• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

WANANCHI IRAMBA WANUFAIKA NA HATI MILIKI 1711 KUPITIA MRADI WA UKIJANI UNAOTEKELEZWA NA HELVETAS

Posted on: February 4th, 2025

WANANCHI IRAMBA WANUFAIKA NA HATI MILIKI 1711 KUPITIA MRADI WA UKIJANI UNAOTEKELEZWA NA HELVETAS


Zaidi ya wananchi 1,700 katika Wilaya ya Iramba wamepata hati miliki za kimila kupitia Mradi wa UKIJANI, unaotekelezwa na shirika la Helvetas kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania. Hafla ya ugawaji wa hati hizi imefanyika Februari 4,2025 Wilayani Iramba, ikihudhuriwa na viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo, na wanufaika wa mradi. Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Mkoani Singida Suleiman Mwenda.


Katika hotuba yake, DC Mwenda amewashukuru waandaaji wa hafla hiyo na kusisitiza umuhimu wa umiliki wa ardhi kwa maendeleo ya wananchi. Alisema hati miliki hizo 1,711, ambazo kati yake 1,077 zinamilikiwa na wanawake, zitachochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa kuimarisha usalama wa ardhi, kuongeza thamani ya umiliki, na kupunguza migogoro ya ardhi.


"Napenda niwapongeze wananchi, mamlaka za vijiji, halmashauri ya wilaya, na wadau wote waliohusika katika mchakato huu. Hii ni hatua kubwa katika kuhakikisha usalama wa milki za ardhi na kuleta maendeleo endelevu," Amesema DC Mwenda.


Mchakato wa Upatikanaji wa Hati Miliki

Mradi wa UKIJANI umetekelezwa katika vijiji vitano vya Mbelekese, Kikonge, Usure, Kinkungu, na Tyeme, vilivyopo katika kata za Mbelekese na Mtoa. Mchakato wa uwezeshaji ulijumuisha hatua tatu kuu:


Kwa upande wake Meneja Mradi wa Ukijani Bi. Shoma Nangale amesema kuwa Ukusanyaji wa Taarifa za Upimaji Maombi ya umiliki wa ardhi yalikusanywa na wataalamu wa upimaji kwa kushirikiana na timu za mipango ya matumizi bora ya ardhi.

Uandaaji wa Hati Miliki– Taarifa zilihakikiwa na hati miliki kuchapishwa kupitia mfumo wa kisasa wa kidigitali, ambapo hekta 2,408.29 za ardhi zilipimwa na kusajiliwa.


Announcements

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.