• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

WAZAZI WILAYA YA IRAMBA WATAKIWA KUHAKIKISHA WANAWAPELEKA WATOTO WAO KUPATA CHANJO ILI KUWAKINGA NA MAGONJWA YANAYOZUILIKA KWA CHANJO

Posted on: December 17th, 2024


Wazazi Wilaya ya Iramba Mkoani Singida wametakiwa kuhakikisha wanawapeleka Watoto wao kwenye Vituo vya kutolea huduma za Afya kwa wakati ili wapate chanjo dhidi ya magonjwa yanayozuilika kwa chanjo.


Wito huo umetolewa Disemba 17, 2024 na Afisa Tarafa, Tarafa ya Kisiriri Bw. Oswald Leopord kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Suleiman Yusuph Mwenda wakati akizungumza katika uzinduzi wa Wiki ya Chanjo uliofanyika kwenye Zahanati ya Bomani.


Aidha Oswald ametoa rai kwa wazazi pamoja na walezi kuhakikisha watoto walio chini yao wamepata chanjo zinazotakiwa kwa wakati ili kuwakinga dhidi ya magonjwa hatari na kuachana na Imani potofu kuhusu chanjo.


"Nitoe rai kwa wazazi wote kuhakikisha watoto wote wanapata chanjo zinazotakiwa kwa wakati kama tunavyoelekezwa na wataalamu ili kuwakinga watoto dhidi ya magonjwa hayo hatari kama vile Surua na Polio....zamani watu walikuwa wakipata matatizo kwa sababu ya kutochanja kwa sababu ya Imani potofu. Tuachane na imani potofu tuwapeleke watoto wapate chanjo." Alisema Oswald Leopord


Kwa upande wake kaimu Mganga mkuu Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Daniel Paul Nkingo amesema Lengo la uwepo ya wiki ya chanjo na mwezi wa matone ya Vitamini A ni kuendelea kukumbushana na kuhamasishana kuhusu umuhimu wa chanjo katika jamii, kuwa fatilia na kuwaibua watoto walioasi chanjo na ambao hawakupata chanjo tangu kuzaliwa kwa sababu zozote zile ili waweze kupata chanjo na kuwaepusha na magonjwa yote yanayozuilika kwa chanjo, kuwapatia matone ya nyongeza ya Vitamini A pamoja na upimaji wa hali za Lishe kwa watoto wenye umri wa miezi 6-59.


"Lengo ni kuwakinga dhidi ya magonjwa ya mlipuko yanayoweza kuzuiliwa na chanjo. Na tunaendelea kutoa Elimu na kuwaibua ambao hawajapata chanjo na walioasi chanjo ili wapate chanjo, kwa kufanya hivyo tunaamini Jamii yetu itakuwa imekingwa." Alisema Daniel Nkingo


Naye Mratibu wa chanjo Wilaya ya Iramba Jackson Shango Shillah amesema kuanzia January 2023 Hadi Novemba 2024 jumla ya watoto 1918 wameasi chanjo na zoezi hili litahusisha kuhakikisha wamepata chanjo.





Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.