• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Waumini Iramba wamuombea Dua ya Kheri na Mafanikio Rais Samia kumi la mwisho Ramadhani

Posted on: May 1st, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz


Singida - Iramba. Waumini wa dini ya Kiislamu na Kikistro wilayani Iramba mkoa wa Singida wamemuombea dua ya Kheri na mafanikio ya kuliongoza Taifa la Tanzania Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Maombi hayo yamefanyika katika ukumbi mkubwa wa Mikutano ya Halmashauri ya wilaya hiyo katika hafla fupi ya kufuturisha waumini iliyoandaliwa na Mkuu wa wilaya hiyo kwa kushirikiana na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo mjini hapa.

Akiongea katika hafla hiyo, Shekhe Mkuu wa Msikiti wa Taqwa mjini Kiomboi na Makamu mwenyekiti wa Kamati ya Amani, Al haji Shekhe Omari Hassan aliwakumbusha waumini hao kuwa Ramadhani ni utakaso kwa kila mwanadamu kujisafisha kuanzia nafsi, mwili, mavazi na matendo yake.

Akinukuu maneno matakatifu toka katika kitabu kitukufu cha qur an, Shekhe Hassan alisema kuwa wanaadamu wamefaradhishiwa kufunga kama vile walivyofaradhishiwa waliokuwa kabla yao.

Aidha, Shekhe Hassan alifafanua kuwa swala la kufunga litakuwa lilianzia toka kwa Mtume Adam (A.S) mpaka kwa Mtume Mohammad (S .W. A), hivyo ndio maana ibada ya funga wanaifunga kwa nguvu kubwa.

Kufuatia Ibada hiyo kuwa katika kumi la mwisho katika Mwezi wa Ramadhani, Shekhe Hassan aliiombea dua Nchii hii iendelee kuwa na amani na salama muda wote.

Aidha, aliwaombea Viongozi wote akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuendelea kuwa na afya njema, msimamo, amani, upendo na makazi mema kwa ajili ya kuitengeneza nchi hii isijeyumba.

“Ewe Mwenyezi Mungu tunakuomba mjalia Rais Samia Suluhu Hassan aendelee kuwa na ujasiri, umahiri, nguvu na ukakamavu wa hali ya juu na uumuongezee busara, kumzidishia elimu na ufahamu wa kuliongoza Taifa hili kwa uadilifu.” Aliomba al haji Hassan na kuongeza kuwa

“Tukiwa katika kumi la mwisho la Mwezi wa Ramadhani tunaomba dua yetu utukubalie Ewe mwenyezi Mungu!”

Kwa upande wake Katibu Msaidizi wa Kamati ya Amani ya wilaya hiyo mchugaji wa Kanisa la KKKT, Elitegemeo Mpumpa alisema kuwa thamani ya mtu ipo pale mtu anapofunguliwa kutoka kwenye ubinafsi, hivyo alimuomba Mkuu huyo wa wilaya kuendelea na moyo huo wa kuwakutanisha viongozi hao.

Akinukuu maneno matakatifu toka katika kitabu cha Zaburi ya 133 mstari wa kwanza, Mchungaji Mpumpa alisema kuwa Tanzama jinsi ilivyo vyema na kupendeza ndugu wakae pamoja kwa umoja, hivyo katika kikao hichi lipo jambo la kimungu ambapo Mungu amependezwa kuona wao wamekaa pamoja bila ya kujali dini zao.

“Kwa kweli jambo hili ni jema na lakiibanda ambalo linampendeza Mungu, hivyo tunakuomba Mkuu wa Wilaya uendelee na Moyo huo huo.” Alisema

Aidha, alimpongeza na kuahidi kuendelea kumuunga mkono Rais Samia kwa namna ambavyo anaendelea kuiongoza nchi na maendeleo makubwa anayoyaleta huku akitolea mfano wa barabara ya Ruruma iliyopo Mji mdo wa Kiomboi wilayani hapo ambapo awali barabara hiyo ilikuwa ni makorongo tu lakini sasa imetengenezwa watu wanapita bila shaka kabisa.

Akiongea katika hafla hiyo fupi Mkuu wa Wilaya hiyo, Suleiman Mwenda aliwaasa waumini hao kuwa wao ni watu wa Taifa moja, hivyo wanapaswa kuendelea kuvumiliana na kuishi kwa upendo na kushirikiano kwa amani.

Hata hivyo, Mwenda aliwakumbusha kuwa kusanyiko hilo ni utamaduni wa Kitanzania na Afrika kwa ujumla kuwa watu wakakaribishana na kula chakula pamoja.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Michael Matomora alitumia hafla hiyo kuwaomba waumini na viongozi wa dini kuwahamasisha waumini na wananchi waliowazunguka kuweka vibao kwa taratibu, vipimo na gharama zilizopo kwa watendaji wa vijiji.

“Nitumie fursa hii kuwaomba Viongozi na waumini kutumia majukwaa yetu kuwahamasisha watu kutekeleza hili na kujiandaa na zoezi la sensa.” Alisema

Aidha. Aliongeza kuwa kukamilika kwa Mfumo wa Anwani za Makazi kutarahisisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.