wanajifunza mfumo wa Utawala na Mageuzi ya historia ya Umma kwa nchi za Afrika (Reform and Governance of State - Owned Enterprises for African Countries ) ikiwa ni pamoja na kutembelea na kupata uzoefu wa majimbo kadhaa nchini humo hatua inayolenga kuagiza mageuzi ya nchi za Afrika.
KIOMBOI, IRAMBA
Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA
Simu: 026 - 2532253
Simu: 026 - 2533001
Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz
Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.