• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Waziri Jaffo aipongeza Singida mchakato wa uchaguzi serikali za mitaa

Posted on: November 7th, 2019

By Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba.  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jaffo ameupongeza Mkoa wa Singida kwa kuwa miongoni mwa mikoa mitano  nchini kwenye zowezi la uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019.

Jaffo ameyasema hayo leo Jumatano Novemba 06, 2019 akiwa Mkoani Singida kukagua utekelezaji wa kanuni na taratibu za uchaguzi wa serikali za mitaa unaoendelea Nchini.

Pia amewapongeza wakazi wa Mkoa wa Singida kwa kuhamasika kujitokeza kwa wingi kitakwimu katika zoezi la uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga kura.

Akiongea katika ziara hiyo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jaffo amesema uandikishaji wa Daftari la Kudumu ni moja ya hatua muhimu ya mchakato wa serikali za mitaa.

“ Katika zoezi la uandikishaji Singida ni miongoni mwa mikoa mitano  iliyofanya vizuri, na kwa wagombea tayari mfululizo wa siku 7 tumekamilisha zoezi la kuchukuwa na kurudisha fomu na hatimaye kufanya teuzi za wenyeviti na wajumbe wa kamati za rufaa,” alisema Jaffo

Waziri Jaffo amezitaka kamati zote za rufaa nchini kuhakikisha wanasimamia haki na usawa kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo iliyopo bila ya kumuonea mtu yoyote wakati wa maamuzi.

“Azma yetu sote ni kuona uchaguzi huu unakwenda vizuri na unakamilika kwa lengo la kuunda mamlaka za serikali za mitaa ambazo zinajibu matatizo makubwa ya wananchi,” aliongeza Jaffo

Akibainisha umuhimu wa zoezi la uchaguzi wa serikali za mitaa, Jaffo amesema uchaguzi huo unatengeneza serikali za mitaa zilizo karibu na wananchi, ambapo Taifa likitoa ajenda zozote za maendeleo basi utekelezaji na msingi wa maendeleo unatoka chini.

Jaffo amewataka wananchi kufahamu kuwa kwa mujibu wa kanuni zilizopo, “Kamati ya Rufaa ya Wilaya” inayoundwa na Katibu Tawala wa Wilaya (DAS) ambaye ndiye mwenyekiti  na  kusaidiwa na wajumbe wanne ambao ni watumishi wa sekta za umma kutoka wilaya zote ndani ya mkoa huku katibu wa kamati hiyo anatoka ndani ya sekta ya umma na ataruhusiwa kupiga kura.

“Mwenyekiti nendeni mkazingatie haki, sikilizeni rufaa na malalamiko yote yatakayotolewa mezani kutoka vyama vyote na watu wote kwa uhuru na upana wake bila kuingiliwa na mtu yoyote,” alisisitiza Jaffo

Akisisitiza mbele ya wajumbe wa kamati ya rufaa mkoani Sin gida Tanzania, Jaffo amewaambia wajumbe hao watende haki na wasiogope.

“Mmepewa rungu lisilokuwa na mashaka , tendeni haki msiogope, hakikisheni kila kitu kinanyooka, kama kuna mtu anastahili haki mpeni haki yake na kama kunakasoro zirekebisheni,” aliongeza Jaffo

Kufuatia mchakato mzima wa uchaguzi wa  serikali za mitaa kuendelea nchini Waziri Jaffo amelitaka jeshi la Polisi kupitia makamanda wa mikoa kuendelea kusimamia utaratibu uliowekwa kwa misingi ya amani na kamwe mtu yoyote asijitokeze kuchafua mchakato wa uchaguzi unaoendelea kwa maslahi yake binafsi.

Akiongea katika ziara hiyo Mwenyekiti wa kamati ya Rufaa ya Wilaya ya Singida DC mkoani hapo, Wilson Shimo, amesema kuwa wamejipanga kusikiliza malalamiko na rufaa zote kwa haki na kurekebisha kwa mujibu wa kanuni zinazowaongoza na kuweka wazi kuwa mpaka jana walikuwa hawajapokea malalamiko yoyote.

Naye mjumbe wa kamati hiyo, Patrick Zamba amesema kuwa  watajitahidi kutoa maamuzi sahihi kwa muda mwafaka kwa mujibu wa sheria na kanuni.

Akiongea katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt, Rehema Nchimbi amesema siku njema daima huonekana asubuhi huku akibainisha kuwa hatua ya mkoa huo kupokea hati ya ushindi na kuwa miongoni mwa mikoa mitano bora ni ishara njema.

“Singida ni njema, tena ni njema na ni njema sana ! na asubuhi hii njema ndio itabeba mchana wote kuwa mwema zaidi, kwa hatua zote mpaka kukamilika kwa mchakato mzima wa uchaguzi huu muhimu,” alisema Nchimbi

.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.