• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Wanafunzi wa Iramba wamewazidi wanafunzi wa Wilaya ya Ikungi na Manyoni matokeo ya mafunzo ya BONGA na TVET yanayoendeshwa na Shirika la SEMA.

Posted on: March 11th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni ametoa ahadi mbalimbali kwa wahitimu wa mafunzo ya BONGA na TVET yaliokuwa yakiendeshwa na Shirika la SEMA kata ya Ulemo na Kinampanda.

Ahadi hizo zimetolewa leo Alhamisi Machi 11, 2020 wakati wa mahafali ya wahitimu wa BONGA na TVET katika ukumbi wa Profesa  Majule uliopo kata ya Kinampanda Wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

Akiongea na Wahitimu hao, Mwageni amewaambia kuwa kama hawatoyaingiza mafunzo hayo katika utendaji yatakuwa hayana maana huku akiwataka kuunda vikundi ili wapate sifa ya kupata mikipo inayotolewa na Halmashauri hiyo.

“ Niwaombe mtambue kuwa pesa za kuwakopesha tunazo, hivyo watakokamilisha usajili wao kwa wakati watapatiwa mikopo ya mwaka huu,” amesema Mwageni na kuongeza

 

“ Mtumie fursa ya uwepo wa stendi mpya ya mabasi Misigiri kwenda kuzindua utoaji wa huduma mbalimbali ikewemo chakula kwa wasafiri watakaokua wanapita  hapo.”

Mwageni amewaahidi wahitimu waliohitimu mafunzo ya kuchomelea kuwapatia chumba watakachotumia shunghuli zao kwa kipindi cha mwaka mmoja bila kulipa pesa ya pango eneo la ulemo.

Kwa wale waliohitimu mafunzo ya kilimo na ufugaji, Mwageni amewaahidi kuwapatia mbegu za viazi lishe, mbegu za matunda ya pensheni na Viriba kilo 10 kwa ajili ya kuotesha mipapai ya kisasa na yakienyeji huku akiwataka kutumia fursa hiyo kuwa mawakala wa kuzalisha na kuuza mbegu.

Halikadhalika Mwageni amewaasa wahitimu hao kufanya shughuli za halali ili kupata pato la halali huku akiwaonya kujiingiza kwenye tabia za utapeli kwa lengo la kupata utajiri wa haraka.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la SEMA, Ivo Manyaku amesema kuwa jumla ya wahitimu 295 kutoka katika Wilaya ya Manyoni, Ikungi na Iramba wamehitimu mafunzo hayo.

Manyaku amesema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba imekua yakwanza kwa kuwa na wahitimu 115 ukilinganisha na wale waliohitimu kutoka Wilaya ya Manyoni na Ikungi.

Aidha Mkurugenzi wa SEMA amewaahidi wahitimu hao wakikamalisha uundaji wa vikundi na usajili atawapatia vifaa vya kufanyia kazi.

Naye mmoja wa wahitimu kutoka  kata ya ulemo, Monica Zakayo amesema kuwa mafunzo hayo yamewajengea ujasiri wa kujitambua ,kujiamini na kufanya maamuzi sahihi.

Zakayo amesema wameweza kupata ujuzi wa upambaji, uchomeleaji, ususi wa saluni na urembo, upishi, kilimo na ufugaji, ufundi wa pikipiki na ufundi wa umeme, hivyo kuwawezesha kutengeneza sabuni za maji ya mikono, kufulia, sabuni za kuondoa mabaka, kupika vyakula mbalimbali , kupamba kumbi mbalimbali na kilimo cha mbogamboga ambavyo vimewapatia mwanga na matumaini ya maisha.

Kwa upande wake mmoja wa wazazi, Izrael Mkumbo ameushukuru uongozi wa serikali na Shirika la SEMA kwa kukubali mradi huo kufanyika kata ya Ulemo na Kinampanda na kuwataka wahitimu hao kuyafanyia kazi yale yote waliojifunza.

Mradi wa BONGA na TVET ni programu inayoendeshwa na Shirika la SEMA linalowalenga vijana wa kike na kiume (13 – 30) walionje ya mfumo wa elimu ili kuwapatia stadi za maisha kuhusu usafi, baleghe na ujana, haki za wanawake, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia na elimu ya ujasiriamali.

Mafunzo hayo yalianza July mwaka jana na kuhitishwa Mach 2020.

SMWISHO

Mkurugenzi wa Shirika la SEMA akiwaasa wahitimu wa mafunzo ya BONGA na TVET yaliofanyika katika ukumbi wa Profesa Majule Kinampanda Wilayani Iramba. Picha Hemedi Munga

Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Gene Ng’ondi akiwaasa wahitimu wa  mafunzo ya BONGA na TVET yaliofanyika katika ukumbi wa Profesa Majule Kinampanda Wilayani Iramba. Picha Hemedi Munga

Wahitimu wa mafunzo ya BONGA na TVET waliopata ujuzi wa ususi na urembo wakionesha ujuzi wao wa ususi wa nywele katika mahafali yaliofanyika katika ukumbi wa Profesa Majule Kinampanda Wilayani Iramba. Picha Hemedi Munga

Wahitimu mbalimbali wa mafunzo ya BONGA na TVET wakifuatilia mada mbalimbali za viongozi wakati wa mahafali yaliofanyika katika ukumbi wa Profesa Majule Kinampanda Wilayani Iramba. Picha Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.